Waraka wa wazi kwa Viongozi wakuu wa Kiroho Nchini

dalalitz

JF-Expert Member
Sep 6, 2013
3,332
1,862
Heshima kwenu.

Huwa nashangaa yanapojiri baadhi ya matukio Nchini ambayo yanagusa maswala ya Imani, Waumini ama
Viongozi wengine wa Kiimani.
Huwa najiuliza ni kwa nini viongozi hawa wawili,
Yule wa Wakristu kwa upendo mmoja na yule wa Waislam kwa upendo mwingine, ambao naamini ndio wakubwa zaidi kwa taasisi za kiimani Nchini,
Wao hawa, wanakuwa wazito kujitokeza na kutoa maoni yao,
Misimamo au hata kuwa na kauli za kuionya au kuikaripia serikali hasa pale inapoonekana serikali inafanya ndivyo sivyo.

Sitaki kuamini kuwa siku zote serikali inapatia tu, kuwa hawa masheikh na wachungaji wanao-'shughulikiwa' kuwa siku zote ni wakosefu?

Nilidhani ninyi ndio viranja wa taasisi na viongozi walio chini yenu pale wanapokwenda kombo.

Simaanishi kuwa mjenge uadui au muwe wapinzani kwa serikali au kuwa muwe mtetezi wa viongozi wa taasisi zilizo chini yenu hata katika mambo ya hovyo,
-la hasha.

Ila ingetarajiwa ninyi muwe mtetezi na kimbilio la walio chini yenu wakati huohuo msiionee haya Wala uoga serikali inapokoroga mambo.

Matokeo yake wenzetu mmekuwa watu wa kauli nyepesi kwa mambo mazito.

Hii si sawa.

Kwa mamlaka mliyonayo ninyi ni baba wa serikali.

Kusema tu mnataka amani,
Mnataka amani ilhali inaoonekana wakati mwingine kuwa HAKI inavunjwa?

Kuota au kuhimiza amani pasi kusimamia HAKI ni bure.

Zama tulizonazo ni za kufuata Sheria lakini Sheria zenye kuzingatia HAKI Na UHURU.

Nawasilisha.
 
Wanaogopa kupotezwa kwenye ramani. Ndo ujue na wao wapo kama sie tuu hawana imani kuwa kupitia wao wanaweza kubadilisha baadhi ya tabia ngumu za waamini wao,kupitia wao na maonyo yao wanaweza wakawapa hofu ya Mungu waamini wao ila na wao kwa sasa wamekua waoga. Hapo ndipo shetani atatawala zaidi na mtu mmoja kujifanya Mungu yupo juu ya sheria
 
Heshima kwenu.

Huwa nashangaa yanapojiri baadhi ya matukio Nchini ambayo yanagusa maswala ya Imani, Waumini ama
Viongozi wengine wa Kiimani.
Huwa najiuliza ni kwa nini viongozi hawa wawili,
Yule wa Wakristu kwa upendo mmoja na yule wa Waislam kwa upendo mwingine, ambao naamini ndio wakubwa zaidi kwa taasisi za kiimani Nchini,
Wao hawa, wanakuwa wazito kujitokeza na kutoa maoni yao,
Misimamo au hata kuwa na kauli za kuionya au kuikaripia serikali hasa pale inapoonekana serikali inafanya ndivyo sivyo.

Sitaki kuamini kuwa siku zote serikali inapatia tu, kuwa hawa masheikh na wachungaji wanao-'shughulikiwa' kuwa siku zote ni wakosefu?

Nilidhani ninyi ndio viranja wa taasisi na viongozi walio chini yenu pale wanapokwenda kombo.

Simaanishi kuwa mjenge uadui au muwe wapinzani kwa serikali au kuwa muwe mtetezi wa viongozi wa taasisi zilizo chini yenu hata katika mambo ya hovyo,
-la hasha.

Ila ingetarajiwa ninyi muwe mtetezi na kimbilio la walio chini yenu wakati huohuo msiionee haya Wala uoga serikali inapokoroga mambo.

Matokeo yake wenzetu mmekuwa watu wa kauli nyepesi kwa mambo mazito.

Hii si sawa.

Kwa mamlaka mliyonayo ninyi ni baba wa serikali.

Kusema tu mnataka amani,
Mnataka amani ilhali inaoonekana wakati mwingine kuwa HAKI inavunjwa?

Kuota au kuhimiza amani pasi kusimamia HAKI ni bure.

Zama tulizonazo ni za kufuata Sheria lakini Sheria zenye kuzingatia HAKI Na UHURU.

Nawasilisha.
Kumuonya mtu au kumkosoa kwaweza fanywa kwa njia nyingi, kuonana na mhusika bila kutangazia umma, barua, au kama inayotumiwa na baadhi ya viongozi wa dini n.k, kwa hii ya mwisho niliyoitaja mara nyingi wengi wa wanaoonywa hawaipendi na huwa haina matokeo mazuri kwa mkosoaji. Yawzekana viongozi wa dini uliowataja hapo walisha wasilisha maoni yao
 
Back
Top Bottom