Omuchimati
JF-Expert Member
- Aug 23, 2014
- 427
- 202
Assalam aleykhum wana JF,
Nimekaa na kutafakari nimetamani kunyamaza lakini nimeshindwa kujizuia kwa yale yanayotokea na kuendelea kwa jamii yangu pendwa ya Tanzania , nikiwa mtanzania halisi nilielelewa katika maandili ya kitanzania na kuitanguliza nchi yangu mbele kama mtanzania halisi mwenye dhamira safi ya kuilinda nchi yangu mpaka mauti yanikute
Nawapa pole sana familia ya Akwilina kwa msiba mkubwa uliowakuta kwa kuondokea na binti yao mpendwa. Akwiline kufuatia kifo chake kilichosababishwa na maandamano haramu ya chama kimojawapo cha Siasa kinachojinasibu kuwa ni chama cha harakati na chenye kuleta ukombozi nchini Tanzania, nawalaani kwa Nguvu zote walioleta haya maandamano, na ninawaalani tena nikiomba hatima yao iwe ni mwaka 2020, wakati wa uchaguzi.
Narejea kwenye ujumbe wangu mahsusi, wapinzani mlichokipanda ndicho mnachokivuna, wakati wa MHE Rais wetu mpendwa Jakaya Mrisho kikwete, mlimbeza , mkamtukana, ilifikia wakati hata Mhe John John Mnyika akatamka kuwa hajawahi kuona Rais dhaifu kama yeye, je mnajua madhila mliokuwa mnayasababisha kwake yeye na familia yake?
Hewala aliwavumilia hata ilifikia wakati aliwaita ikulu mkanywa , juice, pamoja na vitafunwa, achilia mbali pocket money mlizokuwa mnapewa baada ya kikao na Mhe Rais.
Mlipokuwa mnatukana, mnakebehi, mnaandamana hovyo, kuna watu walikuwa nje ya game wanwacheki tu wanasema wallah siku nikikamata hili rungu hawa jamaa watanitambua, rungu limepata mwenyewe leo mnanyooshwa mnalialia, mnatiwa ndani mnalialia, kumbukeni mbinu mlizotumia wakati ule ni hizi hizi mnazozitumia leo msitegemee kuitwa ikulu, mnywe juice,chai na baadae mpewe pocket money.
Ushauri wangu, hii nchi ni yetu sisi sote, kaeni chini mjiulize mmekosea wapi na mnapaswa kujirekebisha vip, social networks zilileta athari kwa nchi mbalimbali msitegemee kuwa hiyo mbinu mnayotumia italeta athari mnazozitegemea kama zilizotokea katika nchi hizo, tafuteni ushauri nje kabisa ya chama chenu, na isiwe kwa wale wafadhili wenu wanaowapeni pesa ili kuleta tafrani na kuzua commotion bila sababu za msingi, mtaendelea kupoteza na mtateketea kabisa.
APANDACHO MTU NDICHO AVUNACHO, MAPIGO MNAYOPATA NI MBEGU MBOVU MLIOIPANDA.
Nimekaa na kutafakari nimetamani kunyamaza lakini nimeshindwa kujizuia kwa yale yanayotokea na kuendelea kwa jamii yangu pendwa ya Tanzania , nikiwa mtanzania halisi nilielelewa katika maandili ya kitanzania na kuitanguliza nchi yangu mbele kama mtanzania halisi mwenye dhamira safi ya kuilinda nchi yangu mpaka mauti yanikute
Nawapa pole sana familia ya Akwilina kwa msiba mkubwa uliowakuta kwa kuondokea na binti yao mpendwa. Akwiline kufuatia kifo chake kilichosababishwa na maandamano haramu ya chama kimojawapo cha Siasa kinachojinasibu kuwa ni chama cha harakati na chenye kuleta ukombozi nchini Tanzania, nawalaani kwa Nguvu zote walioleta haya maandamano, na ninawaalani tena nikiomba hatima yao iwe ni mwaka 2020, wakati wa uchaguzi.
Narejea kwenye ujumbe wangu mahsusi, wapinzani mlichokipanda ndicho mnachokivuna, wakati wa MHE Rais wetu mpendwa Jakaya Mrisho kikwete, mlimbeza , mkamtukana, ilifikia wakati hata Mhe John John Mnyika akatamka kuwa hajawahi kuona Rais dhaifu kama yeye, je mnajua madhila mliokuwa mnayasababisha kwake yeye na familia yake?
Hewala aliwavumilia hata ilifikia wakati aliwaita ikulu mkanywa , juice, pamoja na vitafunwa, achilia mbali pocket money mlizokuwa mnapewa baada ya kikao na Mhe Rais.
Mlipokuwa mnatukana, mnakebehi, mnaandamana hovyo, kuna watu walikuwa nje ya game wanwacheki tu wanasema wallah siku nikikamata hili rungu hawa jamaa watanitambua, rungu limepata mwenyewe leo mnanyooshwa mnalialia, mnatiwa ndani mnalialia, kumbukeni mbinu mlizotumia wakati ule ni hizi hizi mnazozitumia leo msitegemee kuitwa ikulu, mnywe juice,chai na baadae mpewe pocket money.
Ushauri wangu, hii nchi ni yetu sisi sote, kaeni chini mjiulize mmekosea wapi na mnapaswa kujirekebisha vip, social networks zilileta athari kwa nchi mbalimbali msitegemee kuwa hiyo mbinu mnayotumia italeta athari mnazozitegemea kama zilizotokea katika nchi hizo, tafuteni ushauri nje kabisa ya chama chenu, na isiwe kwa wale wafadhili wenu wanaowapeni pesa ili kuleta tafrani na kuzua commotion bila sababu za msingi, mtaendelea kupoteza na mtateketea kabisa.
APANDACHO MTU NDICHO AVUNACHO, MAPIGO MNAYOPATA NI MBEGU MBOVU MLIOIPANDA.