Wasanii 13 wa taarab wafa ajalini

Wasanii 13 wa taarab wafa ajalini

Hizi threads za hii ajali zingeunganishwa!!
 
Wengine mnasema pwani-chalinze na wengine morogoro-mikumi!!! mmmh kikubwa ni ajali, poleni
 
Kwa mujibu wa taarifa za TBC leo asubuhi, muimbaji mkongwe Mwanahawa Alli aliyeimba 'Kinyago cha Mpapure' ni mmoja wa majeruhi watano. Alikuwa kwenye safari hiyo kama muimbaji mualikwa. Wakati anahojiwa na muandishi wa TBC anaonyesha kabisa kuwa bado ana mawenge ya ajali na haamini kilichotokea. RIP Five Stars waliotutoka, wanaume saba na wanawake watatu. kwa ataarifa za mwanzo za Clouds Fm zikimnukuu RPC wa mkoa wa Morogoro, Dereva wa Coaster iliyowabeba wasanii hao na kupata ajali, ni mmoja wa walionusurika na ajali hiyo.
 
Ajali imetokea DOMA karibu na Mikumi baada ya Coaster ya Fivestar kujaribu kulipita lorry la mbao na bahati mbaya mbele kukawa kunakuja lorry lingine, hivyo dereva wa coaster kupunguza mwendo na kuliingilia lorry kwa nyuma, wamekufa 12 baada ya kutobolewa na mbao zilizokua kwenye lorry hilo ambalo lilikua limesimama! majeruhi ni saba na maiti hazitazamiki!! imetokea saa mbili usiku! Source: WAPO RADIO
 
Ameshakufa majeruhi mwingine!! na majeruhi ni tisa! ngoja kupambazuke watupe majina
 
Habari Mbaya sana kuanzia siku mungu aziweke roho za marehemu pema peponi na majeruhi awape kupona haraka
Faraja iwe na family zote zilizopoteza wapendwa wao na Taifa kwa ujumla
 
Idadi ya marehemu 13 majeruhi 9 majina bado, ZENA MOHAMED ALLY JUMA RAJABU KOMBO MWANAHAWA NA SHABANI HAMIS ndio miongoni mwao, weka mkato kila baada ya majina mawili na walitokea Kyela, maiti zimeharibika sana maana walichanwa na mbao baada ya coaster hii kuigonga lorry hilo kwa nyuma, sehemu ni DOMA-.MIKUMI: Source: WAPO RADIO na imethibitishwa na kamanda wa usalama barabarani morogoro
 
Idadi ya marehemu 13 majeruhi 9 majina bado, ZENA MOHAMED ALLY JUMA RAJABU KOMBO MWANAHAWA NA SHABANI HAMIS ndio miongoni mwa MAJERUHI
 
Kundi la five stars modern taarab wamepata ajali mbaya usiku wa kuamkia leo wakitokea mkoani Mbeya kuwarusha roho mashabiki wake. Ajali imetokea wkt dereva wa Five stars akijaribu kulipita lori lililo kuwa limeegeshwa maeneo ya Doma ukisha maliza mbuga ya Mikumi wkt analipita mbele yake kulikuwa na lori jingine likitokea Moro kwenda Iringa dereva akaamua kurudisha tena Coaster upande wa kushoto ndipo alipo livaa lori la mbao. Wanamziki 12 wamefariki pale pale na mmoja kafia hospitali ya Moro idadi ya walio fariki mpaka sasa ni 13. Na majeruhi 9.
Poleni wafiwa poleni wapenzi wa Taarab.
Tupo pamoja nanyi katika kipindi hiki kigumu.
Ni pigo kwa mziki wa taraab ikumbukwe kundi hili liliundwa mwaka 2008.
 
Sheba Juma nae aktutoka jamani,Issa Kijoti ajali hizi zinafupisha maisha ya vijana wadogo kabisa ambao ndo kwaaaaaaanza wanaannza.
Dah!! Inasikitisha kwa kweli kupoteza hawa vijana.......!!
 
Chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa dereva wa coaster na kuto kuwa makini wakati analipita lori lililo simama. Hivyo basi dereva wa coaster ni mzembe kasababisha vifo vya wanamziki wasio kuwa na hatia.
 
This is very sad
MUNGU azilaze roho za marehemu mahali pema peponi Amina.
 
So Sad ........Mungu uwarehemu na uwaponye majeruhi wote. Wape faraja wafiwa
 
May Lord R.I.P. roho za marehemu na awape nguvu ndg na jamaa wa marehemu. Pia nawaombea majeruhi wote wapone haraka..
 
Waliokufa ni zaidi ya 10. Hii ni kwa mujibu wa Radio one breaking news saa 5:34 usiku wa kuamkia leo.
 
Back
Top Bottom