Wasikilizaji wa Radio Imani: Ole wake atakayewalisha watoto wetu mchele wa msaada wenye virutubisho

Migalatia hii itatuharibia nchi na uzwazwa wao, kila kitu inakubali imeletewa ushoga wameupokea na sasa wanaletewa mchelemchele midenda inawatoka
 
Hata kama unaweza kuwa umeandika vizuri , je wizara ya Elim hawajui? Kama wanajua kwanini isipangwe bajet kutoka kwenye tozo nakupeleka vyakula mashuleni mpaka subili letewa mchele wa virutubisho toka Ulaya?

Kwamba sasa mpaka NGO kwa kushirikiana na mataifa ya nje ndo waje na vyakula vya kusaidia wanafunzi ,serikali , wizara husika kazi yake nini?

Ipo misaada ya kupewa ila sio mchele, maharage au aina nyingine ya nafaka
Mkuu;
1. Hivi ww huwa unakubali kula chakula kwa kuangalia au kupata taarifa kwamba kimetolewa na nani na kutoka wapi?
Je, huko hotelini au kwa mamalishe huwa kabla ya kula unauliza kwamba ugali samaki au wali maharage vimetoka wapi?
2. Duh! Unataka kila kitu Serikali / Wizara ifanye na ndo maana wapo ambao hawataki kuchangia chakula cha watoto wao wanafunzi shuleni hadi watoto hao wameathirika kwa Utapiamlo mkali. Hii sio sawa. Unatakiwa uwajibike sehemu yako na Serikali itawajibika panapohusika. Je, Serikali ilikusaidia kuzaa? Umemzaa mtoto unapswa kumlea- Kumbuka mtoto ana Haki zake na mojawapo ni kupewa chakula.
2. Ni misaada ipi ukipewa utapokea kwa mfano.
 
Hoja yao inaongozwa na wasiwasi na ni mufilisi. Tunaletewa misaada ya madawa,chanjo, condom , vyandarua n. K mbona hawalalamiki. Ishu ya ushoga mwenye nguvu akiamua juu ya watu wajinga na wasioweza hata kujilisha atafanikiwa hata kama si kwa kuleta mchele.
 
Lakini mbona kama wanahoja...chakula tunacho, tunalima wenyewe why watuletee mchele wao??

Wasikilizwe...tusiwe km mazwazwa
Chakula hicho tulicho nacho mbona hatuwapi wanafunzi wanakufaa njaa na kuathiriwa na utapiamlo?
 
Dah! Mkuu, Umechanganya-changanya hoja yako nzuri kiasi kwamba imepoteza mwelekeo wake. Hoja yako ya Raslimali zetu bandari na mbuga za wanyama hazijagawiwa (sio kweli)kwani hakuna mTz aliyetaka kuwekeza huko akakataliwa. Hilo la kuingiza UDINI ni kweli halina Tija.
Lakini pia inafaa uzingatie kwamba hakuna mchele wa kuangamiza nguvu kazi na Uchumi ulioingizwa hapa Tz hoja ya kuleta Udini kwenye jambo hili hoja yako ina mashiko.
Mkuu, Sikukuelewa unaposema mbwa wako kwenye system wanachomekea vi-mada (religious group interests) vya udini.... mi nijuavyo neno Mbwa ni mahsusi kwa wale jamaa (wahusika watanielewa) wako kwenye system na kirefu cha neno hilo humaanisha Management By Walking Around. Hao kamwe hawawezi kufanya kitu hicho ulichowatuhumu nacho - never.
HIvi kwenye yale mambo ya bandari kuna maswali ya wananchi yalijibiwa badala ya kukamata na kuweka ndani? Wakili Mwabukusi na Dr Slaa ni wahanga! Bado unaona ni vyema bandari zote apewe mwekezaji mmoja! Umeuona ule mkataba!?? IGA etc. Kuna mambo yanaendelea hapa nchini! Kila wakati Wananchi wakiamua kupigia kelele kuhofia raslimali au maslahi yao utaona lihoja likija hasa UDINI!
Hebu ona sakata la bandari lilivyotaka kuuliwa kwa UDINI. Tuwape waarabu kwa vile ni waislamu wenzetu/Tusiwape waarabu kwa sababu ni waislamu.

Sualo la Mchele kutoka marekani! HIvyo hivyo
Narudia ni lazima kuna mbwa wa TISS wanaovuruga mijadala ya kijamii hapa!!
 
Migalatia hii itatuharibia nchi na uzwazwa wao, kila kitu inakubali imeletewa ushoga wameupokea na sasa wanaletewa mchelemchele midenda inawatoka
Mkuu kwani nyama za ngamia wanazopewa waislamu kutoka uarabuni zimepimwa? Unajua waarabu wanatia nini kwenye nyama zile?
 
Unajuwa waarabu huwa wanaweka nini kwenye hizo tende mkuu?
Swali langu lilikuwa kama kiwakilishi kwa waziri kuwa je na tende wanazotupa zimepimwa!?
Au ndo wanaamua kutilisha matango pori tu kisa vita ya kibiashara ya wauzaji wa mchele kutupa taharuki kiasi hicho.
 
Hakuna kitu kitapita kiwandani kisiwekwe kirutubisho mkuu..
Swali langu lilikuwa kama kiwakilishi kwa waziri kuwa je na tende wanazotupa zimepimwa!?
Au ndo wanaamua kutilisha matango pori tu kisa vita ya kibiashara ya wauzaji wa mchele kutupa taharuki kiasi hicho.
 
Sakata la mchele wenye virutubisho kutoka Marekani limeendelea kuchukua sura mpya baada ya waislamu kuukataa bila kumumunya maneno. Wakiongea kupitia redio ya kiislamu ya Imaan FM inayounguruma kutokea mkoa wa Morogoro, wamesema hawautaki mchele huo na wametoa tahadhari kwa mtu yeyote atakayewalisha watoto wao. Wamesema chakula wanacho cha kutosha hapa nchini na kushauri waletewe vitu wasivyokuwa navyo kama vile ndege, magari na ambulance.

Ili kuonyesha kuwa hawatanii katika hili, hata watangazaji waliokuwa wakiendesha kipindi walionekana kushabikia kitendo hicho. Mtu yeyote aliyepiga simu kwenye kipindi akionyesha kwenda kinyume na msimamo wao, walimkatia simu mara moja. Hebu wasikilize wewe mwenyewe kupitia klipu hiyo hapo chini.

MAONI YANGU
Huu mchele sasa naona umeanza kutugawa kiitikadi. Wakristo nao wakitoka hadharani na kuweka msimamo wao, hapatatosha. Ifike mahali ubaguzi wa kijinga kama huu ukemewe kwani unaweza kuligawa taifa na kuhatarisha umoja na mshikamano tulio nao hapa nchini. Tusiruhusu kikundi kidogo cha watu kitugawe kwa sababu yoyote ile.

Nawasilisha.
Wakristo hawana huo muda mchafu wa kujadili vitu vya kijinga na kuja kutoa misimamo ya kijinga!
 
Back
Top Bottom