Waraka maalum kwenda kwa waziri wa mambo ya ndani kuelezea ukabila uliokithiri idara ya uhamiaji

Wadau hivi ni kwanini wachaga kila mahali wawe wanalalamikiwa, yani mpaka uhamiaji naona huu ni uzushi sababu hawa watu uwepo wao ni kutokana na elimu walizonazo.

Mkuu una uhakika unayozungumza!! Kwani makabila mengine hawana elimu?
 
Huu ni uzushi tu...hi mijamaa ya kichaga bwana inasoma we nenda vyuoni tu humo alafu angalia wachaga jinsi walivyowengi wanapiga shule balaa tofauti na makabila mengine nenda mashuleni humo na vyuoni tafuta mluguru,mdigo,mnyamwezi,mzaramo,------ na mengineyo kama utapata hata kumi ila wachaga tu ni wengi..pia kwenye kutafuta jamaa wanajua bwana we nenda kijiji huko mkoa mwingine kabisa kama hutakuta mangi anauza duka au anachoma mbuzi....tuache ulalamishi sa nyingine tupige kazi bwana na tuhamasishe na sisi ndugu zetu wasome waje wapambane..
 
Bado na TRA nayo imejaza wachagga

Waende Chuo Kikuu chochote! Wachukue orodha ya Majaji kabla ya utawala wa JK wa kuteua majaji! Wakishamaliza huko waende tena mitaani, waangalie mafundi saa, simu, wapiga rangi viatu, fudni cherehani, halafu mafundi waashi, halafu waende ofisi za uchoraji nyumba.....halafu wakaangalie mapadre wangapi wachagga Dar halafu Zanzibar, halafu Mtwara....wakishatoka huko waende shule za vijijini kule Nachingwea waone walimu wachagga ni wangapi....mbona mwajitesa! Mchagga ni nani? Aliyesomea Uchagani? Aliyezaliwa Uzaramoni? Aliyeolewa Usukumani? aliyekulia Dar? Uchaga ni nini? Acha ukabila utakutafuna!

Oh nilisahau na masheik kule Arusha, hapa Dar na kule Dodoma!
 
Uongozi dhaifu, mambo huenda mrama. Rai imetolewa wahusika wachukue hatua. Waite agency iwachape usaili watakaoonekana bomu waondolewe mara moja. Wachaga chapeni kazi survival for the fittest hata kama ni kwa mlango wa nyuma tuliifungua hiyo milango wenyewe! Ifungeni lakini hawa jamaa watapitia ya mbele bila wasiwasi. Big up Wachaga.
 
alioandika ho waraka ana chuki tu...angalia idadi ya wanaomaliza vyuo ,shule kama ungeweka ukabila na maksi zao ungejua angalia wanaosoma shule nzuri zenye viwango utajua.....angalia watu waliopo kwenye idara hizo wengi ni wapi.............sasa kama uhamiaji wengi ni wachaga unategemea viongozi watoke wapi ?waliosoma zaidi shule wachaga unafikiri hizo kazi wamuajiri nani,,,,,acheeni ujinga someni...wachaga wan bidii katika kila jambo wafanyalo wanaojaribu kuiga nao pia hufanikiwa......hata biashara za bar nyingi hoteli nyingi ni wachaga...teh teh.....mmekalia ushirikina tu.....
 
wadauuu...
KWA MTAZAMO WANGU...
Ngoja tuweke sawa kitu, mnadhan ni UCHAGA TUU...
Labda mngesema ni UNDUGU WA KICHAGA, kwa sababu wachaga kibao walishaomba kazi hapo wakakosa, ila kama kuna mtu mnafahamiana na ni ndugu yako ndio unanafas ya kuajiriwa pale...
Na ili linawezwa fanywa na kabila lolote tz.
Sio vizuri ukaweka wachaga wote kama waraka ulivyo.
Pili ni vyema wa Tz tukawa na umoja na kujaliana bila kuangalia makabila yetu, leo ile kasumba ya kuoana kimakabila inapotea na inaweza fika kipindi tukuwa tunajua lugha nyingi kw sababu ya muunganiko huu.
Pia ni vyema watu waka wanajitaidi kuwapa watoto wao elimu hasa wa KIKE, leo hii tunasema wachaga,wahaya,wanyakyusa,wasukuma,wabena,wakinga wanajitaidi saaana kwenye elimu,ni ngumu kidogo kwa msomi kunyenga mahusiano/kuona na mtu asiye na elimu.Kw hiyo kama kutakuwa na muinuko na ushindan wa elimu ni vyema itapelekea kunyenga usawa ktkt maisha.
SHUKRANI.
 
alioandika ho waraka ana chuki tu...angalia idadi ya wanaomaliza vyuo ,shule kama ungeweka ukabila na maksi zao ungejua angalia wanaosoma shule nzuri zenye viwango utajua.....angalia watu waliopo kwenye idara hizo wengi ni wapi.............sasa kama uhamiaji wengi ni wachaga unategemea viongozi watoke wapi ?waliosoma zaidi shule wachaga unafikiri hizo kazi wamuajiri nani,,,,,acheeni ujinga someni...wachaga wan bidii katika kila jambo wafanyalo wanaojaribu kuiga nao pia hufanikiwa......hata biashara za bar nyingi hoteli nyingi ni wachaga...teh teh.....mmekalia ushirikina tu.....

Mkuu huo ndo ukweli tuache kuwalaumu wachaga hawa jamaa wanajituma sana na wanajua sana kupambana na maisha!
 
someni na fanyeni kazi kwa bidii, hata wakiondolewa wote leo watarudishwa tena tu kwani ni wachapa kazi. Ingia mtaa wowote wa nchi hii hautakosa duka la mangi, je? na huko ni nani aliwapendelea?

MImi ni Mchaga na sijipendelei
hata kama Mchaga hajasoma lakini anajituma na kupambana na kwa taarifa tu ni kwamba tunathubutu kufanya mambo ambayo wengi hawawezi
kuna wachaga wanasafiri kwenda china na taiwan kuchukuwa mizigo na jamaa hawajui kiingereza wala hawajasoma
nafikiri imefika wakati watanzania wakubali kwamba wachaga wanachangia sana kwenye kubadilisha uchumi wa taifa letu
wote tungekuwa kama wakwere kukaa vibarazani kutwa kucheza bao tungefika??kaa chini tafakari
 
MImi ni Mchaga na sijipendelei
hata kama Mchaga hajasoma lakini anajituma na kupambana na kwa taarifa tu ni kwamba tunathubutu kufanya mambo ambayo wengi hawawezi
kuna wachaga wanasafiri kwenda china na taiwan kuchukuwa mizigo na jamaa hawajui kiingereza wala hawajasoma
nafikiri imefika wakati watanzania wakubali kwamba wachaga wanachangia sana kwenye kubadilisha uchumi wa taifa letu
wote tungekuwa kama wakwere kukaa vibarazani kutwa kucheza bao tungefika??kaa chini tafakari

Na tuombe mungu mchagga asipate u rais.Mbona mtatumaliza
 
asilimia kubwa ya wachaga ni wakristo na hapa nchini kuna malalamiko ya kuhusu wakristo kutawala serkali...sasa hapa inabidi mfikirie kwa umakini je huo ni udini au ukabila...kutoka mfumo kristo to chagalism mbona kazi hipo tanzania...
 
jaribu kufanya utafiti, nenda chuo chochote kusanya watu kumi, trust me 6 wanatoka kilimanjato, unategemea nini

si sita tu. Yawezekana nane kabisa. Hawa jamaa wanasoma shule na kuitafuta popote pale. Ukiingia kwenye vyuo vya diploma wamejaa kuanzia kwao mpaka tandala makete huko wakati mhehe wa iringa ukimwambia aende tandala anakataa na kusema kijijini haendi.
 
Ukiona hivyo ujue mwakyembe au magufuli ndo anaweza kuondoa uchafu huo
 
Ndugu yangu, mimi nipo kwenye kampuni moja binafsi. Managers wote Watano including HR sio wachaga...ila wafanyakazi 8 kati ya 23 ni wachaga. Sijui hapo utasemaje..Na kila mmoja amekuja kivyake.

Ukienda kwenye mabenki ndio utashangaa. Darasa nililokuwa nasoma chuoni karibu nusu ya darasa walikuwa wachaga. Nashauri hili swala tuanze kulitazama kwa jicho la tatu. La sivyo tutaendelea kuwa watu wa kulalamika tuuu.
 
Nimeshangaa kumbe yule Kamishna wao HAJAAPISHWA hadi leo! Ni kumtega ili awekwe mchagga? Ila mwandishi alipaswa asimumunye maneno, aseme yupi kawekwa wapi na hasitahili, aliyestahili ni fulani kwa vigezo a, b, c na sio ilivo sasa. Hata kama ni ukweli ni rahisi mno kuamini kuwa kilichoandikwa ni matokeo ya 'wivu wa kike' [ashakum si matusi]
 
MHE: WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI TUNAOMBA USHUGHULIKIE UKABILA HUU NA RUSHWA HII NDANI YA IDARA YA UHAMIAJI.

Mhe. Waziri Nchimbi huu ni sehemu tu ya matatizo ya Idara ya Uhamiaji na tumeonelea tuguse maeneo makuu mawili ambayo kwayo madhara mengine yametokea. Mosi ukabila,Idara kwa sasa inaongozwa na wachaga na kurithishana madaraka kwa ajili ya kulinda mtandao wao. Muasisi wa mtandao huu ni Kishe ambaye kwa sasa yupo Namanga kama mfawidhi. Huyu ndiye aliye mleta Mongi, Shayo, Kasike, Mtenga, Mgonja na Kumuwekea mazingira ya kuwa mwanasheria wa idara Hannerole Manyanga .

Hawa wamekamata utawala na kwa kupitia ofisi hiyo wameajili na kuwapangia wachaga na wapare kwenye maeneo ya mikoa mikubwa ambako wanawasapoti kwa kuhakikisha wanapewa upendeleo katika nafasi za fedha hata kama hawana sifa hizo. Ukifanya utafiti utagundua kuwa mchaga mwenye ufaulu mdogo ata ajiliwa akiachwa mtu wa kabila lingine mwenye ufaulu mzuri hivyo idara sasa inaajili watu wa kawaida sana tofauti na hapo awali. Tabia hii ya kuajiliana na kupangiana vituo imetengeneza mtandao wa kupeana pesa, yaani wanageuzana ni chanzo cha mapato cha walio wasaidia kupata kazi ama kituo.

Tabia hiyo imejenga tabia ya watumishi kuona kua bila pesa huwezi saidiwa kwani vijana walio waajili wanaongoza kwa matendo yasiyo ya ki utumishi wa umma,maana wanajua kazi yao ni kupeleka pesa na hakuna wa kuwawajibisha. Hawa ni maarufu kumtengenezea mtu kashfa hasa anayetishia kuuvuruga mtandao wao bila ya yeye mwenyewe kujua.

Ebu angalia namna walivyo mpatia cheo DCI Mongi ili arithi na kuficha siri za Shayo. Huyu Mongi hakuwepo wakati vyeo vya mkululo (U Kamisha msaidizi) vilipo tolewa alikuwa katika tume ya utumishi wa umma, na alipo rudi kwa namna ya mashaka , yeye binafsi alikua mmoja wapo wa kutaka kuvifuta, kwani baada ya kuona mchakato utachukua muda mrefu akaanzisha mchakato wa yeye kujipatia cheo.

Wakimtumia Joseph Francis Kasike na Hannerole Manyanga (Mwanasheria) kuomba cheo hicho kupitia Ofisi yako na kushindwa kupewa mara mbili kwa hoja kuwa bado utumishi Wizara wanavifanyia kazi , huyo Kasike akaamua kwenda utumishi kuu na kumuona Bwana Mlay ambaye yuko utumishi kuu Ikulu, kwa nafasi yake akampatia cheo ndugu Mongi eti idara ime muombea cheo. Sasa amepangiwa kazi ya Nduguye Shayo mwenye tuhuma ya uchakachuaji wa permit za Idara.

Mhe. Nchimbi sisi hatuna ubaya na hawa watu na tunafanya kazi nao lakini tabia zao zina tupelekea kujiuliza mustakabari wa Idara hii kwa vizazi vijavyo. Ebu angalia na hii ya hivi karibuni ambayo imetokea Tanga. Kuna afisa anaitwa Erasimus Francis ambaye naye ni mchaga, alihamishwa toka Arusha kwenda Pangani kama adhabu baada ya uchakachuaji wa permit huko Arusha. Huyu afisa aliondoka kituoni kwake takribani miezi sita bila ya ruhusa na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa kwake na afisa uhamiaji Mkoa DCI Nyaki (mchaga) , kama alivyo wachukulia Afisa Gervas Mpangie wa Tanga, ambaye ni mgonjwa wa moyo na kutokana na maradhi yake ambayo ofisi inajua alienda matibabu na kuchelewa kurudi sasa ana jibu mashitaka, na kama alivyo chukuliwa Ghalib Yusuph wa Tanga ambaye alizidisha siku za likizo kwa sababu za kuuguliwa na wazazi, sasa anajibu Mashitaka.

Bali kwa huyu mchaga hali ni tofauti. Hakuna barua toka kwa RIO Tanga. Lakini Honelole Manyanga, Joseph Francis Kasike na Mary stella( PHRO – Mpya nayeye Mchaga). Wamemtafuta na kumtaja Erasimus Francis kama msomi mzuri hivyo hawawezi kumpoteza na wamemhamisha toka Pangani hadi Chuoni Moshi TRITA, na kumpeleka training ili apate pesa kwani Idara ili mchanganya (frustrate) kwa kumpeleka pangani, kuna maafisa wazito na weredi wa kazi za idara sana wamenyanyasika na adhabu za visingizio hapa idarani hatuja wahi waona wakithamini ujuzi na uzoefu wao na waliishia kuacha kazi ama kuishia kulewa tu mpaka wanakufa au kustaafu .

Hivi hii ni nini? Kama si kulewa madaraka, ebu niulize ni watumishi wangapi ambao si wachaga wametendewa hivi? Na Kwanini vikao vikaliwe vya watu wa kabila moja? Mhe. Waziri Idara ina wasomi wengi mno na wenye uelewa mkubwa wa masuala ya fani mbalimbali lakini aliye katika mtandao huu Mchaga ndiye bora kuliko wote. Wamejenga utamaduni wa mkono mtupu haulambwi. Mtandao wao unaigharimu Idara, Umebadili dhamira ya kuwa Afisa uhamiaji ni mtumishi na badala yake Uhamiaji imekuwa ni kusaka fedha kwa njia zisizo halali kwani wapo watakao kulinda na kukutetea.

Wachaga ni watumishi wa vituo vilivyo vikubwa tu, huwezi kuwakuta Pemba ambako tunapelekwa siye tukionekana ni kero kwao bali wao ni wasomi wazuri waa Idara (si wao haiwezi kuwapoteza). Wana haki ya kutamba maana wamefanikiwa kukamata Idara ya Fedha- Peniel Mgonja, Joseph Mtenga -Planning, Msaidizi wa Mhasibu mkuu Jane Temu na Ludovick Kavishe – system wameikamata idara wanaweza kushawishi na kutekeleza walio jipangia bila kubainika wala wasiwasi. Hapo idarani kuna watumishi wenye CPA nab ado hawajawa wasaidizi wa Chief Accountant, hata walio jaribu kuwa wasaidizi wasio wachaga walifanyiwa zengwe na kuondolewa, angalia wakuu wa vitengo wengi wao ni hao hao Wana wa Israel.

Permit yupo Dawson Mongi, Passport yupo Hilgat L Shauri. Legal yupo Hannerole, Utumishi yupo Mary Stella na Joseph Kasike, Manunuzi yupo Mshana na Transpot yupo Musa. Mtandao huu umetumika vibaya kwani hata baadhi ya Maafisa uhamiaji mikoa wametumika kuu imarisha. Kwa tabia mbaya za maafisa hao wa Mikoa kupenda kuwa nyanyasa watumishi na kuwatishia kuwa hamishia vituo vigumu kama manyara,Pemba, Lindi,Songea , Rukwa na Mtwara watumishi wasio kubaliana na utendaji wao mbovu wame jikuta wakiwapigia magoti wana mtandao hawa ili kutimiza adhima yao.

Mhe. Nchimbi, ukienda mikoani tembelea makao makuu ya mikoa na kituo chochote cha mpakani ambacho kipo active, utaona idadi ya wachaga waliopo hapo na sehemu walizo pangiwa. Wanapangiwa sehemu ambazo hawaja somea na kuna wasomi walio somea sehemu hizo. Hawaoni shida hata wakiwa wote kwenye kitengo kimoja wao ni wa ISRAEL , na sisi wengine ni Wapalestina ndivyo wanavyo jiita na kutuita. Kwa kua eti wana IGP, Mkuu wa Magereza, Na Uhamiaji wata Muweka Hannerole Manyanga kuwa kamishina mkuu wa Uhamiaji. Na sisi tunasubiri utimie unabii wao.

Lakini tuna jiuliza kama hali ndiyo hii kuna uwezekanao mkubwa kuwa mtandao wao si mdogo bali ni mkubwa na upo hata nje ya Idara na Wizara. Mhe Nchimbi hii ni dalili ya mvua au mvua kamili maana tayari picha unaiona. Uteuzi Ma RIO wa hivi karibuni ni kero kabisa una fanana na kinachoendelea kwa jirani yetu. Towo – Lindi, Kombe – Kagera, Rose – Njombe, Nyaki – Tanga, Mlay na Mosha – Tunduma, Kishe – Namanga, Masawe – Dodoma, RIO - Dsm. Sasa wamemsogeza Arnold Munuo toka Lusumo kuja Dar es salaam kuja kuandaliwa kushika nafasi ya utumishi na hali wapo watu waliobobea na wasomi wapo vitengo vingine.
Mtandao huu si kwa manufaa kwa nchi au Idara bali ni kwa manufaa ya matumbo yao na jamaa zao, tabia hii uambukiza kwani waswahili usema ukiona huwezi kuwashinda basi ungana nao, hivyo Viongozi wengine wengi wame ungana na Mtandao huu ili kuficha maovu yao. Sisi tuna jiuliza kweli serikali hailioni hili na kama inaliona inakaa kimya kumaanisha nini? (Sisi tuna hofu isije ikawa ndiyo labda serikali yote imekuwa mdau wa mtandao wa wachaga.) . Huyu Mary Stella Majula (PHRO) yeye kaja na jukumu la kuwa shughulikia watu wa kanda ya ziwa eti ni wengi hapo makao makuu, na hali yeye anaenda kwao (Moshi-Marangu)kila mara, akitumia pesa za serikali na hali hatujui huko anafanya nini au idara iko Kilimanjaro tu?

Tabia ya kuwawinda watu wa kanda ya ziwa ni hatari kubwa kwa watumishi, sisi tuna dhani hataishia hapo ataendelea kuwashughulikia na watumishi toka kanda ya kati, Kusini, Kusini nyanda za juu na Mashariki kwani kaletwa kusafisha njia ya wana wa Israel, kuu pata Ukurugenzi

Wafuatao ni wanamtandao waliopo Makao makuu na viongozi wao wenye majina yaliyo nakshiwa.
1.Peniel Ombeni Mgonja 2. Isaack Bahati Fota 3. E Crymont Nsowela 4.Dawson Emil Mongi
5. Nandula Patience Kombe 6. Anna Kyara Michael 7.Hannelore M Manyanga 8. Rogate Mingo Daniel
9. Joseph Henry Mtenga 10. Lusarago D Mreka 11. Gloria W Mbasha 12. Peter William Lemery
13. Kale sylivia Joseph Utouh 14. Violeth Kiwelu Eliabu 15. Felis Bilauri Mshana 16.Abdallah Musa Msangi 17. Liberatus Stanley Njuu 18. Mary Stella Majula 19. Joseph Francis Kasike 20. Sifael Stephen Tendwa 21. Novatus Aloyce Mlay 22. Beatrice Anamensa Kanza 23. Adinani Kidah Musa 24. Hendrick Fraita Mtui
25.Zakayo Leonard Lema 26. Novaita Edmund Mrosso 27. Moses Ismail Malisa 28. Dotto Roman Selasin
29. Christian Bernard Daat 30. Liberia Onesphony Manyanga 31. Christian Francis Mndeme 32. Frida Frant Maeda 33. Happiness William Kambuga 34. Triphonia Joseph Kinebo 35. Laurentia Isdom Blasius 36. Hilda Dawson Uiso
37. Tunu Mfinanga Asili 38. Marylen Msangeni Elisaria 39. Francis Noel Katawa 40. Irene Abel Mlack 41. Prosper Dions Mushi 42. Fasiruni Shabani Msofe 43. B Roman Kereti 44. Arnold Remy Mrema
45. Damian Roman Chikwa 46. Magreth Johnson Ngomuo 47. Hyasinter Ndewingla Tarimo 48. Salome Edgar Bolly
49. Gelard Honest Kawishe 50. Glory Ephraimu Mbuya 51. Hilgat Laurent Shauri 52. Paul John Mselle 53. Rose Robert Shayo 54. Patric Boniface Ngowi 55. Peter Jerome Kundy 56. Lucy Anselm Nyaki 57. Donald Lyimo Dustan 58. Siana Manasseh Kidin 59. Epiphania Joseph Lyimo 60. Juliana Selestine Mnerey
61. Lilian Humphrey Maleko 62. Raphael Timothy Maembe 63. Beatrice Elineema Lema 64. Lilian Emmanuel Lema 65. Irene Fraterine Lyamungu 66. Victor Stanley Ngowo 67. Jane Temu 68. Emmanuel Elihuruma Mrema 69. David Amani Minja.70. Ludovick Kavishe.

Mhe. Nchimbi hali hiyo ipo makao makuu tu na hao tulio wa wekea vivuli ndiyo vinala wa mtandao huu katika vitengo mbalimbali. Mkakati tulio nalo ni kuanika uozo wote mikoani baada ya kukueleza ya Makao makuu kwani hata huko mtandao ume waweka wachaga kwenye maeneo wasio na sifa nayo huko mikoani kupitia Ma Rio, ama yenye kuwaneemesha wao kwa njia moja ama nyingime. Pamoja na kasumba ya kutengenezeana mazingira ya nafasi za masomo na kozi fupi na safari za nje ya nchi kwa watumishi junior wakati senior officers hawajawahi kwenda wala kutumwa. Idara hii huwezi zungumzia suala la elimu, kwani vihiyo wa elimu bado watabaki ni haohao wachaga waliozoea kubebana hata vyuoni.

Pili Rushwa, ya ndani ya Idara ni kama mazoea sasa kwani bila pesa huna cheo wala huja amishiwa unapo stahili, Imefika wakati Wana sema ``nitakufanya utakaa usipewe ofisi ndani ya Idara hii kamwe’’ hii utokea pale unapoonekana kikwazo mfano ni juzi tu, pale msaidizi wa Kishe kule namanga alipo mwambia Waziri Kagasheki kuwa incharge huwa akaagi ofisini bali kwenye mapombe tu, kilicho tokea msaidizi alihamishwa haraka sana, hali ni hiyo hiyo ipo Tunduma kwani ukimkuta Mlay ofisini basi katambikie, ila yeye amekasimu madaraka kwa Mosha na hivi sasa nasikia wanahalalisha ukaimu wa Mosha kwa kuwaondoa wale waliomzidi cheo.

Mhe. Nchimbi vyeo, kuajili na uhamisho ni rushwa isiyo kifani na mhusika mkuu ni Kasike, Mongi, Mgonja na Hannerole. Mgonja hana waku mlalamikia kwa kutajwa kwake kwani kama hanufaiki na mtandao huu anajisikiaje pale watu wanalalamika hali yeye yupo na hakuna mabadiriko, ana nufaika kwani mambo yake yanakwenda sawa, hivyo mwenye shibe hamjui mwenye njaa sisi tunajua walipo jificha tuta wauumbua wakibisha kwani tunaishi nao.

Mhe. Nchimbi tumetaja jina lako mara kadhaa na si wadhifa wako kwani una nyadhifa nyingi, hivyo tukaonelea tutaje ambayo kwayo jamii ilikutambua na kuku heshimu kwa sababu kuu mbili, Mosi Tunaomba uhakikishe Kamishna Mteule Ulungi ana apishwa ili aache visingizio kucheza karata walizo mzoesha akina Shayo, ili alione tatizo na umsaidie kuitengeneza idara katika sura ya kitaifa. Pili uungalie mtandao huu kwa mapana yake kwani ni aibu na haionyeshi usomi wetu hata kidogo. Imefikia vijana wanao ajiliwa sasa wanajua watapangiwa wapi kabla ya kumaliza mafunzo na ni lazima wapangiwe huko huko, hivyo uanza kazi leo na leo leo wanaanza kuchakachua hii ni Rushwa mbaya sana haifai.

Mwisho tuna wataka maafisa wote wa uhamiaji popote pale walipo watambue kuwa hawako salama, hivyo basi ni kujitahidi kuufichua mtandao huu na viongozi vibaraka wa mtandao huu, kwani hakuna wa kuthubutu kama hatuja thubutu. Tunakuja mikoani andaeni au tumeni kwenye email mukabila@gmail.com hii dondoo za kumpelekea Mhe. Nchimbi na Mkurugenzi wetu.

Aksante.
Nakala – PCI Ulungi.
Watumishi wote wa Makao Makuu DSM / Znbar via Kaswende – usiufiche waraka huu.
Mikoa yote ya Uhamiaji.



aliyeandika huu waraka ni shemeji yangu mmoja wa kanda ya ziwa, ninamfahamu vizuri, kwa bahati mbaya amefanya kazi uhamiaji muda mrefu hata kwao hajawahi kujenga hata nyumba ya kufikia, ndugu na wazazi wake wanateseka yeye anajenga chuki na wachaga!!!! tukimaliza kwa wachaga tutakuta si wachaga tu, kuna wahaya, wanyakyusa na wagogo, tukimaliza hawa tutaanza kuwajengea wabena kama ilivyokuwa tuhuma za Luhanjo, naona tumehama kwenye ukanda kuwa chadema ni chama cha kikanda tunaenda kwenye udini!!! Hamfany kazi ni majungu tu na kukaa vijiweni, tumewajua tutawashughulikia sawasawa, anayetaka kupata cheo ajitahidi awe na elimu na uzoefu mzuri uliotukuka na si kwa propaganda hizi za kipumbavu!!! lkn shemeji tumeshakujua na tutakushughulikia uende zako usukumani ukachunge ngo'ombe
 
Kama waziri husika hatafanyia kazi tuhuma hizi yeye si waziri wa kudumu katika wizara hii atakuja waziri mwingine TYPE ya MAGUFURI atafanyia kazi tuhuma hizi na yeye atabakia kuwa historia ya kushindwa kutatua matatizo ya wananchi.
 
Hili si jambo la kupuuzwa. Kuna kitu muhimu cha kufuatiliwa. haiwezekani kabila moja liwe na watu 70 katika Idara moja-tena makao makuu pekee.
 
Back
Top Bottom