Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,777
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, amesema kauli ya “No Reforms No Election” inayopigiwa chapuo na baadhi ya vyama vya upinzani si hoja ya kisiasa, bali ni wito wa makusudi wa kuvuruga amani na kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika wilayani Sengerema Juni 24, 2025, Wasira alisema wito huo unawachochea wananchi hususan vijana, wazee na wanawake kuacha shughuli zao halali na kushiriki katika vitendo vya fujo kwa lengo la kuzuia uchaguzi, jambo ambalo ni kinyume cha sheria na taratibu za nchi.
Akizungumza katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika wilayani Sengerema Juni 24, 2025, Wasira alisema wito huo unawachochea wananchi hususan vijana, wazee na wanawake kuacha shughuli zao halali na kushiriki katika vitendo vya fujo kwa lengo la kuzuia uchaguzi, jambo ambalo ni kinyume cha sheria na taratibu za nchi.