Waraka Maalum kuhusu URAIS kwa Wajumbe wa Kamati Kuu CHADEMA

Waraka wangu nimeuelekeza Kamati kuu ya CDM.Wewe mwana CCM hauhusiki.Samahani sana.

Kwa nini usingeufunga kwenye bahasha ukaupeleka makao makuu ya Chadema pale Kinondoni Manyanya mtaa wa Ufipa.
 
Analysis ya Molemo ni nzuri na ya haki lakini binafsi naamini kunyamaza na kuwaacha wanachama hawa waamuliwe na nguvu ya umma ndiyo njia bora kwa sasa ku-pre empty hii move iliyopangwa na CCM kupitia washauri wao Usalama wa Taifa (TISS). Molemo, unapomsikia mtu mwenye wadhifa mkubwa kama Wassira akisimama hadharani na kubwabwaja juu ya "kusambaratika" kwa CDM kabla ya uchaguzi mkuu usidhani ni jambo jepesi au la kupuuzwa. Ujue kuna jambo lililopangwa kisawa sawa na wanategemea litaenda kadiri ya mipango yao. Kwa muda mrefu sasa CCM imekuwa ikizitumia asasi zinazogharimiwa na kodi kwa manufaa ya chama chao na baadhi ya asasi zinazotumika ni Polisi, Usalama wa Taifa na hata Mahakama. Hali hii ambayo inaeleweka vema na viongozi karibu wa ngazi zote ndiyo inayokifanya chama kutenda kwa tahadhari kubwa katika kuyashughulikia matatizo ya ndani ya chama ambayo kwa hakika mengi ni ya kupandikizwa na maadui wa chama kwa kutumia watu walio ndani ya chama wanaotumika wakiwa wanajua au bila kujua.
CHDEMA chama kilichokomazwa na mikasa na majaribu ya miaka mingi na sasa ni mali ya wananchi bila kujali jiografia, imani au hali na mwitikio wa wananchi kwa harakati za chama hiki ndiyo unaosababisha kiwewe toka CCM na vibaraka wao. Naamini kwa kufanya hivi CCM wataaibika.
 
Huyo Mufti anaendesha taasisi ipi na ilianzishwa na nani? huyo lazima umuone msema kweli taasisi yake ikiishiwa inasaidiwa bajeti na kanisa katoliki au hulijui hilo?

Tunashukuru serikali ya ccm imetekeleza ilichoahidi kwa waislam kuhusu mahakama ya kadhi.Mufti mkuu ameshamteua kadhi mkuu wa nchi.Niipongeze serikali ya ccm walau kwa hili.
 
Mkuu nakushukuru sana kwa kuunga mkono hoja yangu.Naamini Kamati kuu itakapojadili waraka huu itazingatia pia ushauri wako.Pamoja sana Kamanda.
 
Analysis ya Molemo ni nzuri na ya haki lakini binafsi naamini kunyamaza na kuwaacha wanachama hawa waamuliwe na nguvu ya umma ndiyo njia bora kwa sasa ku-pre empty hii move iliyopangwa na CCM kupitia washauri wao Usalama wa Taifa (TISS). Molemo, unapomsikia mtu mwenye wadhifa mkubwa kama Wassira akisimama hadharani na kubwabwaja juu ya "kusambaratika" kwa CDM kabla ya uchaguzi mkuu usidhani ni jambo jepesi au la kupuuzwa. Ujue kuna jambo lililopangwa kisawa sawa na wanategemea litaenda kadiri ya mipango yao. Kwa muda mrefu sasa CCM imekuwa ikizitumia asasi zinazogharimiwa na kodi kwa manufaa ya chama chao na baadhi ya asasi zinazotumika ni Polisi, Usalama wa Taifa na hata Mahakama. Hali hii ambayo inaeleweka vema na viongozi karibu wa ngazi zote ndiyo inayokifanya chama kutenda kwa tahadhari kubwa katika kuyashughulikia matatizo ya ndani ya chama ambayo kwa hakika mengi ni ya kupandikizwa na maadui wa chama kwa kutumia watu walio ndani ya chama wanaotumika wakiwa wanajua au bila kujua.
CHDEMA chama kilichokomazwa na mikasa na majaribu ya miaka mingi na sasa ni mali ya wananchi bila kujali jiografia, imani au hali na mwitikio wa wananchi kwa harakati za chama hiki ndiyo unaosababisha kiwewe toka CCM na vibaraka wao. Naamini kwa kufanya hivi CCM wataaibika.

Nimeipenda sana pointi zako kuhusu hili jambo.
 
Kwa nini usingeufunga kwenye bahasha ukaupeleka makao makuu ya Chadema pale Kinondoni Manyanya mtaa wa Ufipa.

Nani kakuambia malemo yuko umbali wa kuweza kuupeleka kinondoni
Sio kila jambo kama huna hoja unachangia unaweza hata kwenda kuosha viombo vikawa visafi
 
Nakushukuru mkuu kwa majibu mazuri kwa huyu kilaza.
"Jambo usilolijua ni kama usiku wakiza"
Kwa mbali naona mpango wa EL ukikamilika.Kwani mwaka 2015, Zitto ataleta utengano ndani ya CDM kisha kura zipungue na EL alambe urais.
Kamati kuu inabidi iwe makini sana na huyu kijana anayetumiwa.aliwahi kutumiwa pia kutushawishi watz tununue ile mitambo ya Richmond iliyotokana na Deals feki.
Hili jambo si la kulichukulia kirahisi,kuna uwezekano mkubwa sana Umri wa kugombea uraisi ukapunguzwa,kwani Hainiingii akilini mtu ambaye sidhani kama atakua 40's by then ,aanze kutangaza nia sasa.Huu mpango umeratibiwa muda mrefu sana.Kwani Zitto alitangaza kugombea Uraisi kule kigoma akiwa kwenye Kampeni za Ubunge.Tangu enzi hizo niliisha ona matatizo aliyokuwa akiyatengeneza.
Lkini Mwisho wa Ubaya ni Aibu,na sikuzote uongo na unafiki haviwezi kuushinda Ukweli
 
Thanks MANI
Lengo hapa ni kujenga na si kubomoa.

Mimi nadhani CDM tungemaliza chaguzi za ngazi zote ndani ya chama ndipo tuhamie kwenye masuala ya nani awe rais na nani asiwe rais,Katiba ya cdm ni nzuri tu pamoja na mapungufu yake machache.:A S 41:
 
zitto ni kirusi, akidhani yeye ni maarufu kuliko chama, basi anajidanganya, mwache aendelee kutumika tu, ataishia kama walivyoishia wakina khalid kabouru na tambwe hiza.
 
Ikumbukwe kwamba mpaka sasa wanachama WATATU wa CHADEMA wameshatangaza Rasmi nia zao za kugombea URAIS wa Tanzania kupitia CHADEMA mwaka 2015.Wanachama ambao wameshatangaza nia zao ni Mhe. John Magale Shibuda (Mbunge wa Maswa), Deogratius Kisandu(Katibu wa BAVICHA-Tanga) na Mhe. Zitto Zubeir Kabwe(Naibu Katibu Mkuu Bara- CHADEMA)



Source???

Naomba kama kuna barua, au fomu walijaza utuwekee hapa jukwaani...
 
Molemo na wana JF,
Tunashukuru kwa Makala yako, nimeisoma na ujumbe wako unataka Tamko ya Chama juu la hili.
Kikubwa Busara itumike kuliko Ushabiki, Upande zote mbili ziangaliwe, yaani Faida na Hasara za kuwatimua au kufanya maamuzi, maana Siasa ni Mchazo mchafu, mpinzani atatumia nafasi adimu atakayoiona.
Wananchi ndio wenye Nchi, Elimu ya Uraia ndio Silaha hapo. Elimu ifike mpaka huko Vijijini, huko ndio kwenye Tatizo kubwa.
Nawakilisha.


Wajumbe Kamati Kuu,

Kwa heshima kubwa nawaandikia waraka huu mfupi kuhusu jambo moja ambalo ni la msingi kabisa na ambalo wanachama wa kawaida kabisa wangependa ufafanuzi mapema iwezekanavyo. Nimeona nitumie njia hii ya kupitia mtandao wa Kijamii wa JF nikiamini ndiyo njia bora zaidi kwa sasa na wajumbe wote wa kamati kuu kwa namna moja au nyingine ni watumiaji wa mtandao huu maarufu wa JF.

Kwanza niwapongeze wajumbe wote wa Kamati Kuu na wanachama wote kwa ujumla kwa juhudi kubwa mnazofanya kwa pamoja kupitia Vuguvugu la Mabadiliko-M4C ambalo kwa kiasi kikubwa limewekiweka chama chetu katika nafasi nzuri sana hasa katika maeneo ambako vuguvugu hili limepita.

Ni takribani miezi mitatu sasa tangu kuanza kwa mjadala mpana hasa kupitia vyombo vya habari,mitandao ya kijamii na mijadala ya kawaida mitaani kuhusu UGOMBEA WA URAIS NDANI YA CHADEMA.

Ikumbukwe kwamba mpaka sasa wanachama WATATU wa CHADEMA wameshatangaza Rasmi nia zao za kugombea URAIS wa Tanzania kupitia CHADEMA mwaka 2015.Wanachama ambao wameshatangaza nia zao ni Mhe. John Magale Shibuda (Mbunge wa Maswa), Deogratius Kisandu(Katibu wa BAVICHA-Tanga) na Mhe. Zitto Zubeir Kabwe(Naibu Katibu Mkuu Bara- CHADEMA)

Ni ukweli ulio dhahiri kuwa wanachama hawa watatu waliotangaza rasmi nia zao hawajavunja Katiba wala kanuni yoyote ya chama lakini pia ni wazi kutangaza kwao kumesababisha sintofahamu kubwa ndani ya chama.


Athari kubwa zinazoonekana za wazi mpaka sasa ni:

* Kabla ya wanachama hawa kutangaza nia zao mijadala mbalimbali katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ilitawaliwa zaidi na Harakati za chama katika kujiimarisha kupitia Vuguvugu la M4C lakini sasa mijadala hiyo imehamia kujadili URAIS ndani ya CHADEMA kitu ambacho ni furaha kuu kwa maadui wa CHADEMA.

*
Makundi ndani ya Chama - Ifahamike kwamba CHADEMA inapaswa kuepuka kwa kila hali makundi ya aina yoyote ili kujitofautisha na vyama vingine vyenye makundi na yanayohatarisha uhai wa vyama hivyo. Tutakuwa tunajidanganya sana tukidhani kwamba hakuna watu wanaowaunga mkono wanachama hawa watatu ambao kwa lugha rahisi watakuwa tayari wanaunda mtandao wa watu watakaowapigania ndani ya chama ili majina yao yapitishwe na vikao wakati ukifika. Tufahamu kwamba hata kama watakuwa wanaungwa mkono na watu watano watano kila mmoja wao basi tayari hayo ni makundi na tayari hiyo ni mitandao. Tufahamu kwamba takriban bado miaka mitatu kufikia uchaguzi mkuu ujao!!


*
Nilikuwa katika safari zangu za kibiashara huko Kishapu na nilishangaa kukuta wanachama wa kawaida kabisa wanaokaa vijiweni wakilalamikia hatari inayonyemelea chama chao kwa kile walichodai ni malumbano ya kusaka madaraka.Wakawa na hofu kwamba chama chao kitaishia kama NCCR ya wakati huo.Nilishtuka na sikuamini kusikia hayo kutoka kwa wanachama wadogo kabisa wa kule Kishapu.


Nimalizie waraka wangu huu kuiomba Kamati Kuu ya CHADEMA pindi itakapokutana ijadiliane hili swala kwa uhuru kabisa na kujaribu kutizama athari zilizoko mbele ya chama endapo kama hali hii itaachwa iendelee ingawa hakuna kanuni wala katiba iliyovunjwa.

Kamati Kuu ijiulize swali:
Je, Viongozi kama kumi kila mmoja akitangaza nia hiyo miaka 3 kabla ya uchaguzi mkuu umoja wa chama kweli utalindwa
? Je, kunaweza kuwa na watangaza nia kumi kwa mfano halafu wasiunde mitandao ya kuwaunga mkono ili wapitishwe na vikao vya juu?


Si kazi yangu kutoa majibu ya maswali haya bali kwa niaba ya wanachama wengi na wapenzi wa CHADEMA tunaomba Kamati Kuu ije na majibu ya maswali haya na mwongozo kwa ujumla kuelekea 2015.

Naomba kuwasilisha.

Molemo.
 
"Jambo usilolijua ni kama usiku wakiza"
Kwa mbali naona mpango wa EL ukikamilika.Kwani mwaka 2015, Zitto ataleta utengano ndani ya CDM kisha kura zipungue na EL alambe urais.
Kamati kuu inabidi iwe makini sana na huyu kijana anayetumiwa.aliwahi kutumiwa pia kutushawishi watz tununue ile mitambo ya Richmond iliyotokana na Deals feki.
Hili jambo si la kulichukulia kirahisi,kuna uwezekano mkubwa sana Umri wa kugombea uraisi ukapunguzwa,kwani Hainiingii akilini mtu ambaye sidhani kama atakua 40's by then ,aanze kutangaza nia sasa.Huu mpango umeratibiwa muda mrefu sana.Kwani Zitto alitangaza kugombea Uraisi kule kigoma akiwa kwenye Kampeni za Ubunge.Tangu enzi hizo niliisha ona matatizo aliyokuwa akiyatengeneza.
Lkini Mwisho wa Ubaya ni Aibu,na sikuzote uongo na unafiki haviwezi kuushinda Ukweli

Hana ubavu...
 
Wajumbe Kamati Kuu,

Kwa heshima kubwa nawaandikia waraka huu mfupi kuhusu jambo moja ambalo ni la msingi kabisa na ambalo wanachama wa kawaida kabisa wangependa ufafanuzi mapema iwezekanavyo. Nimeona nitumie njia hii ya kupitia mtandao wa Kijamii wa JF nikiamini ndiyo njia bora zaidi kwa sasa na wajumbe wote wa kamati kuu kwa namna moja au nyingine ni watumiaji wa mtandao huu maarufu wa JF.

Kwanza niwapongeze wajumbe wote wa Kamati Kuu na wanachama wote kwa ujumla kwa juhudi kubwa mnazofanya kwa pamoja kupitia Vuguvugu la Mabadiliko-M4C ambalo kwa kiasi kikubwa limewekiweka chama chetu katika nafasi nzuri sana hasa katika maeneo ambako vuguvugu hili limepita.

Ni takribani miezi mitatu sasa tangu kuanza kwa mjadala mpana hasa kupitia vyombo vya habari,mitandao ya kijamii na mijadala ya kawaida mitaani kuhusu UGOMBEA WA URAIS NDANI YA CHADEMA.

Ikumbukwe kwamba mpaka sasa wanachama WATATU wa CHADEMA wameshatangaza Rasmi nia zao za kugombea URAIS wa Tanzania kupitia CHADEMA mwaka 2015.Wanachama ambao wameshatangaza nia zao ni Mhe. John Magale Shibuda (Mbunge wa Maswa), Deogratius Kisandu(Katibu wa BAVICHA-Tanga) na Mhe. Zitto Zubeir Kabwe(Naibu Katibu Mkuu Bara- CHADEMA)

Ni ukweli ulio dhahiri kuwa wanachama hawa watatu waliotangaza rasmi nia zao hawajavunja Katiba wala kanuni yoyote ya chama lakini pia ni wazi kutangaza kwao kumesababisha sintofahamu kubwa ndani ya chama.


Athari kubwa zinazoonekana za wazi mpaka sasa ni:

* Kabla ya wanachama hawa kutangaza nia zao mijadala mbalimbali katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ilitawaliwa zaidi na Harakati za chama katika kujiimarisha kupitia Vuguvugu la M4C lakini sasa mijadala hiyo imehamia kujadili URAIS ndani ya CHADEMA kitu ambacho ni furaha kuu kwa maadui wa CHADEMA.

*
Makundi ndani ya Chama - Ifahamike kwamba CHADEMA inapaswa kuepuka kwa kila hali makundi ya aina yoyote ili kujitofautisha na vyama vingine vyenye makundi na yanayohatarisha uhai wa vyama hivyo. Tutakuwa tunajidanganya sana tukidhani kwamba hakuna watu wanaowaunga mkono wanachama hawa watatu ambao kwa lugha rahisi watakuwa tayari wanaunda mtandao wa watu watakaowapigania ndani ya chama ili majina yao yapitishwe na vikao wakati ukifika. Tufahamu kwamba hata kama watakuwa wanaungwa mkono na watu watano watano kila mmoja wao basi tayari hayo ni makundi na tayari hiyo ni mitandao. Tufahamu kwamba takriban bado miaka mitatu kufikia uchaguzi mkuu ujao!!


*
Nilikuwa katika safari zangu za kibiashara huko Kishapu na nilishangaa kukuta wanachama wa kawaida kabisa wanaokaa vijiweni wakilalamikia hatari inayonyemelea chama chao kwa kile walichodai ni malumbano ya kusaka madaraka.Wakawa na hofu kwamba chama chao kitaishia kama NCCR ya wakati huo.Nilishtuka na sikuamini kusikia hayo kutoka kwa wanachama wadogo kabisa wa kule Kishapu.


Nimalizie waraka wangu huu kuiomba Kamati Kuu ya CHADEMA pindi itakapokutana ijadiliane hili swala kwa uhuru kabisa na kujaribu kutizama athari zilizoko mbele ya chama endapo kama hali hii itaachwa iendelee ingawa hakuna kanuni wala katiba iliyovunjwa.

Kamati Kuu ijiulize swali:
Je, Viongozi kama kumi kila mmoja akitangaza nia hiyo miaka 3 kabla ya uchaguzi mkuu umoja wa chama kweli utalindwa
? Je, kunaweza kuwa na watangaza nia kumi kwa mfano halafu wasiunde mitandao ya kuwaunga mkono ili wapitishwe na vikao vya juu?


Si kazi yangu kutoa majibu ya maswali haya bali kwa niaba ya wanachama wengi na wapenzi wa CHADEMA tunaomba Kamati Kuu ije na majibu ya maswali haya na mwongozo kwa ujumla kuelekea 2015.

Naomba kuwasilisha.

Molemo.

Mkuu Malemo

Tafakari yako inaeleweka vema, hata mie Kwenye kisima Cha kuwaza nimejaribu kudososa sana suala hili Kwa undani wake. Bado tuamini kwamba siasa Za DUNIA yote ya leo bado ni changa, nenda dunia yote Hakuna siaSa ya NCHI watayosema hii ni komavu. Zote kila siku hubadilika. Na kukopi mitazamo ya wenzetu, tukaitumia Kama yetu nadhani ni upofu wa pili.

Ni wazi toka hitimisho la uchaguzi 2010, vyama vyetu vyote vingeshaweka bayana nani 2015, atapeperusha bendera ya mbio Za Urais, Na Ubunge.. Ili kila Mtu akajiandaa kisaikolojia kujizatiti kwenye eneo lake. Na endapo Mtu hatoridhika Basi mapemaa awe ameshajiondoa na Chama kukabili mtikisiko Wa kuondoka kwake mapemaa..

Tusijidanganye, siasa zetu wananchi wanamwangalia Mtu kwanza, Chama baadae, Na kupitia mgongo wa Mtu bora hata baadhi ya wagombea wengine hushinda. Sasa endapo muda wa majeruhi, eti kamati Kuu au mkutano mkuu utamuengua Yule wananchi wampendae Basi Na mauti ya Chama yatawafika hapo hapo. Kwanini kuacha haya yatokee, ni vema Basi wataogombea nafasi yoyote ya kiuongozi hiyo 2015 wajulikane tu mapemaa.. Mambo ya uoga huzaa matakataka haya ambayo bado tutayashugudia ambayo si mazuri Kwa mustakabali Wa Chana chochote.

Mkuu Malemo umeongelea Mtu tatu lakini si hao tu mbona kila Mtu urais anautaka, Urais watu wanauona Kama udereva wa guta Sijui ,,!! Manake hata jirani yangu nae anaitaka funny enough hajui hata apitie Chama gani..kina naniuu, Perege wote wanataka kuwa marais, funny Tanzania .. Embu Hiyo Kamati Kuu ikae, iweke Sasa azimio Na hoja ya kumteua Mtu, mkutano mkuu uitishwe Na achaguliwe kiumbe wa 2015, kisha mkutano mkuu ukae tena Na uchague huko Majimboni..

Sakata la Majimboni ni fujo tu Sasa, mwenyekiti ana Mtu , katibu Wa kwake, wajumbe kila mmoja ana Mtu wake, fujo ni Kubwa sana sana.. Ujenzi Wa Chama umedorola.. Embu kieleweke ITOSHE..!!
 
Naukumbuka huu waraka wangu kwa Kamati Kuu.WanaChadema wakiona vituko vya kundi la masalia watagundua kwa nini niliandika waraka huu kwa sababu si kweli kwamba hawa watu walikuwa wanaonyesha demokrasia.La hasha walikuwa wanafanya kazi waliyotumwa!
 
Kesho natupa kadi ya CDM sipo tayari kuabika tena 2015 viongozi wanazidi kutunisha mifuko yao tu bila kungalia hatima ya chama,mji muiokote pale HUKO BAR Kabila bar med hajaitupa kwa dustbin na kuchomwa moto
 
Back
Top Bottom