Hizo za walokole si roho mtakatifu bali ni ROHO MTAKAFUJO.Ndio maana wanatumia viini macho kujifanya eti wanaponya watu kwa jina la YESU.Kwa hakika YEHOVA anaweza yote na laiti angetokea nabii wa kweli akaenda pale mhimbili akaingia Mochwari akamfufua mtu mmoja tu au aende moi amponye mtu mmoja tu alievunjika mguu na kutoka nae basi Tanzania nzima ingesadiki ila walokole ni wasanii tu 'eti misule imerudi'.
nimekuelewa kiasi kwa uliloandika, ukipata wasaa jibu swali zima, likiwa na nyongeza ya dodoso uliyotoa litakaloonyesha kwa nini Yesu hakufanya ubatizo wa japo kundi dogo, japo alitabiriwa kwamba atabatiza.
Oh kumbe pasaka papa alijitungia tu.... hatari kabisa hii.Pasaka wasabato wanasheherekea kwa kunywa na kula mwili wa BWANA kiimani kama alivyoagiza na sio kwa kula pilau,kuku na bia.katika ile sinema ya YESU uliona YESU akila ubwabwa? Na kwenye biblia kuna sehemu yoyote imeandikwa kwamba pasaka ni mwezi wa nne? la hasha bali ilitungwa na papa mwaka.
Kumbe ni mungu wao mbona mnalilia kwenda kule bila visa huyo mungu wenu hellen si angewapeleka huko majuu.
Mkuu uko uliko-bold unaweza nipa maana yake.Nimerudi mkuu. Yesu mwenyewe alisema hivi Msidhani nalikuja kuleta amani duniani, la sikuja kuleta amani bali upanga. Na pia akasema Nalikuja kumfitini mtu na ndugu zake. Na sehemu nyingine akasema alikuja kuleta mifarakano duniani. Yesu alikuwa anaabudu katika masinagogi na bila shaka alikuwa katika dini ya kiyahudi(lakini sijui kama alikuwa dhehebu la mafarisayo ama masadukayo). Lakini nadhani alifuata dhehebu la mafarisayo(maana waliamini katika uwepo wa malaika, na ufufuo wa wafu).
kuna tofauti kati ya neno utaokoka na unaokoka,katika warumi 10:9 imesema utaokoka that's means ni future tense
pia neno linasema atakayevumilia mpaka mwisho ataokoka...wokovu 2lionao kwa sasa ni ule wa kifo cha yesu ambayo ni neema tu ambayo kila mwanadamu anaipata
barikiwa
Oh kumbe pasaka papa alijitungia tu.... hatari kabisa hii.
duh! hiyo red ndo nani huyo?
Nimerudi mkuu. Yesu mwenyewe alisema hivi Msidhani nalikuja kuleta amani duniani, la sikuja kuleta amani bali upanga. Na pia akasema Nalikuja kumfitini mtu na ndugu zake. Na sehemu nyingine akasema alikuja kuleta mifarakano duniani. Yesu alikuwa anaabudu katika masinagogi na bila shaka alikuwa katika dini ya kiyahudi(lakini sijui kama alikuwa dhehebu la mafarisayo ama masadukayo). Lakini nadhani alifuata dhehebu la mafarisayo(maana waliamini katika uwepo wa malaika, na ufufuo wa wafu).
Ntuzu mbona hamtoi majibu humu au maswali magumu?
Mkuu kabla sijaingia kwenye kukujibu hoja yako kwa kirefu naomba unijibu hili swali
Kabla ya Yesu kuja duniani Torati ilikuwa imehubiriwa sehemu nyingine za Dunia tofauti na Israel?
Ok, Kwa hiyo wasabato ni wafarisayo au wasadukayo? Alafu naomba unisaidie mistari inayoelezea kuwa Yesu alienda kusali kwenye Sinagogi nataka niisome zaidi.
huwa tunaongoka maana kuoka hadi ajapo yesu
Mnafiki ni wewe farisayo wa kisabato usiyeyafahamu maandiko. Warumi 10:9 inasema nini kuhusu kuokoka? Ok kama hufahamu hili soma zaburi 16:3 inasemaje kuhusu watakatifu walioko duniani? Ndio maana Paulo akaandika habari hizi mapema kwenye
2 Timotheo 3:5 , " wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao." kuwahusu watu kama nyie mnaojidai mnamjua KRISTO huku mkikana nguvu zake yeye. Narudia tena usabato ni dini ya kishetani yenye kujificha chini ya mwavuli wa BWANA YESU.Okokeni leo maana neema ipo bure.
Maswali yangu ilikuwa kuhusu pasaka,embu tueleze wasabato na kufa na kufufuka kwa Yesu,ni kwa nini hamsherekeagi Pasaka,pili ni kwa nini hamtumiagi vinywaji venye gesi?,Yesu aliposema kimwingiacho mtu hakimtii unajisi bali kitokacho kinywani alimaanisha nini?,sorry kwa kutoka nje ya mada(binafsi kunena kwa lugha sikuafiki).Mkuu nilikua nilikua na pilika Kidogo!
Naona kuna hoja nyingi sn mnazungumza!
Ebu Naomba uniulize hayo Maswali nione nitakavyoweza kukujibu Ingawa niko njiani!
Maswali yangu ilikuwa kuhusu pasaka,embu tueleze wasabato na kufa na kufufuka kwa Yesu,ni kwa nini hamsherekeagi Pasaka,pili ni kwa nini hamtumiagi vinywaji venye gesi?,Yesu aliposema kimwingiacho mtu hakimtii unajisi bali kitokacho kinywani alimaanisha nini?,sorry kwa kutoka nje ya mada(binafsi kunena kwa lugha sikuafiki).
Kama Yesu alituza Sabato mbona aliponya na hata kukemea wakuu wa sunagogi waliomkaripia(lk13:10-17)..Yesu anasema ukinipenda utazishika sheria zangu! Na ndani ya hizo sheria imo sabato!
Sheria za Mungu zimezungumzwa Ktk agano la kale na Yesu mwenyew na pia Ktk kitabu cha ufunuo!
Sasa Wewe unapo sema sabato ni dini ya kishetani kwa kigezo gani Mkuu? Na ukumbuke Kua Yesu mwenyewe alikua akitunza sabato!