Wasanii 13 wa taarab wafa ajalini

IMG_6618.JPG


Inasikitisha kwa kweli
 
Wakati tumejaza mizoga serikalini Watanzania wataendelea kufa hadi pale watakapobaini kwamba kuwaendekeza mafisadi ni usaliti wa hali ya juu.

Si mizoga tu bali misukule pia. Kumbuka wanaume (kina Temba, Chenge, Malow, nk) wameonesha kuwa wasanii wa Tanzania ni zaidi ya mizoga.

Ndo hao hao wanaokuwa mstari wa mbele kutunga nyimbo za kusifia mafisadi ili warudi madarakani au waonekane wanakubalika. Mungu mkubwa, hutoa na utwaa. Jina lake liimidiwe sana.
 
Jana tarehe 21/03/2011 taifa lilipoteza wasanii zaidi ya 10 wa kikundi kimoja cha taarab baada ya kupoteza maisha kufuatia basi waliokuwa wakisafiria kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini kugonga nyuma ya lori ambalo linadaiwa kuharibika na kisha kutelekezwa barabarani.

Vifo hivi vimetokea katika siku ambayo Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Kikwete amemwamuru Waziri wa Ujenzi Mhe John Magufuli kuacha kutumia ubabe katika kubomoa nyumba za wananchi anazodai ziko katika hifadhi ya barabara kwa madai ya kutekeleza sheria za usimamizi wa barabara hapa nchini.

Awali kabla ya kutangaza bomoa bomoa holela hiyo, Mhe John Magufuli aliushangaza umma wa watanzania pale alipoagiza kuondolewa kwa mabango ya matangazo ya biashara kwa madai kuwa yanasababisha ajali kwa kuzuia madereva kuona vizuri. Mhe John Magufuli alidai kuwa anatekeleza sheria za barabara.

Ibara ya 9 (1-10) za Kanuni za Sheria ya barabara namba 13 ya 2007 zilizopitishwa kwa Tangazo la Serikali Namba 21 la Tar 23 Januari 2009 zinaipa TANROAD mamlaka ya kuondoa magari yoyote yaliyoharibika na kukaa barabarani kwa zaidi ya masaa 6 mijini na masaa 24 vijijini. Lakini kwa kuwa kuwasimamia TANROAD kutekelza wajibu huu hakutoi mwanya wa kuwepo waanddishi wa habari na wananchi kujua leo Magufuli kafanya nini, waziri huyu hana habari na sheria hii ambayo laiti kama inetekelezwa ingepungua idadi ya ajali mabya za barabarani, vifo, majeruhi na mayatima,

Wakati taifa likiendelea kuomboleza vifo hivi ambavyo vingeweza kuepukwa endapo waziri Magufuli badala ya kukimbilia kujitafutia sifa binafsi kwa kuwabomolea wananchi nyumba zao na mabango ya bishara angekaa chini na wataalamu wa wizara yake na kufanya uchambuzi wa kina kuhusu vyanzo vya ajali za barabarani na namna sheria zilizopo za barabara zinavyoweza kutumika kupunguza ajali hizo. Kwa kufanya hivyo vyanzo vya jali kama magari yanaytolekezwa barabarani vingeweza kushughulikiwa haraka na kwa uzito wake.

Ni dhahiri kuwa kama uchambuzi huo ungefanyika magari yanayotelekezwa barabarani yangeonekana kuhitaji mwarobaini kabla ya mabango ya biashara au bomoa bomoa katika hifadhi za barabara kwa kuwa vyote vimo katika sheria Magufuli anazodai kuzitekeleza. Iweje atekelze sheria kwa kuchagua zile tu zinzoweza kumpatia sifa kutoka kwa wananchi wasioona mbali (Cheap Popularity)

Lakini kutokana na kujitafutia sifa binafsi, tokea achaguliwe mwaka jana waziri Magufuli amekuwa akihangaika na mambo yanayoweza kumpatia sifa binafsi kama vile kuagiza bomoa bomoa holela kwa madai ya kutekeleza sheria ilihali akiacha wananchi wakiendelea kupoteza maisha, kuwa vilema, mayatima kuongezeka kutokana na sababu ambazo kama sheria za barabara zingekuwa zinatekelezwa kama amabvyo Mhe Magufuli anadai kuzitekeleza vifo hivyo vingeweza kuepukwa.
 
poleni hasa jamaa wa karibu na marehemu
Mungu ametoa,mungu ametwaa
awapumzishe kwa amani
 
Jana tarehe 21/03/2011 taifa lilipoteza wasanii zaidi ya 10 wa kikundi kimoja cha taarab baada ya kupoteza maisha kufuatia basi waliokuwa wakisafiria kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini kugonga nyuma ya lori ambalo linadaiwa kuharibika na kisha kutelekezwa barabarani.

................

Lakini kutokana na kujitafutia sifa binafsi, tokea achaguliwe mwaka jana waziri Magufuli amekuwa akihangaika na mambo yanayoweza kumpatia sifa binafsi kama vile kuagiza bomoa bomoa holela kwa madai ya kutekeleza sheria ilihali akiacha wananchi wakiendelea kupoteza maisha, kuwa vilema, mayatima kuongezeka kutokana na sababu ambazo kama sheria za barabara zingekuwa zinatekelezwa kama amabvyo Mhe Magufuli anadai kuzitekeleza vifo hivyo vingeweza kuepukwa.

Tumia akili zako na za kuambiwa! Toka lini mtu akapata popularity kwa kubomoa nyumba? Equally mabango na magari yanaweza kusababisha ajali kwa hiyo huna point ya maana zaidi ya chuki binafsi. So what were you trying to say if I may ask? Kwa sababu ya ushabiki (au sijui niseme uwezo wako ulipofikia wa kuchambua mambo) umeshindwa kujua anayofanya Magufuli ni kwa mujibu wa sheria vile vile. Pole sana sidhani kama criticism zako ni constructive!
 
...hush..hush, now Maria. It is just Satan's work. (Nakwazika mno watu wanaposema ni KAZI YA MUNGU! really? Mungu huyu huyu tunayemjua mwenye wingi wa rehema????)

kweli Baba Desi, sio kila kitu ni MUNGU kuna some 'satanic work'
 
Sad to see somebody so biased against a person who has shown the willingness to work for the good of Tanzania. Parked lorries, yes they are a problem equally problematic are structures built in areas that are suppoed to be road reserves! Even the decision to stop the demolitions is by and large politically motivated. In all honest stopping demolitions is actually seeking cheaping popularity!
 
rip marehemu wote

hapo hakuna siasa ila ukweli ni kuwa serikali inayo simamia miundo mbinu ndiyo inapaswa kubeba lawama zote kwani ajali tz ni nyingi sana na zinasababishwa na miundombinu mibaya
barabara hata kama zikiwa kama ulaya bado madereva esp wafuasi wa chadema sio watumiaji wazuri wa barabara,na huwa wanaendesha hovyo sana bila kufuata sheria,mfano kwa macho yangu siku slaa alipokuja kutafuta udhamini pale mjini moshi wafuasi wengi wa chadema wakiwa na pikikipi na magari walikuwa wakikimbiza vyombo vyao na kuendesha kwa mbwembwe nyingi sana kiasi cha kusababisha ajari!
 
Maskini itakuwa ndo hao 5 star,mimi kama mimi walinipita nikiwa kazini(iringa~mafinga road) pale kilimani palipokuwa na makaburi yenye utata ya kiyeuyeu iringa.Ilikuwa ROSA moja yenye rangi intermediate ya nyeupe na kijivu.BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA,JINA LA BWANA LIBARIKIWE.

Nimeona picha za ajali Gari ilikuwa na alama ya Toyota. Kwa hiyo ni Coaster maana Rosa ni Mitsubishi/Fuso. R.I.P. waliotutangulia.
 
Back
Top Bottom