Hawa clouds, yaan badala ya kuweka habari za msingi kuhusu huo msiba, wao wanaleta malumbano ya kimapenzi kati ya diamondi ,diva na wema sepetu, Usupa star kazi kwelikweli,,,
Je? Ajali hii ni sababu ya miundombinu mibovu au ni uzembe wa dereva.... Swali kwako mleta mada,una taarifa gani mpaka sasa? kuhusu hii ajaliRIP Marehemu wote
Hapo hakuna siasa ila ukweli ni kuwa serikali inayo simamia miundo mbinu ndiyo inapaswa kubeba lawama zote kwani ajali Tz ni nyingi sana na zinasababishwa na miundombinu mibaya
Hivi kundi hili lina include wanamuziki gani? wengine siyo wapenzi sana wa muziki wa mwambao,Mungu awalaze mahali pema peponi
Maskini itakuwa ndo hao 5 star,mimi kama mimi walinipita nikiwa kazini(iringa~mafinga road) pale kilimani palipokuwa na makaburi yenye utata ya kiyeuyeu iringa.Ilikuwa ROSA moja yenye rangi intermediate ya nyeupe na kijivu.BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA,JINA LA BWANA LIBARIKIWE.