Wakati mwingine Watanzania wenzangu huwa atutafakali kwa kina matukio fulani fulani! Siku za nyuma nuliwahi kuhuliza swali dogo, nilisema hivi " Kwa nini Mzee Wassira alipigiwa kura nyingi pale Kizotta kuwazidi Mh.Dk JK na Mh.Dk Shein??" Kwa akili za kawaida kulikuwa na ulazima gani wa yeye kupigiwa ndio kura zote, wakati wenzake kuna kura ziliwakataa!! Mzee Wassira hata angepata nusu ya kura angeweza kuchaguliwa tu kwenye kamati kuu, sasa hii landslide ilikuwa inahashiria nini siku za usoni? Alitumia mbinu gani kuwapiku wenzake wote pale ukumbini. Je kampeini alifanya saa ngapi wakati muda wote alionekana ametulia kwenye kiti chake hana papala wala wasi wasi. Nikiona baadhi ya wana JF wanambeza beza nawashangaa sana, mimi sio mtume wala nabii lakini nina uhakika kwamba kadiri siku zinavyo sogea karibu na kampeini/Uchaguzi 2015 Mzee Wassira atawashangaza wengi. Hajatangaza nia, lakini nionavyo mimi it's a question of TIME.