Matatizo ya barua kutokufika mahali ilikopaswa kufika ni matatizo ambayo yapo katika ofisi mbalimbali za umma na binafsi.lakini jambo la msingi wewe unayeandika barua na kuweka anuani unatakiwa kuzingatia maudhui ya barua kwasababu unaweza kuandika barua mfano unataka imfikie afisa tawala,barua yenyewe imeandikwa kwa mambo binafsi na pengine unazungumzia madhaifu yaliyopo katika taasisi yake,lakini sasa hapo nje kwenye bahasha uliandika cheo kwa maana ya afisa tawala..kampuni soso..hyo barua itafunguliwa na yawezekana isifike kwasababu ya kilichoandikwa humo ndani.nini cha kufanya sasa.
Zingatia mambo haya.
1.kama barua ina maelezo binafsi humo ndani hata kama mwisho wa siku itafanyiwa kazi kiofisi hakikisha unaandika jina la muhusika.hii mara nyingi inasaidia kutowapa nafasi wapokeaji kwasababu hawajui nani ametuma na kwa lengo lipi.
2.Kama ni barua ya kiofisi hakikisha unaandika cheo na cha uliyeelekezwa kutuma kwake ili kutoa nafasi barua ile iweze kufanyiwa kazi hata pale mwenye cheo husika hatokuwepo ofisini basi anayekaimu ataifanyia kazi.
3.epuka kuandika anuani yenye jina la mtu na cheo chake ndani ya barua yenyewe au juu ya bahasha.mara nyingi kufanya hivi kunatoa nafasi barua yako kusubirishwa au kutofanyiwa kazi.kwenye ofisi mtu hutambuliwa kiutendaji au nyadhifa na nyadhifa haziondoki ofisini bali mtu.
Hvyo tambua kuna namna mbili za msingi unapaswa kuzingatia.
Address your letter in personal/private(andika kwa kutaja jina la mtu husika juu ya bahasha) or official (andika cheo/wadhifa wa mtu juu ya bahasha).
Nb.usiandike jina na wadhifa juu ya bahasha ili kuepusha mkanyiko kwa mpokeaji kwani hulazimika kufungua barua ambayo pengine ilikuwa inaeleza mambo binafsi sana na ya siri ambayo mtu mwingine hakupaswa kusoma.