Yesu alikufa siku ya Ijumaa(siku ya maandaalio ya sabato), akashinda kaburini siku ya jumamosi(sabato), akafufuka siku ya kwanza ya juma(jumapili). Hii rejea Luka 23 na sura ya 24 kama una Biblia. Hala fu wayahudi pia wanasali siku ya jumamosi(sabato). Na sabato ndio itakayoshindaniwa hadi Yesu atakaporudi, hujiulizi kwa nini .....
Asante kwa majibu yako..
BIBLIA katika kitabu cha Waefeso 4:5-6
inasema: "Bwana mmoja, Imani moja, ubatizo
mmoja, Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote,
aliye juu ya yote na ndani ya yote". Kama
maandiko yanavyosema kwamba Mungu ni
mmoja, imani ni moja, ubatizo ni mmoja,
lazima siku ya ibada iwe ni moja.
Hivyo, yatupasa tuelewe wazi kwamba kuna
mahali tumefanya makosa, maana haiwezekani
Mungu huyu mmoja atuwekee siku mbalimbali
za ibada kiasi hiki, na kutufanya
tuchanganyikiwe na kujiuliza ipi ni ipi.