Wasifu (CV) ya Dr. John Pombe Magufuli

Wasifu (CV) ya Dr. John Pombe Magufuli

Urais sio sawa na uenyekiti wa Chama!Uzoefu unaotakiwa kuongoza nchi na chama ni vitu viwili tofauti!Magufuli na Lowassa wote wanauzoefu wa kuongoza serikali lakini si chama!

Chama kilimwamini ndo maana kikampa aipeperushe bendera. Mchuano wa kumpata mgombea Uraisi ndani ya CCM ni mrefu sana walijitokeza hao wenye experience ya chama na walimwagwa
 
Huo wasifu unatosha kabisa kumwachia chama na atakisongesha tu bila shida
 
Mkuu, kwani Mzee Mwinyi ni Mtanganyika vile? Tehetehetehetehe

Mwinyi ni Mtanganyika namba wani sio mzanzibari . Kuwa yeye rais kule ni hayo mambo ya ccm kuona wa znz hawawezi kitu...nani asiejua meinyi kazaliwa tandika kakulia tandika na kenda kusoma madrassa znz.
Wale wapemba pale kariakoo ni wapemba tu hawawi watanganyika kwa sababu wanauza nguo.
 
1.Mzee watoto saba sio mchezo...kumbe ni mzima kwenye game.
2.Alihamia Lake baada ya kuchemka Seminary.. na yeye nikilaza pia.
3.Alikwenda kusoma Diploma ya ualimu baada ya kushidwa kupata points za kuingia UDSM au kwenda Makerere hili nalo na yeye ******..
4.Mpaka kesho bado natafuta research papers zake alizokuwa akifanya kwenye Masters au PhD yake sijawahi kupata..
Research papers za Mbowe unazo?
 
Porojo za mtandaoni hazimnyimi magufuli uongozi
 
Sisi matokeo yake yatatusaidia nini? Ili mradi mheshimiwa rais anadeliva kama alivyoahidi haijalishi ana PhD au cheti
 
Unataka matokeo ya Mh Rais ya kazi gani???

unataka kwenda segerea eeeeeeeee

Wewe ni nan ku-judge elimu ya Mh Rais????

Bila shaka kuna kitu unakitafutaaaa
 
acheni kutafuta kiki za kijinga kwa rais we nani katika taifa hill leta matokeo ya baba yako faki kyuu
 
CV YA Dr MAGUFULI
NGULI WA SAYANSI

Dk. John Pombe Joseph Magufuli,
Ana Shahada ya Uzamivu ya Kemia (2006 – 2009) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Uzoefu wa kazi
Mwaka 2008 – 2010: Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Samaki; Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato).

Mwaka 2005 – 2008: Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; na Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato)

Pamoja na kuwa busy na mambo ya kazi za siasa, Uwaziri na Ubunge, Mheshimiwa Magufuli aliweza kusoma na kumaliza PhD yake pale UDSM jambo ambalo ni la kupigiwa mfano tofauti na Mbunge mmoja wa Upinzani aliyeshindwa kumaliza Shahada yake laini (BBA) hapo hapo UDSM miaka nenda rudi.BAADHI YA MACHAPISHO/PUBLICATIONS YA MTEULEMulokozi A. M.; Akwilapo, L.D.: Buchweishaija, J.; Magufuli J. P., and Kyobe, J. Securing the Mechanism of the Decomposition of CaCO3 by the Thermodynamics of the Reaction¿, East and Southern Africa Environmental Chemistry Workshop, pp 71-83, 1st ¿ 5th December 2003, Dar es Salaam 5 Dec 2003
Kiukweli hiki ni kichwa hakuna mfano, yaani kimepiga Ph.D ya Kemia kwa desertation mtindo wa part time!.

Ph.D za UDSM hutolewa kwa aina mbili
1. By Thesis
2.By Desertation.

Ph.D by thesis ndio mtu unaweza kujichimbia popote na kutumia muda wowote kuikamilisha, hii sio full time.

Ph.D by Desertation hii ni full time ukiwekewa supervisor. Kitendo cha Magufuli kufanya Ph.D akiwa kazini tena waziri na Mbunge bila kuchukua study leave na kuimaliza ndani ya miaka 3, ni kupigiwa mfano. Kiukweli huyo Supervisor wake Prof.Buchweishaija anastahili pongezi za dhati.

Ukiangalia trend kama hii huwezi kushangaa mtu akimkingia kifua mmoja wa wateule wake aliyefanya mambos kama hizo, kitu muhimu kabisa ni "The End Justifies The Means".

Hongera sana mwanasayansi wetu kichwa, na Kiukweli ndani ya hiki kichwa hesabu imesimama wima.

Tuzidi kumuombea rais wetu zaidi ya kuwa very intelligent with very high I.Q, tumuombe Mungu amfanye kama Mfalme Sulaiman kwa kumjalia hekima na busara which is the only thing missing!.

Paskali.
 
CV YA Dr MAGUFULI
NGULI WA SAYANSI NA RAIS MTRAJIWA AWAMU YA 5:

Dk. John Pombe Joseph Magufuli, alizaliwa Oktoba 29, 1959 wilayani Chato – wakati huo ikiwa Mkoa wa Kagera (sasa Mkoa wa Geita).
Ana Shahada ya Uzamivu ya Kemia (2006 – 2009) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mwaka 1991 – 1994, alisoma Shahada ya Uzamili (Kemia) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na baadaye Chuo Kikuu cha Salfordnchini Uingereza.

Mwaka 1985 – 1988, alisoma Shahada ya Kwanzaya Elimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akichukua masomo ya Kemia na Hisabati.

Mwaka 1981 – 1982, alisoma diploma katika Chuo cha Mkwawa akichukua masomo ya Kemia na Hisabati.

Mwaka 1979 – 1981, alipata elimu ya juu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Mkwawa, Iringa.

Mwaka 1977 – 1978, alisoma elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Lake, Mwanza.

Mwaka 1975 – 1977, alisoma Shule ya Msingi Katoke, Biharamulo mkoani Kagera.
Mwaka 1967 – 1974, alisoma Shule ya Msingi, Chato.

Mafunzo
Machi 1984 – Juni 1984 alihudhuria mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mpwapwa mkoani Dodoma.

Januari 1984 – Machi 1984 alikuwa JKT Makuyuni, Arusha.
Julai 1983 – Desemba 1983 alikuwa JKT Makutupora, Dodoma.

Uzoefu wa kazi
Mwaka 2010 – hadi sasa: Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Chato.
Mwaka 2008 – 2010: Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Samaki; Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato).

Mwaka 2005 – 2008: Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; na Mbunge wa Biharamulo Mashariki (Chato)

Mwaka 2000 – 2005: Waziri wa Ujenzi, na Mbunge wa Biharamulo Mashariki.
Mwaka 1995 – 2000: Naibu Waziri wa Ujenzi; na Mbunge wa Biharamulo Mashariki.
Mwaka 1989 – 1995: Mkemia Chama cha Ushirika cha Nyanza Cooperative Union (Ltd.), Mwanza.

Mwaka 1982 – 1983: Mwalimu Shule ya Sekondari Sengerema (akifundisha masomo ya Kemia na Hisabati).
Dk. Magufuli amepata tuzo mbalimbali za ndani na nje ya nchi.
Ameshiriki na kuongoza mikutano mingi ya kitaifa na kimataifa.

Ameandika vitabu na majarida mbalimbali. Ameoa na ana watoto kadhaa.
[12:08, 27/08/2015] Ayub Cmn:
Pamoja na kuwa busy na mambo ya kazi za siasa, Uwaziri na Ubunge, Mheshimiwa Magufuli aliweza kusoma na kumaliza PhD yake pale UDSM jambo ambalo ni la kupigiwa mfano tofauti na Mbunge mmoja wa Upinzani aliyeshindwa kumaliza Shahada yake laini (BBA) hapo hapo UDSM miaka nenda rudi.BAADHI YA MACHAPISHO/PUBLICATIONS YA MTEULEMulokozi A. M.; Akwilapo, L.D.: Buchweishaija, J.; Magufuli J. P., and Kyobe, J. ¿Securing the Mechanism of the Decomposition of CaCO3 by the Thermodynamics of the Reaction¿, East and Southern Africa Environmental Chemistry Workshop, pp 71-83, 1st ¿ 5th December 2003, Dar es Salaam 5 Dec 2003
Magufuli, J. P., ¿Funding requirements for the EAC Road network project the East African Community Roads Development partners Consultative meeting 29th ¿ 30th April, 2003 Arusha Tanzania. 30 Apr 2003
Magufuli, J. P., (MP) PIARC First Delegate and Minister for Works of the United Republic of Tanzania.¿ Access to Mobility a basic Social Service, Special Trunk Roads project, Design and Build Tanzania model, XXIInd World Road Congress, 19 ¿ 25 October, 2003 Durban, South Africa. 25 Oct 2003
Mulokozi, A. M., Kyobe, Magufuli, J. P. and R. Whitehead. ¿A New Rate Equation for Solid State Decompositions and its application to the Decomposition of CaCo3. TCS Inaug. Conf. Proc., 11 ¿ 16 July, 1999, p162 ¿ 183. 16 July 1999
Magufuli, J. P., ¿Background of the Mtwara Development Corridor¿ Meeting of the head of States from Malawi, Tanzania, Zambia and Mozambique during the Rounding of the Mtwara Development Corridor, 15 December, 2004, Lilongwe ¿ Malawi.

JPM kachimba ile mbaya!
Nampa hongera.
 
Kiukweli hiki ni kichwa hakuna mfano, yaani kimepiga Ph.D ya Kemia kwa desertation mtindo wa part time!.

Ph.D za UDSM hutolewa kwa aina mbili
1. By Thesis
2.By Desertation.

Ph.D by thesis ndio mtu unaweza kujichimbia popote na kutumia muda wowote kuikamilisha, hii sio full time.

Ph.D by Desertation hii ni full time ukiwekewa supervisor. Kitendo cha Magufuli kufanya Ph.D akiwa kazini tena waziri na Mbunge bila kuchukua study leave na kuimaliza ndani ya miaka 3, ni kupigiwa mfano. Kiukweli huyo Supervisor wake Prof.Buchweishaija anastahili pongezi za dhati.

Ukiangalia trend kama hii huwezi kushangaa mtu akimkingia kifua mmoja wa wateule wake aliyefanya mambos kama hizo, kitu muhimu kabisa ni "The End Justifies The Means".

Hongera sana mwanasayansi wetu kichwa, na Kiukweli ndani ya hiki kichwa hesabu imesimama wima.

Tuzidi kumuombea rais wetu zaidi ya kuwa very intelligent with very high I.Q, tumuombe Mungu amfanye kama Mfalme Sulaiman kwa kumjalia hekima na busara which is the only thing missing!.

Paskali.
Hahahahahaaaaaaa PhD ya Magu, CV haijakamilika hiyo, ina maana hakusoma Bachelor, Advanced level, O-level, Primary, Chekechekea(Vijidudu)??

Naona umerukia kutaja PhD tu.
Weka mambo wazi au hana vyeti kama kipenzi chake Bashite?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom