Nadhani huyu jamaa amempendelea sana Mama Kikwete, amempa fursa ya kufanya yale haswa anayotakiwa kufanya. Wakurupukaji tu ndiyo wameshindwa kuliweka sawa.
Kwani wameshindwa nini kuhakikisha kuwa fedha zikikusanywa zinasimamiwa vizuri ili kuinua elimu ya watoto kwenye hiyo shule?
Wakati mwingine unaweza kuletewa fursa nzuri ya kuwa Raia mwema ukajiona uko kwenye nafasi ya kustahili heshima sana ukaikataa au kuichafua ile nafasi. Inawezekana sana kwa jinsi ninavyoona, kuna mtu alimuahidi huyu jamaa kwamba atamsaidia kwenda kufikisha ujumbe wake kwa Mama, lakini jamaa akaharakisha kabla hata habari hazijamfikia.
Mtu mwenye busara kukataa kusaidia shue ya watoto wadogo, labda kuna jambo tusilolifahamu hapo!