Wasichokijua wenye akili fupi na za hovyo hovyo juu ya makelele yenye tija ya Tundu Lissu

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,571
108,926
Tokea mchana baada kukamilika kwa mazungumzo na Wazungu wa Madini wa Barrick na kupelekea utiaji saini wa makubaliano mapya ya usimamizi na malipo stahiki nimekuwa nikipitia Social Platforms nyingi ( JF ikiwemo ) na kugundua kwamba Watu wengi wamekuwa wakimshutumu na hadi kumdhihaki Mbunge Mheshimiwa Tundu Lissu kwa kumuambia kwamba ' ameshindwa ' na mambo mengine mengi.

Ama hakika leo ndiyo niweza kujua kwamba kumbe Watanzania wengi uwezo wao wa ' Kufikiri ' ni mdogo sana na kwamba bado tuna safari ndefu mno ya kuweza kukimbizana na wana Jumuia Afrika Mashariki wenzetu hasa Wanyarwanda, Wakenya na Waganda ambao kiukweli IQ zao zipo juu mno na pengine ndiyo maana wametuacha Kimaendeleo.

Yaani Watanzania badala ya kuchambua hili jambo vizuri tena Kisomi kabisa ili kuonyesha kwamba huko Vyuo Vikuu hatukuenda kupoteza muda au kukua tu wengi wetu tumeacha kujikita katika ' Hoja ' Kuu na ya Msingi na badala yake tumetanguliza mbele itikadi zetu za Kisiasa ( hapa namaanisha UCCM na UCHADEMA ) katika jambo ambalo pengine halihitaji zaidi Siasa ila linahitaji zaidi mjadala mpana.

Kwa wale ' Critics ' wote wa Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu labda niwaambieni tu kwamba mnaweza leo mkamcheka na kumdhihaki Lissu kwa kila aina ya maneno na kashfa ila tambueni kwamba yale ' makelele ' yake au ule ' uropokaji ' wake ambao Mimi nimeubatiza rasmi kwa majina ya ' makelele tija ' au ' uropokaji tija ' ndiyo umepelekea leo hii tumekuwa na haya matokeo ' chanya ' ya mazungumzo marefu na Watu wa Barrick na nadhani Watanzania tulipashwa ' Kumpongeza ' Lissu badala ya kumdhaki hivi.

Hivi mnadhani bila makelele yale / uropokaji ule wa Tundu Lissu Serikali yetu ingejipanga vyema kuandaa Timu yake iliyokuwa chini ya Waziri Profesa Kabudi ili waweze kufanya mazungumzo makini ambaye yangeinufaisha leo hii nchi yetu Kimapato kama hivi ilivyotokea? Siyo kila Mtu anayekupinga au kukusema vibaya ' anakuchukia ' tena kwa Mimi ninavyojua ni kwamba yule Mtu anayekusema au kukukosoa ndiyo mwenye ' mapenzi ' mema na ya kweli nawe kuliko yule ambaye kila mara anakuchekea na kukusifu halafu siku ukija ' kuharibikiwa ' ndiyo anakudharau zaidi.

Ingekuwa ni nchi zingine ambazo zina Watu wenye IQ za kweli na ambazo zinawatosha sawasawa nadhani baada ya haya mazungumzo yaliyozaa ' tija ' na Barrick leo basi tungempongeza na hata kumpa ' Tuzo ' Mheshimiwa Tundu Lissu kwani yale ' makelele tija ' yake ' uropokaji tija ' wake ndiyo umesaidia ' kuchochea ' kuwepo kwa umakini wa mazungumzo na hawa Wazungu wa Barrick lakini bahati mbaya mno Watanzania wengi wenye akili fupi na za hovyo hovyo leo kutwa nzima wanachokifanya ni kumsema vibaya Tundu Lissu na kumdhihaki.

Nikiwa kama Mtanzania ( GENTAMYCINE ) niseme tu kwamba nimefurahi sana kuona kwamba leo kumekuwa na mafanikio ya Tume iliyoundwa na Mheshimiwa Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli ambayo pia imeleta mafanikio makubwa hivyo angalau sasa Tanzania itakuwa inapata kile inachostahili kutoka katika Rasilimali zake za madini ila nadhani pia hata Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu nae anahitaji kupongezwa kwani sidhani kama bila ' makelele tija ' yake / ' uropokaji tija ' wake leo Tanzania ingefikia hapa ilipofika.

Namuunga sana mkono Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli katika harakati zake za kuiletea Maendeleo Tanzania lakini pia namuunga mno Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu katika harakati zake za kuishtua na kuiamsha Serikali juu ya mambo ambayo ama hawayajui au wanayajua lakini wanataka kuyapeleka ndivyo sivyo. Nilidhani leo kutakuwa na ' mijadala ' yenye ' tija ' badala yake kila nikipita mitaani ' Vijiweni ' na nikitembelea mitandao yetu hii nashuhudia tu akili zile zile ' fupi ' na za ' hovyo hovyo ' kutoka kwa Watanzania ambao bahati nzuri kutwa wanajiita ' Wasomi ' au ' Great Thinkers '.

Watanzania tubadilike Kifikra na Kimtizamo kama kweli tunataka kukimbia Kimaendeleo na Kidemokrasia.

Nawasilisha.
 
SIkupenda watu wamwingize Lissu hapa. Pia sikupenda watu wafanye ulinganishi kati ya juhudi za JPM na kilichoitwa "kelele" za Lissu. Matokeo yameonekana na sote tunajua aliyetusaidia kufika hapa ni nani. Ulimwengu unajua hilo pia. Tena imebainika ya kwamba kilichotokea ni mwanzo tu wa Tanzania mpya na uzatiti wa raslimali zake. Kazi ya Waziri wa Sheria imeonekana, kazi ya Kamati ya Majadiliano imeonekana. Dira ya mkuu wa nchi kuhusu rasilimali za nchi hii imedhihirika. Hatulinganishi, tunaendelea mbele.
 
SIkupenda watu wamwingize Lissu hapa. Pia sikupenda watu wafanye ulinganishi kati ya juhudi za JPM na kilichoitwa "kelele" za Lissu. Matokeo yameonekana na sote tunajua aliyetusaidia kufika hapa ni nani. Ulimwengu unajua hilo pia. Tena imebainika ya kwamba kilichotokea ni mwanzo tu wa Tanzania mpya na uzatiti wa raslimali zake. Kazi ya Waziri wa Sheria imeonekana, kazi ya Kamati ya Majadiliano imeonekana. Dira ya mkuu wa nchi kuhusu rasilimali za nchi hii imedhihirika. Hatulinganishi, tunaendelea mbele.

Kwahiyo Mkuu baada ya huu ufafanuzi wake mzuri kabisa, je una maoni gani juu ya Watanzania wenzetu wenye akili ' fupi ' na za ' hovyo hovyo? ' ambao wanamuona Tundu Lissu hana maana au hakuwa na maana au alikuwa na nia ' ovu ' na Tanzania wakati ukweli ni kwamba ' makelele tija ' yake / ' uropokaji tija ' wake ndiyo umesaidia kuwepo na mafanikio ya Kiumakini katika mazungumzo haya na Watu wa Barrick?
 
Ndugu yangu GENTAMYCINE kazi ya upinzani ni kukosoa,kukosoa na kukosoa kadri iwezavyo ilimradi haivunji sheria za nchi,haisababishi uvunjifu wa amani na wanachokikosoa ni cha msingi kwa ustawi wa taifa letu.

Upinzani kazi yake ni kuja na mawazo mbadala tofauti na mawazo yale ya serikali husika,na ndomana wanaitwa/tunawaita serikali mbadala. Tunahitaji upinzani ulio imara wenye hoja zilizopangika na kueleweka,sio kudandia dandia vijimambo visivyo na mbele wala nyuma.

Timu ya Lissu,Zitto na Dr.Slaa ilikua timu bora zaidi katika kujenga hoja za msingi na za kufikirisha,hivi sasa upande wa upinzani esp CHADEMA amebaki mtoa mada mmoja tuu Lissu wengine wote hamna kitu.
 
Tokea mchana baada kukamilika kwa mazungumzo na Wazungu wa Madini wa Barrick na kupelekea utiaji saini wa makubaliano mapya ya usimamizi na malipo stahiki nimekuwa nikipitia Social Platforms nyingi ( JF ikiwemo ) na kugundua kwamba Watu wengi wamekuwa wakimshutumu na hadi kumdhihaki Mbunge Mheshimiwa Tundu Lissu kwa kumuambia kwamba ' ameshindwa ' na mambo mengine mengi.

Ama hakika leo ndiyo niweza kujua kwamba kumbe Watanzania wengi uwezo wao wa ' Kufikiri ' ni mdogo sana na kwamba bado tuna safari ndefu mno ya kuweza kukimbizana na wana Jumuia Afrika Mashariki wenzetu hasa Wanyarwanda, Wakenya na Waganda ambao kiukweli IQ zao zipo juu mno na pengine ndiyo maana wametuacha Kimaendeleo.

Yaani Watanzania badala ya kuchambua hili jambo vizuri tena Kisomi kabisa ili kuonyesha kwamba huko Vyuo Vikuu hatukuenda kupoteza muda au kukua tu wengi wetu tumeacha kujikita katika ' Hoja ' Kuu na ya Msingi na badala yake tumetanguliza mbele itikadi zetu za Kisiasa ( hapa namaanisha UCCM na UCHADEMA ) katika jambo ambalo pengine halihitaji zaidi Siasa ila linahitaji zaidi mjadala mpana.

Kwa wale ' Critics ' wote wa Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu labda niwaambieni tu kwamba mnaweza leo mkamcheka na kumdhihaki Lissu kwa kila aina ya maneno na kashfa ila tambueni kwamba yale ' makelele ' yake au ule ' uropokaji ' wake ambao Mimi nimeubatiza rasmi kwa majina ya ' makelele tija ' au ' uropokaji tija ' ndiyo umepelekea leo hii tumekuwa na haya matokeo ' chanya ' ya mazungumzo marefu na Watu wa Barrick na nadhani Watanzania tulipashwa ' Kumpongeza ' Lissu badala ya kumdhaki hivi.

Hivi mnadhani bila makelele yale / uropokaji ule wa Tundu Lissu Serikali yetu ingejipanga vyema kuandaa Timu yake iliyokuwa chini ya Waziri Profesa Kabudi ili waweze kufanya mazungumzo makini ambaye yangeinufaisha leo hii nchi yetu Kimapato kama hivi ilivyotokea? Siyo kila Mtu anayekupinga au kukusema vibaya ' anakuchukia ' tena kwa Mimi ninavyojua ni kwamba yule Mtu anayekusema au kukukosoa ndiyo mwenye ' mapenzi ' mema na ya kweli nawe kuliko yule ambaye kila mara anakuchekea na kukusifu halafu siku ukija ' kuharibikiwa ' ndiyo anakudharau zaidi.

Ingekuwa ni nchi zingine ambazo zina Watu wenye IQ za kweli na ambazo zinawatosha sawasawa nadhani baada ya haya mazungumzo yaliyozaa ' tija ' na Barrick leo basi tungempongeza na hata kumpa ' Tuzo ' Mheshimiwa Tundu Lissu kwani yale ' makelele tija ' yake ' uropokaji tija ' wake ndiyo umesaidia ' kuchochea ' kuwepo kwa umakini wa mazungumzo na hawa Wazungu wa Barrick lakini bahati mbaya mno Watanzania wengi wenye akili fupi na za hovyo hovyo leo kutwa nzima wanachokifanya ni kumsema vibaya Tundu Lissu na kumdhihaki.

Nikiwa kama Mtanzania ( GENTAMYCINE ) niseme tu kwamba nimefurahi sana kuona kwamba leo kumekuwa na mafanikio ya Tume iliyoundwa na Mheshimiwa Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli ambayo pia imeleta mafanikio makubwa hivyo angalau sasa Tanzania itakuwa inapata kile inachostahili kutoka katika Rasilimali zake za madini ila nadhani pia hata Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu nae anahitaji kupongezwa kwani sidhani kama bila ' makelele tija ' yake / ' uropokaji tija ' wake leo Tanzania ingefikia hapa ilipofika.

Namuunga sana mkono Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli katika harakati zake za kuiletea Maendeleo Tanzania lakini pia namuunga mno Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu katika harakati zake za kuishtua na kuiamsha Serikali juu ya mambo ambayo ama hawayajui au wanayajua lakini wanataka kuyapeleka ndivyo sivyo. Nilidhani leo kutakuwa na ' mijadala ' yenye ' tija ' badala yake kila nikipita mitaani ' Vijiweni ' na nikitembelea mitandao yetu hii nashuhudia tu akili zile zile ' fupi ' na za ' hovyo hovyo ' kutoka kwa Watanzania ambao bahati nzuri kutwa wanajiita ' Wasomi ' au ' Great Thinkers '.

Watanzania tubadilike Kifikra na Kimtizamo kama kweli tunataka kukimbia Kimaendeleo na Kidemokrasia.

Nawasilisha.
Mi sidhani kama upo sahihi unaposema "makelele yake ndo yamepelekea haya yaliyo tokea leo " kama nakumbu kumbu nzuri, nakumbuka alishawahi kusema kama siyo yeye basi itakua viongozi wenza wa cdm, kwamba katika hili tutashindwa vibaya mno,, 'au hawakutamka/kutamka hivo?


Basi kama walitamka/alitamka hivo, 'hayo maneno ndo yanafanya ashambuliwe mtandaoni.
 
Ndugu yangu GENTAMYCINE kazi ya upinzani ni kukosoa,kukosoa na kukosoa kadri iwezavyo ilimradi haivunji sheria za nchi,haisababishi uvunjifu wa amani na wanachokikosoa ni cha msingi kwa ustawi wa taifa letu.

Upinzani kazi yake ni kuja na mawazo mbadala tofauti na mawazo yale ya serikali husika,na ndomana wanaitwa/tunawaita serikali mbadala. Tunahitaji upinzani ulio imara wenye hoja zilizopangika na kueleweka,sio kudandia dandia vijimambo visivyo na mbele wala nyuma.

Timu ya Lissu,Zitto na Dr.Slaa ilikua timu bora zaidi katika kujenga hoja za msingi na za kufikirisha,hivi sasa upande wa upinzani esp CHADEMA amebaki mtoa mada mmoja tuu Lissu wengine wote hamna kitu.

Kwahiyo na Wewe una maoni gani hasa juu ya ' makelele tija ' / ' uropokaji tija ' wa Mheshimiwa Tundu Lissu na je ni sahihi kwa Watanzania wenye akili ' fupi ' na za ' hovyo hovyo ' kumdhihaki hadi kumtukana juu ya yale aliyokuwa akiyashikilia bango na yaliyokuwa na manufaa kwa Tanzania?

Nitashukuru ukinijibu Mkuu.
 
Mi sidhani kama upo sahihi unaposema "makelele yake ndo yamepelekea haya yaliyo tokea leo " kama nakumbu kumbu nzuri, nakumbuka alishawahi kusema kama siyo yeye basi itakua viongozi wenza wa cdm, kwamba katika hili tutashindwa vibaya mno,, 'au hawakutamka/kutamka hivo?


Basi kama walitamka/alitamka hivo, 'hayo maneno ndo yanafanya ashambuliwe mtandaoni.

Jifunze ' Kufikiri ' tafadhali. Hivi kwa mfano umeshawahi kujiuliza ni kwanini Kocha wa mpira wa Man United ' mropokaji ' Mourinho huwa anatabia ya ' kuwaponda ' Wachezaji fulani ambao Sisi wapenzi wa mpira huwa tunawaona ni wazuri? Kwa taarifa yako tu ni kwamba Kocha Mourinho huwa anafanya vile ' makusudi ' ili kumtia ' ndimu / hasira ' yule Mchezaji kusudi azidi kufanya juhudi na aweze kuleta mafanikio makubwa Kikosini Kwake hatimaye kuisaidia Timu. Hivyo hivyo kwa Tundu Lissu siyo kwamba alivyokuwa ' anaponda ' vile labda alikuwa anafurahia au anafanya kusudi bali lengo lake kubwa lilikuwa ni ' Kuwaamsha ' waliolala wakati Tanzania bado ilikuwa inaendelea kufanywa Shamba la Bibi na hawa Wazungu hasa katika madini yetu. Ukiwa na akili ' fupi ' na za ' hovyo hovyo ' unaweza ukamwona / ukadhania Lissu alikuwa na lengo baya ila kwa hiki kilichofikiwa hata Yeye ana mchango wake mkubwa tena sana tu japo wengi tutamdhihaki, kumcheka na kumsema vibaya.
 
Tokea mchana baada kukamilika kwa mazungumzo na Wazungu wa Madini wa Barrick na kupelekea utiaji saini wa makubaliano mapya ya usimamizi na malipo stahiki nimekuwa nikipitia Social Platforms nyingi ( JF ikiwemo ) na kugundua kwamba Watu wengi wamekuwa wakimshutumu na hadi kumdhihaki Mbunge Mheshimiwa Tundu Lissu kwa kumuambia kwamba ' ameshindwa ' na mambo mengine mengi.

Ama hakika leo ndiyo niweza kujua kwamba kumbe Watanzania wengi uwezo wao wa ' Kufikiri ' ni mdogo sana na kwamba bado tuna safari ndefu mno ya kuweza kukimbizana na wana Jumuia Afrika Mashariki wenzetu hasa Wanyarwanda, Wakenya na Waganda ambao kiukweli IQ zao zipo juu mno na pengine ndiyo maana wametuacha Kimaendeleo.

Yaani Watanzania badala ya kuchambua hili jambo vizuri tena Kisomi kabisa ili kuonyesha kwamba huko Vyuo Vikuu hatukuenda kupoteza muda au kukua tu wengi wetu tumeacha kujikita katika ' Hoja ' Kuu na ya Msingi na badala yake tumetanguliza mbele itikadi zetu za Kisiasa ( hapa namaanisha UCCM na UCHADEMA ) katika jambo ambalo pengine halihitaji zaidi Siasa ila linahitaji zaidi mjadala mpana.

Kwa wale ' Critics ' wote wa Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu labda niwaambieni tu kwamba mnaweza leo mkamcheka na kumdhihaki Lissu kwa kila aina ya maneno na kashfa ila tambueni kwamba yale ' makelele ' yake au ule ' uropokaji ' wake ambao Mimi nimeubatiza rasmi kwa majina ya ' makelele tija ' au ' uropokaji tija ' ndiyo umepelekea leo hii tumekuwa na haya matokeo ' chanya ' ya mazungumzo marefu na Watu wa Barrick na nadhani Watanzania tulipashwa ' Kumpongeza ' Lissu badala ya kumdhaki hivi.

Hivi mnadhani bila makelele yale / uropokaji ule wa Tundu Lissu Serikali yetu ingejipanga vyema kuandaa Timu yake iliyokuwa chini ya Waziri Profesa Kabudi ili waweze kufanya mazungumzo makini ambaye yangeinufaisha leo hii nchi yetu Kimapato kama hivi ilivyotokea? Siyo kila Mtu anayekupinga au kukusema vibaya ' anakuchukia ' tena kwa Mimi ninavyojua ni kwamba yule Mtu anayekusema au kukukosoa ndiyo mwenye ' mapenzi ' mema na ya kweli nawe kuliko yule ambaye kila mara anakuchekea na kukusifu halafu siku ukija ' kuharibikiwa ' ndiyo anakudharau zaidi.

Ingekuwa ni nchi zingine ambazo zina Watu wenye IQ za kweli na ambazo zinawatosha sawasawa nadhani baada ya haya mazungumzo yaliyozaa ' tija ' na Barrick leo basi tungempongeza na hata kumpa ' Tuzo ' Mheshimiwa Tundu Lissu kwani yale ' makelele tija ' yake ' uropokaji tija ' wake ndiyo umesaidia ' kuchochea ' kuwepo kwa umakini wa mazungumzo na hawa Wazungu wa Barrick lakini bahati mbaya mno Watanzania wengi wenye akili fupi na za hovyo hovyo leo kutwa nzima wanachokifanya ni kumsema vibaya Tundu Lissu na kumdhihaki.

Nikiwa kama Mtanzania ( GENTAMYCINE ) niseme tu kwamba nimefurahi sana kuona kwamba leo kumekuwa na mafanikio ya Tume iliyoundwa na Mheshimiwa Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli ambayo pia imeleta mafanikio makubwa hivyo angalau sasa Tanzania itakuwa inapata kile inachostahili kutoka katika Rasilimali zake za madini ila nadhani pia hata Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu nae anahitaji kupongezwa kwani sidhani kama bila ' makelele tija ' yake / ' uropokaji tija ' wake leo Tanzania ingefikia hapa ilipofika.

Namuunga sana mkono Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli katika harakati zake za kuiletea Maendeleo Tanzania lakini pia namuunga mno Mheshimiwa Mbunge Tundu Lissu katika harakati zake za kuishtua na kuiamsha Serikali juu ya mambo ambayo ama hawayajui au wanayajua lakini wanataka kuyapeleka ndivyo sivyo. Nilidhani leo kutakuwa na ' mijadala ' yenye ' tija ' badala yake kila nikipita mitaani ' Vijiweni ' na nikitembelea mitandao yetu hii nashuhudia tu akili zile zile ' fupi ' na za ' hovyo hovyo ' kutoka kwa Watanzania ambao bahati nzuri kutwa wanajiita ' Wasomi ' au ' Great Thinkers '.

Watanzania tubadilike Kifikra na Kimtizamo kama kweli tunataka kukimbia Kimaendeleo na Kidemokrasia.

Nawasilisha.
Sisi wanabavicha na makamanda wengine tunaunga mkono uchambuzi wako murua. Ubarikiwe.
 
Jifunze ' Kufikiri ' tafadhali. Hivi kwa mfano umeshawahi kujiuliza ni kwanini Kocha wa mpira wa Man United ' mropokaji ' Mourinho huwa anatabia ya ' kuwaponda ' Wachezaji fulani ambao Sisi wapenzi wa mpira huwa tunawaona ni wazuri? Kwa taarifa yako tu ni kwamba Kocha Mourinho huwa anafanya vile ' makusudi ' ili kumtia ' ndimu / hasira ' yule Mchezaji kusudi azidi kufanya juhudi na aweze kuleta mafanikio makubwa Kikosini Kwake hatimaye kuisaidia Timu. Hivyo hivyo kwa Tundu Lissu siyo kwamba alivyokuwa ' anaponda ' vile labda alikuwa anafurahia au anafanya kusudi bali lengo lake kubwa lilikuwa ni ' Kuwaamsha ' waliolala wakati Tanzania bado ilikuwa inaendelea kufanywa Shamba la Bibi na hawa Wazungu hasa katika madini yetu. Ukiwa na akili ' fupi ' na za ' hovyo hovyo ' unaweza ukamwona / ukadhania Lissu alikuwa na lengo baya ila kwa hiki kilichofikiwa hata Yeye ana mchango wake mkubwa tena sana tu japo wengi tutamdhihaki, kumcheka na kumsema vibaya.
Ndugu, kwani lisu siasa kaanza jana? mbona kitambo tu, kwanini asinge fanya haya nyuma kabla ya awamu hii ya tano!? tokea mwaka 70, sijui kama sikosei jamaa wamekua wakutunyonya lisu hukuyaona haya kabla?.
 
Sisi wanabavicha na makamanda wengine tunaunga mkono uchambuzi wako murua. Ubarikiwe.

Akhsante sana Mkuu na ni jambo la kheri pia kujua kwamba Mimi mwana CCM tena nisiyejificha kabisa humu JamiiForums GENTAMYCINE leo hii nakubalika tu kwa ' Hoja ' zangu na ' Wapinzani ' wetu wakubwa BAVICHA na CHADEMA yao. Nadhani Siasa za aina hii ndizo tunatakiwa tuzidumishe Tanzania na siyo zile za ' chuki ' na ' majitaka ' Taifa Kwanza Siasa baadae.
 
Ndugu, kwani lisu siasa kaanza jana? mbona kitambo tu, kwanini asinge fanya haya nyuma kabla ya awamu hii ya tano!? tokea mwaka 70, sijui kama sikosei jamaa wamekua wakutunyonya lisu hukuyaona haya kabla?.

Mbona hushangai kuna Wanaume ambao wanajua kabisa kwamba Wake zao wamekuwa ' wakiwasaliti ' miaka hata 20 iliyopita lakini wanaamua ' Kutalikiana ' nao leo / mwaka huu? Hapa nataka kumaanisha nini yawezekana labda hata huko nyuma kiwango cha ' Kunyonywa ' kwa Rasilimali zetu hakikuwa kama hiki cha sasa lakini pia Mimi na Wewe hatujui kwani yawezekana huyu huyu Tundu Lissu labda amekuwa akishauri katika Taasisi muhimu na nyeti za Serikali hasa za awamu zilizopita lakini akapuuzwa hivyo kwa kuwa na ' uchungu ' zaidi kama Mtanzania basi akaona kwamba kwa awamu hii ngoja tu ajitoe ' mhanga ' kupigania ' Rasilimali ' zetu na ndicho amekuwa akikifanya hadi ' matatizo ' haya yalipomkuta.
 
Back
Top Bottom