Waraka Maalum kuhusu URAIS kwa Wajumbe wa Kamati Kuu CHADEMA

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Wajumbe Kamati Kuu,

Kwa heshima kubwa nawaandikia waraka huu mfupi kuhusu jambo moja ambalo ni la msingi kabisa na ambalo wanachama wa kawaida kabisa wangependa ufafanuzi mapema iwezekanavyo. Nimeona nitumie njia hii ya kupitia mtandao wa Kijamii wa JF nikiamini ndiyo njia bora zaidi kwa sasa na wajumbe wote wa kamati kuu kwa namna moja au nyingine ni watumiaji wa mtandao huu maarufu wa JF.

Kwanza niwapongeze wajumbe wote wa Kamati Kuu na wanachama wote kwa ujumla kwa juhudi kubwa mnazofanya kwa pamoja kupitia Vuguvugu la Mabadiliko-M4C ambalo kwa kiasi kikubwa limewekiweka chama chetu katika nafasi nzuri sana hasa katika maeneo ambako vuguvugu hili limepita.

Ni takribani miezi mitatu sasa tangu kuanza kwa mjadala mpana hasa kupitia vyombo vya habari,mitandao ya kijamii na mijadala ya kawaida mitaani kuhusu UGOMBEA WA URAIS NDANI YA CHADEMA.

Ikumbukwe kwamba mpaka sasa wanachama WATATU wa CHADEMA wameshatangaza Rasmi nia zao za kugombea URAIS wa Tanzania kupitia CHADEMA mwaka 2015.Wanachama ambao wameshatangaza nia zao ni Mhe. John Magale Shibuda (Mbunge wa Maswa), Deogratius Kisandu(Katibu wa BAVICHA-Tanga) na Mhe. Zitto Zubeir Kabwe(Naibu Katibu Mkuu Bara- CHADEMA)

Ni ukweli ulio dhahiri kuwa wanachama hawa watatu waliotangaza rasmi nia zao hawajavunja Katiba wala kanuni yoyote ya chama lakini pia ni wazi kutangaza kwao kumesababisha sintofahamu kubwa ndani ya chama.


Athari kubwa zinazoonekana za wazi mpaka sasa ni:

* Kabla ya wanachama hawa kutangaza nia zao mijadala mbalimbali katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ilitawaliwa zaidi na Harakati za chama katika kujiimarisha kupitia Vuguvugu la M4C lakini sasa mijadala hiyo imehamia kujadili URAIS ndani ya CHADEMA kitu ambacho ni furaha kuu kwa maadui wa CHADEMA.

*
Makundi ndani ya Chama - Ifahamike kwamba CHADEMA inapaswa kuepuka kwa kila hali makundi ya aina yoyote ili kujitofautisha na vyama vingine vyenye makundi na yanayohatarisha uhai wa vyama hivyo. Tutakuwa tunajidanganya sana tukidhani kwamba hakuna watu wanaowaunga mkono wanachama hawa watatu ambao kwa lugha rahisi watakuwa tayari wanaunda mtandao wa watu watakaowapigania ndani ya chama ili majina yao yapitishwe na vikao wakati ukifika. Tufahamu kwamba hata kama watakuwa wanaungwa mkono na watu watano watano kila mmoja wao basi tayari hayo ni makundi na tayari hiyo ni mitandao. Tufahamu kwamba takriban bado miaka mitatu kufikia uchaguzi mkuu ujao!!


*
Nilikuwa katika safari zangu za kibiashara huko Kishapu na nilishangaa kukuta wanachama wa kawaida kabisa wanaokaa vijiweni wakilalamikia hatari inayonyemelea chama chao kwa kile walichodai ni malumbano ya kusaka madaraka.Wakawa na hofu kwamba chama chao kitaishia kama NCCR ya wakati huo.Nilishtuka na sikuamini kusikia hayo kutoka kwa wanachama wadogo kabisa wa kule Kishapu.


Nimalizie waraka wangu huu kuiomba Kamati Kuu ya CHADEMA pindi itakapokutana ijadiliane hili swala kwa uhuru kabisa na kujaribu kutizama athari zilizoko mbele ya chama endapo kama hali hii itaachwa iendelee ingawa hakuna kanuni wala katiba iliyovunjwa.

Kamati Kuu ijiulize swali:
Je, Viongozi kama kumi kila mmoja akitangaza nia hiyo miaka 3 kabla ya uchaguzi mkuu umoja wa chama kweli utalindwa
? Je, kunaweza kuwa na watangaza nia kumi kwa mfano halafu wasiunde mitandao ya kuwaunga mkono ili wapitishwe na vikao vya juu?


Si kazi yangu kutoa majibu ya maswali haya bali kwa niaba ya wanachama wengi na wapenzi wa CHADEMA tunaomba Kamati Kuu ije na majibu ya maswali haya na mwongozo kwa ujumla kuelekea 2015.

Naomba kuwasilisha.

Molemo.
 
Alhsante mkuu nadhani wahusika watalifanyia kazi ni wazo zuri lenye kujenga !
 
ungewashauri wamchukulie hatua yule msaliti mkubwa zitto kabwe kwa kuanzisha upuuzi huu,nani asiyejua kuwa huyo jamaa anatumiwa na ccm ili kuvuruga chama chetu,kama hatumiwi atuambie anaongea nini na dhaifu wanapokaa kitu kimoja kwenda wanakokwendaga
 
Naunga mkona hoja, kila rheli kamati kuu, tupo tayari hata mkisema tuwafukuze coz hawan amadhara yoyote wanafiki hao3
 
Naunga mkona hoja, kila rheli kamati kuu, tupo tayari hata mkisema tuwafukuze coz hawan amadhara yoyote wanafiki hao3

Wanachama wanachotaka ni Kamati Kuu kutoa mwongozo ambao utasaidia kuepusha mijadala isiyo na lazima kipindi hiki.
 
Molemo taitakya moghaka, wewe unajua vizuri kuwa hili halitaji kukurupuka, no room for discusing the dead issue, hebu unataka akina MBATIA, LIPUMBA NA NAPE wapate la kusema? waache wafu wazikane wenyewe. tafakari sana hilo Molemo, acha watz wawahukumu wenyewe hao waliotangaza nia, kwa sasa majority tujielekeze for M4C. Chadema kwa sasa ni chama zaidi ya chama, je umenielewa? punguza munkali kamanda, hebu unakumbuka issue ya ndg yetu chacha wangwe? Mungu yuko pamoja na watz wanyonge, hata hili litapita
 
Bwana Molemo umefanya analysis nzuri sana kwa nia nzuri ya kuimarisha CDM, nadhani wajumbe wa kamati kuu pamoja na uongozi wa juu wa CDM wanapaswa kutoa mwongozo juu ya jambo hili kwani kudharau au kupuuza jambo hili la kila mtu kutangaza nia ya kuutaka urais itaondoa umoja ambao ndio umekuwa ukiitofautisha CDM dhidi ya CCM & proccm.
Naunga mkono hoja 100%
 
Molemo taitakya moghaka, wewe unajua vizuri kuwa hili halitaji kukurupuka, no room for discusing the dead issue, hebu unataka akina MBATIA, LIPUMBA NA NAPE wapate la kusema? waache wafu wazikane wenyewe. tafakari sana hilo Molemo, acha watz wawahukumu wenyewe hao waliotangaza nia, kwa sasa majority tujielekeze for M4C. Chadema kwa sasa ni chama zaidi ya chama, je umenielewa? punguza munkali kamanda, hebu unakumbuka issue ya ndg yetu chacha wangwe? Mungu yuko pamoja na watz wanyonge, hata hili litapita

Nakubaliana na wewe mkuu.Mungu ataiepusha Chadema na matatizo yote.
 
Bwana Molemo umefanya analysis nzuri sana kwa nia nzuri ya kuimarisha CDM, nadhani wajumbe wa kamati kuu pamoja na uongozi wa juu wa CDM wanapaswa kutoa mwongozo juu ya jambo hili kwani kudharau au kupuuza jambo hili la kila mtu kutangaza nia ya kuutaka urais itaondoa umoja ambao ndio umekuwa ukiitofautisha CDM dhidi ya CCM & proccm.
Naunga mkono hoja 100%

Ni kweli kabisa.Nimeamua kuliweka hili wazi hasa baada kuzungumza na vijana wale wa Kishapu.Ninachotaka ni mwongozo wowote kutoka Kamati Kuu.Ninaamini Hekima ya wajumbe wa Kamati Kuu itatuvusha salama.
 
Hongera sana kiongozi. Nashukuru umegusa suala muhimu kwa wakati huu.
Vyote vikae pembeni tujenge chama.
 
Nakubaliana na wewe mkuu.Mungu ataiepusha Chadema na matatizo yote.
Molemo, hebu umewahi kujiuliza vile vifo ktk mikutano ya CDM vilikuwa vina indicate nini? hakika chama chetu kilikuwa kifutwe, walikuwa watumie jeshi ili kutudhibiti fujo na lolote lile ambalo lingetokea baada ya kufuta chadema, lakini mungu wa rehema akawafichua waziwazi pale iringa, sasa wanashindwa watatumia strategy ipi... Mungu atatupigania, wao wamajipanga kukiangamiza CDM naye mungu atasimama nasi
 
Mimi naona kwa sasa ni bora kamati kuu ikae kimya kana kwamba hakuna kinachoendelea na ionekane kwamba kila mwanachama ana uhuru wa kutangaza kugombea ili mradi awe na sifa zinazotakiwa na katiba ya chama na ya nchi.

Mkianza kutafutana mtakuwa mna-play on ZZK tunes maana lengo la kujitangaza kwake ni kuleta mgogoro ili baadaye chama kisambaratike ijulikane kuwa akina Wassira ni watabiri kumbe ndio mastermind wa mpango mzima. Kwa CDM kukaa kimya inakuwa sawa na mwanaume anayemfumania mkewe halafu anakaa kimya hamsemeshi kitu na kumpa mate so makubwa ya kuwaza nini kitafuata. Zitto ametumwa na magamba kupeleka mgogoro ndani ya CDM na dawa yake ni kumchunia hivi hivi.

"mwanagu ni mbishi na hashauriki" nanukuu kauli ya mama yake mzazi wa Zitto. Kizuri tutakachopata toka kwa Zito akiwa rais ni First Lady Wema Sepetu lakini maendeleo tusahau kwani mafisadi wanaomtumia hawana nia na maendeleo ya hii nchi.
 
Back
Top Bottom