Waraka kwa Mbowe na Zitto

mzee haijalishi; watakapochoka na matatizo na kuamua kweli wanataka kujiandaa kutawala wataamua la kufanya.

CHADEMA ndio imeshika moyo wa upinzani hapa nchini na wananchi wameweka matumaini juu ya Chama hiki. Wananchi wameiamini CHADEMA na kuipa wabunge lukuki kama ambavyo walivyoiamini NCCR-Mageuzi mwaka 1995. Kwa hiyo basi ni jukumu la CHADEMA kuienzi imani ya wananchi kwa kuwatumikia kwa uadilifu. Kinachotokea sasa kwa CHADEMA ni kama wamekuwa na muhemuko wa Madaraka. Kwa mfano kuna wabunge wachache sana ambao wanaojenga hoja ndani na nje ya bunge wengine ni ubabe tu na kukosa hoja. Ndani ya CHADEMA kumeanza kuonekana minyukano ya hapa na pale. Nimesikia na huko Mwanza nako hali si shwari, Shinyanga Shibuda naye ameondolewa kukaimu na ana kinyongo. Kuongezeka kwa ruzuku nako kunaleta sintofahamu ndani ya Chama. CHADEMA imeaminiwa kwa niaba ya wapinzani wote isipoangalia itaishia kuwa kama NCCR-MAgeuzi ya mwaka 2000 baada ya kunyukana. Na hii itakuwa ni pigo kubwa kwa Watanzania wote kwa kuwa watakosa imani kwa vyama vya upinzani. CHADEMA angalieni ndani ya nyuma kunaonekana kamoshi!
 
Ngoja niweke hivi: Hadi pale CHADEMA itakapobadilisha mfumo na muundo wake kama chama itaendelea kujikuta kwenye matatizo yale yale. Haitojalisha nani ni Mwenyeki, Katibu au Naibu! Walipocopy na kupaste mfumo wa CCM walinakili vile vile namna matatizo yanavyotokea ndani ya CCM. Quote me.
Kwenye CCM hakuna mtu aina ya Zitto ambaye baada ya maamuzi ya vikao anatoa msimamo wake. Walichocopy na kupaste ni majina ya vikao hivi. Kamati Kuu ya CHADEMA kimuundo ni tofauti sana na ile ya CCM.
 
Naipongeza sana cdm kwa harakati zao, kwani wanaandaa vijana amabao watakuwa viongozi baadae, ila sijaona mipango wala ramani zozote ndani ya cdm za kutaka kuichukua nchi.

Pia siri za vikao vya cdm zinavuja mapema sana, kwa sababu wapo watu waliojutolea kuwachafua baadhi ya viongozi wao.

Mfano, ikitokea zitto na mbowe wametofautiana, utayakuta yote hapa jf na magazetini, tena hasa ikiwa zitto ndiye aliyeshindwa, na walijipanga kuitumia jf sana kipindi cha kampeni, ila baada ya hapo wakaingia magazetini, naa zitto naye alivyopandwa hasira akaanza kujibu, kumbe hajui anapigana na mbowe nyuma ya kivuli cha magazeti, matokeo yake vikamshushia heshima kwa jamii.

Ila ndani ya cdm kwa wajumbe bado ananguvu ya ajabu, kwani wanachama walio wajumbe wa vikao mbalimbali wanajua ukweli ni upi, hivyo mbowe na genge lake walipoona hivyo wakatafuta namna ya kumdhoofisha ndani ya cdm pia, hapa wakafanya juu chini wakahakikisha lema na wenje anakuwa mjumbe wa kamati kuu,hilo lipo sasa wanaanza kumtumia kwenye vikao.

Mbowe take care brother.
 
TO the contrary, namshauri mbowe afanye mpango wa kumfukuza Zitto mapema iwezekanavyo ili akajiunge na CCM yake mapema badala ya kulea kidonda, Wakati mwingine dawa ya kansa ni kukata kiungo chenye kansa mapema ili kansa isienee mwili mzima, Si bure Zitto ana lake jambo au katumwa!!!

Hatoki mtu, hafukuzwi mtu, anatumia uhuru wake kutoa mawazo, yanaweza kubaliwa au la. Tatizo lako ni zidumu fikra za fulani.:israel:
 
TO the contrary, namshauri mbowe afanye mpango wa kumfukuza Zitto mapema iwezekanavyo ili akajiunge na CCM yake mapema badala ya kulea kidonda, Wakati mwingine dawa ya kansa ni kukata kiungo chenye kansa mapema ili kansa isienee mwili mzima, Si bure Zitto ana lake jambo au katumwa!!!

Kumbe chadema mtu mmoja anaweza kumfukuza mwanachama mwingine? Kama ni hivyo ndivyo basi hapa kuna walakini
 
Vijana wa ccm wanajulikana mapema humu ndani kutokana na uwezo wao mdogo wa kujenga hoja mimi nakwambia tunatumia kauli hii:Its your choice either to join us or to be against us' anguko kuu la chama tawala Tanzania ni 2015 shime wananchi njoni tulikate kichwa joka hili linalomeza maendeleo yetu

Maskini weeeeeeeeee! lait km wewe ndio msemaji wa chama, basi wengi wangekimbia chama kwa kushindwa kwako kujadili hoja na kuanza kaatack watu.Hata hivyo wewe ndio unaonyesha umetumwa ili kuwafanya watu wakichukie chama chao kwa kauli zako. By the way who are u in CDM?
 
vijana tunakiamini chama cha demokrasia na maendeleo,kwa namna kinavyosimama na kuibua na kuhoji mambo muhimu sana katika jamii yetu.

Hata wazazi wetu wanaamini chadema ndio kimbilio letu, licha ya wao kutuonya kuhusu kujitokeza mbele sana kwenye harakati za siasa, wakihofia usalama wetu.

Ila sasa viongozi wetu mnapoonekana kuvutana kwa ajiri ya tamaa za madaraka na ruzuku, ni aibu sana na ipo siku vijana wengi watafuatilia kiundani mambo ya chama chetu na ikiwa watabaini ukweli ulio tofauti na hisia zao, basi wataingia msituni kwani hawataamini mabadiliko kupitia chama cha siasa.

Ikiwa chadema hakitabadilika kimtazamo, kisera na ki-organisation, hakuna mafanikio, nawaomba sana mbowe, slaa na zitto kubalini kukaa na kushauriana.

I dnt understant wht the deal with uwenyekiti, tafadhali sana vijana vyuoni sasa wameanza kuhoji undani wa ugomvi wa mbowe na zitto kila wanapo onana.

Na ni kwa nini wanaonekana kutosikilizana hata kwa jambo la maana, tunajitahidi kujibu maswali magumu sana kutoka kwa vijana wasiojua chadema, ila tunafanikiwa kuwatuliza na kuwapa moyo, ila wakati mwingine unajibu mtu na unaona haimwingii akilini.

Please msituumize kabisaaa.

ni kweli kuna hiyo sintofahamu ya chini chini kati ya zito na mbowe;hilo halina ubishi.wote hawa wawili ni watu ambao huamini katika yale wanayosema na hili ndo tatizo kubwa.kimsingi fahari wawili hawakai zizi moja.

Nashauri,mbowe na zito wakae chini watafakari mara mbili mbili, la sivyo wote wakae kando.chadema kuna team kubwa sana ya viongozi na hakuna anaye mtegemea mbowe wala zito. Walikuwepo wazee qwetu kina bob makani na mtei,hatukusikia zihi kelele.
 
Ujamaa na kujitegemea with the AA incorporation in our constitution.Kiongozi hatakiwi kuwa mfanyabiashara ni lazima awe mkulima au mfanyakazi,na asiwe ameajiri hata house girl!!....
Hapo ndipo mnapokosea, Ujamaa na Kujitegemea ni mwongozo wa CCM...
ChademaKiongozi wa chama (sio wa serikali) anaweza kuwa mkulima/mfanyakazi au mfanyabiashara ili mradi ni kiongozi na mwenye kuelewa na kufuata itikadi za kile anachokihubiri (Hizi ni ajira)..
Mimi naelewa kazi ya Padre (katoliki) ni kufundisha tu dini haruhusiwi kufanya kazi nyingine wala biashara, hii haina maana hata Sheikh au Rabi pia hawaruhusiwi kuwa wafanyabiashara..
 
:A S cry:[/FONT][/SIZE] PORTI UNAJUA MWENYE MATATIZO NI HUYO BWANA MDOGO ZITTO. YEYE KAMA ANATUMWA NA CCM ASEME TUU. YEYE ZITTO ANAKULA HAPA NA PALE ---- ASIPOANGALIA VIZURI HAWA HAWA CHAMA CHA MAFIA WATAMMALIZA AU WATAMFANYIA KOLIMBA. UUNAFIKIRI KUSOMESHWA NA KUPEWA PESA NA GARI YA NGUVU UTAKUBALI KIRAHISI TUU.. HUYO ZITTO ANATUMIWA KUVURUGA CHADEMA NA SIJUI KWA NINI CHADEMA PIA WASIWE NA MAONO HIYO KUJUA NAKUMONDOA..
 
Chama kina katiba, sio cha mtu mmoja wewe unayesema wamfukuze unakosea, je wengine wakisema mbw anatumiwa na mtei( baba mkwe wake) utalalama ee??? ebu acha uchonganishi (blessing)
 
Hili siyo jukumu la CDM ni jukumu la wana CCM; CDM jukumu lake (na la vyama vingine vya upinzani) ni kuidhoofisha serikali iliyoko madarakani ili hatimaye wapiga kura waikatae na kuiondoa madarakani ili chama hicho kiingie madarakani kuongoza.
Kama ndio hivyo CDM wanafanya jukumu la wana CCM. Na pia wanahaja ya kubadili mbinu maana wao wanazungumza maneno yaleyale na strategy zilezile hata huko kudhoofisha kutakuwa endelevu? Sasa hivi kilichopo CDM ni kugombania madaraka na umaarufu. Na wakiendelea na kamchezo haka 2015 watakuwa hoi. Wenzao wanajipanga, ushindi ule wanauhesabu kama defeat lakini CDM huenda hawajajua what next. Wakiafanya haya maandamano miaka 5 ikifika 2015, hayo maandamano yatakosa wahudhuriaji na baadae hata sera hazitahusika. Sasa hivi wangejitahidi kujenga mizizi kule walikochukua majimbo kama ilivyokuwa Karatu na Kigoma kaskazini. Waweke miradi ya kimaendeleo kutoka kwenye fedha za chama. Fedha za ruzuku ziende kule. Na waanze kuidentify majimbo mengine ambayo wanayaweza. Siasa si kupayuka tu hadharani.
 
Hapo ndipo mnapokosea, Ujamaa na Kujitegemea ni mwongozo wa CCM...
ChademaKiongozi wa chama (sio wa serikali) anaweza kuwa mkulima/mfanyakazi au mfanyabiashara ili mradi ni kiongozi na mwenye kuelewa na kufuata itikadi za kile anachokihubiri (Hizi ni ajira)..
Mimi naelewa kazi ya Padre (katoliki) ni kufundisha tu dini haruhusiwi kufanya kazi nyingine wala biashara, hii haina maana hata Sheikh au Rabi pia hawaruhusiwi kuwa wafanyabiashara..
`tatizo lako unafkiri ki-chama na sio kitaifa,do you think people give a f**k about CDM or CCM?....we want to make our country better and our leaders more commited than those loonies you like to brag about!....ooh and i saw your post on those mitumbas,daaamn!,what a circus holler!!
 
Kazi ya chama cha upinzani katika siasa ni kukosoa,kuchambua na kuelekeza utekelezaji wa sera za serikali kwa maendeleo ya wananchi kwa njia za amani kama maandamano,mikutano ya adhara,midahalo etc, dhima ya chama cha upinzani kuchukua dola ni ya mwisho katika vipaumbele vya chama endapo itaonekana chama tawala hakina sera na utekelezaji mbovu wa kuwaletea maendeleo wananchi. ikiwa upinzan nia yao ni kuchukua madaraka tu kama walivyo ndugu zetu CUF basi ukombozi hautakuwepo Tanzania. mungu ibariki Tz.
 
Matatizo ya zito na mbowe yalianza pale tu wazee wa CDM walipomshauri bwana mdogo zito kuacha kugombea nafasi ya uenyekiti ndani ya chama ili kuepusha kukigawa chama kwa kuwa wote wawili wana influence kubwa ndani ya chama.Ikiwa wazee wa CDM walifanya hivyo ili kukinusuru chama je walibaka siasa ama walitumia busara? nyerere aliwai kumkataa kikwete asigombee urais mwaka 1995 je nyerere naye alibaka au alitumia busara?kwa kuwa nyerere aliwai kusema chama ambacho angeamia kama angetoka ccm ni CDM.
 
Wanajamii ebu kuweni waelevu hasa katika kutoa suluhu juu ya maelewano kidogo yaliyopo kati ya Mbowe na Zito. Yeyote anayependekeza kufukuzana kama suluhu amepungikiwa kichwani, aende akalale atumikie kichwa na tumbo lake. We can not solve the problem by creating another problem, kumfukuza Zito siyo suluhu ni kuongeza tatizo. Nafikiri viongozi wanalielewa na wanayo busara ya kutosha kuvumilia kuliko kufukuzana Mbowe and zito must learn how to work together they are our learned fellows, they should be believers and followrers of the philosophy of synergy that pressume their combined effects is greater than the sum of their separate individual effects, CDM as a political party we need them together not as individuals. wapenzi wa CDM na wale wanaoipenda nchi hii wahimizeni mbowe na zito kulijua hilo achananeni na viroja vya kuwa mahakimu wa uwongo na kweli. si wajibu wetu kusema nani mkosaji ni wajibu wetu kusema in politics we are not looking for angels, we are not looking for team of millitary personnel, we are in serch of politicians who feels insecure when they are alone, politicians who have a strong belief in team work and presume their major responsibility is to build a winning team, Jamii forum should be an architecture of learnning to love even at times when we feel sinned by our beloved fellows or enemies.
 
Another crazy youth who had been frustrated in CCM and imitates being a member of CHADEMA. Na kwambia na bado mtajifanya mnaipenda CHADEMA kwa unafiki mpaka mtachanachana vikadi vyenu vya Magamba na kujiunga na Chama Kubwa, CHADEMA! Hopeless you! CCM go to hell !
 
Ila wachunguzi wa mambo watafikia hatua watahoji kwa nini mbw anagombana na kila mtu, aliwahi kusikika akisema "kuliko kufanya kazi na chacha wangwe ni bora hata nilikose jimbo la tarime".

NAHITIMSHA KWA KUSEMA KUWA CHANZO NI UKUBWA ANAOUBEBA NA KUTAKA YEYE MBOWE AWE KILA KITU.
 
Unaweza kushangaa sana,sijui ni kwa nini watu wanafanya kazi zinazohitaji tafiti za kisayansi kwa speculations...
 
ni kweli tunajitahd kujibu maswali uraian lakn hao watu wawili hatuwaelewi, chondechonde chadema kumbukeni tumewekeza kwenu
 
Back
Top Bottom