Mtumaini Mungu
JF-Expert Member
- Aug 3, 2021
- 879
- 1,061
Ee Bwana, Mtakatifu Mungu wetu sifa na utukufu ni Mali Yako nami kwa unyenyekevu mkubwa navirejesha kwako Sasa na hata Milele.
Ndugu watanzania wenzangu, hapa karibuni zimetolewa nafasi nyingi za ajira katika vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, kuanzia Jeshi la Polisi Tanzania chini ya Afande IGP Simon Sirro, Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Hata idara ya uhamiaji.
Cha kushangaza ni kuwa wale ambao miaka ya nyuma walikuwa wanaukimbia huu "mgari" wa majeshi kutokana na shuruba na ugumu wa kazi leo hii wanaulilia na kuponda kuwa kwanini ajira hizi zinatolewa kwa waliofeli?
Wapo watu ambao wamefika mbali na kuanza kuyaponda majeshi yetu kuwa yanapoteza muelekeo kwa kuchukua vijana waliofeli kidato cha nne, Mimi naomba niwaulizeni Kwani hapo zamani majeshi yalikuwa hayachukui watu waliofeli? Watu wa darasa la saba?
Kazi za Majeshi ni kazi ambazo msingi wake mkuu ni "AMRI".. Hao waliofeli wanaenda huko kufanya kazi kwa kufuata amri, Na hata Ukichukuliwa wewe msomi bado utahitajika kufuata AMRI za wakuu wako bila kujali PHD yako ya kwenye vyeti.
Msomi ukiingia huko kwenye Majeshi bado huna nafasi ya KUHOJI au KUFANYA MAMBO kinyume na Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa, ni Lazima ufate Amri Kama ilivyo kwa Wale waliofeli.. Bila shaka kwa sasa vijana wanaohitajika ni wale ambao kazi na majukumu yao yanalandana na elimu zilizo ainishwa, watakapo hitaji wenye elimu za juu au za fani/taaluma tofauti na hizo zilizo ainishwa watawaita.
Ushauri wangu kwa waziri anayehusika na masuala ya kazi na ajira, Huku mtaani kuna wahitimu wengi na hawana ajira, tengenezeni mifumo ya kuwatumia hawa vijana ili kuipa thamani elimu yao na kurudisha kile walichokitumia kuitafuta hiyo elimu.
Nyie vijana wenzangu, wenye four zile za mwisho mtakaopata nafasi huko majeshini.. Ushauri huu mmepewa na YESU KRISTO WA NAZARETH...
Luka 3:14
"Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu."
Ee Mungu Uturehemu sawasawa na wingi wa Fadhili Zako.
Ndugu watanzania wenzangu, hapa karibuni zimetolewa nafasi nyingi za ajira katika vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, kuanzia Jeshi la Polisi Tanzania chini ya Afande IGP Simon Sirro, Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Hata idara ya uhamiaji.
Cha kushangaza ni kuwa wale ambao miaka ya nyuma walikuwa wanaukimbia huu "mgari" wa majeshi kutokana na shuruba na ugumu wa kazi leo hii wanaulilia na kuponda kuwa kwanini ajira hizi zinatolewa kwa waliofeli?
Wapo watu ambao wamefika mbali na kuanza kuyaponda majeshi yetu kuwa yanapoteza muelekeo kwa kuchukua vijana waliofeli kidato cha nne, Mimi naomba niwaulizeni Kwani hapo zamani majeshi yalikuwa hayachukui watu waliofeli? Watu wa darasa la saba?
Kazi za Majeshi ni kazi ambazo msingi wake mkuu ni "AMRI".. Hao waliofeli wanaenda huko kufanya kazi kwa kufuata amri, Na hata Ukichukuliwa wewe msomi bado utahitajika kufuata AMRI za wakuu wako bila kujali PHD yako ya kwenye vyeti.
Msomi ukiingia huko kwenye Majeshi bado huna nafasi ya KUHOJI au KUFANYA MAMBO kinyume na Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa, ni Lazima ufate Amri Kama ilivyo kwa Wale waliofeli.. Bila shaka kwa sasa vijana wanaohitajika ni wale ambao kazi na majukumu yao yanalandana na elimu zilizo ainishwa, watakapo hitaji wenye elimu za juu au za fani/taaluma tofauti na hizo zilizo ainishwa watawaita.
Ushauri wangu kwa waziri anayehusika na masuala ya kazi na ajira, Huku mtaani kuna wahitimu wengi na hawana ajira, tengenezeni mifumo ya kuwatumia hawa vijana ili kuipa thamani elimu yao na kurudisha kile walichokitumia kuitafuta hiyo elimu.
Nyie vijana wenzangu, wenye four zile za mwisho mtakaopata nafasi huko majeshini.. Ushauri huu mmepewa na YESU KRISTO WA NAZARETH...
Luka 3:14
"Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu."
Ee Mungu Uturehemu sawasawa na wingi wa Fadhili Zako.