Wasikilizaji wa Radio Imani: Ole wake atakayewalisha watoto wetu mchele wa msaada wenye virutubisho

Hiyo redio ni ya kipuuzi kuwahi kutokea nchini. Hata hao watangazaji wao ni wapuuzi na wakiukaji wa miiko ya utangazaji. Hao waislam ni kina nani duniani/nchini mpaka watoe ole? Ni wapuuzi, wana uhakika gani kama huo mchele ni mbaya? Basi kama ni hivyo watoto wao wasile, watakula wengine na wasilalamike kubaguliwa, shame on them
 
Waislam wako sawa na wana uhuru wa kuukataa huo mchele.
Na Kwa wakristo kama wanaona unawafaa ni fursa nzuri kuchukua chakula cha kutosha wakale na familia zao.

Ila usiseme ni ubaguzi wa kidini maana hamna dini inaitwa marekani, zipo nchi nyingi ambazo hazikubaliani na marekani na siyo nchi za kiislam.
Huko Sudan, Yemen na Somalia kwenye waislam wa kutosha wanakula mchele wa Mamarekani. Gaza unashushwa kwa maparashuti watu wanaugombea ..... Tanzania maskini jeuri. Kuna watu hajui kuwa Tanzania almost 40 % ya watoto wamedumaa kwa ajili ya kukosa lishe bora. Yaani watoto wapate utapia mlo kwa vile tu wanasubiria mchele wa Kyela. Watoto dodom wanashindia mboga mboga za majani sometimes bila hata kuonja starch. Kama Tanzania ina chakula cha kutosha si iwapelekee huo mchele wa Kyela bure .... kwa mwka mzima.

Anyway, Watu wengi hawajui kuwa huo msaada haukuja kwa bahati mbaya. Actually, huu msaada ni wa tatu .... tayari serkali ilishapokea msaada wa kwanza, watoto wakaupiga, wakapokea wa pili wakapiga .... sasa hii awamu ya tatu tumejua kwa kuwa tu serikali ya USA wametangaza.

Kwangu mimi, Bashe namumuona ni Mnafiki mkubwa. Haiwezekani chakula kiingie nchini hata kama ni cha msaada bila Wizara ya Kilimo kutoa kibali. Pia huo mchele ukiingia lazima upewe msamaha wa kodi .... hivyo Mwigulu naye lazima afahamu. Kwa wao kuanza kupiga danadana na kuwapotosha wananchi ndiyo wameleta taflani isiyokuwa na sababu. Badala ya kuwaeleimisha wananchi wao wanakuja na siasa na propaganda zao. Pathetic...!!

Hata North Korea wenyewe wakizidiwaga huwa wanaupokea mchele wa marekani ..... ndiyo ije hii Tanzania yetu.
 
Sakata la mchele wenye virutubisho kutoka Marekani limeendelea kuchukua sura mpya baada ya waislamu kuukataa bila kumumunya maneno. Wakiongea kupitia redio ya kiislamu ya Imaan FM inayounguruma kutokea mkoa wa Morogoro, wamesema hawautaki mchele huo na wametoa tahadhari kwa mtu yeyote atakayewalisha watoto wao. Wamesema chakula wanacho cha kutosha hapa nchini na kushauri waletewe vitu wasivyokuwa navyo kama vile ndege, magari na ambulance.

Ili kuonyesha kuwa hawatanii katika hili, hata watangazaji waliokuwa wakiendesha kipindi walionekana kushabikia kitendo hicho. Mtu yeyote aliyepiga simu kwenye kipindi akionyesha kwenda kinyume na msimamo wao, walimkatia simu mara moja. Hebu wasikilize wewe mwenyewe kupitia klipu hiyo hapo chini.

MAONI YANGU
Huu mchele sasa naona umeanza kutugawa kiitikadi. Wakristo nao wakitoka hadharani na kuweka msimamo wao, hapatatosha. Ifike mahali ubaguzi wa kijinga kama huu ukemewe kwani unaweza kuligawa taifa na kuhatarisha umoja na mshikamano tulio nao hapa nchini. Tusiruhusu kikundi kidogo cha watu kitugawe kwa sababu yoyote ile.

Nawasilisha.
Nawaunga mkono kwa 100% , virubisho kwenye vyakula ati kupunguza utapia mlo kwa watoto, hivi kwa umri huu tumefika kwa kula vyakula vyenye virutubisho kutoka ulaya?

Wanunue vitabu na kugawa mashuleni, wawekeze katika vyuo vyetu hasa vya kati mfano veta, mambo ya vyakula tz tuna vyakula vya asili ambavyo vimejaa virutubisho kibao , na vimetukuza vizuri tu
 
Back
Top Bottom