Wapi bora zaidi kuoa, mjini au kijijini?

Wapi bora zaidi kuoa, mjini au kijijini?

Tatizo siyo kuoa kijijini wala mjini bali ni nani unamuoa,utamaduni wake, imani yake, mahitaji yake, vipaumbele vyake, mtazamo wake katika mchezo kula na kulana na mwisho kabisa je,anakupenda na yuko tayari kuwa nawe katika mazingira yeyote ya kiuchumi in relation to your neighbours
 
Ongeza vigezo.
Waliosoma au la
Ukumbukwe kijijini kuna sekondari za kata vyuo viko mjini zaidi

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
Apo kwenye elimu kwa upande wangu naona mambo mawili
1. Anaweza pata elimu na akatambua nafasi yake nakukuheshimu
2. Anaweza pata elimu akataka kulingana na wewe au kutaka kuwajuu zaidi (wanaleta ushindani)
 
Tabia na mwenendo wa binti husika, haijalishi ni wa kijijini au wa mjini.

Kinachojenga Tabia ya binti ni Malezi toka kwa Wazazi wake, na Jamii inayomzunguka katika makuzi yake

Njia bora ya kupata binti mwenye maadili ni kuangalia
  • Familia yake kwa ujumla ni jinsi gani wanalea watoto.
  • Kwa kijijini Wakina Bibi na Babu huwa wanatusaidia sana kujuafamilia husika, na hupewa angalizo kabisa mapema, kama kuoa basi familia ile inafaa zaidi na sio ile ne ile familia.
  • Maisha na mazingira ya mjini ni changamoto kwa makuzi na kumlea Binti, Hasa Familia (Baba na Mama) wasipokuwa makini.
  • Hivyo ndugu Dismas Mmasi jambo litakalokusaidia kupata binti bora ni; Hakikisha unafanya kila liwezekanolo kuijua vyema na kiundani familia anayotoka binti husika, kabla ya kufanya maamuzi.
  • Tafiti zinaonyesha kuwa maisha na malezi wanayoyapitia watoto wakiwa chini ya miaka 18 (hapa Familia na Jamii inayomzunguka inahusika), ndio huathiri mwenendo na tabia zao pindi wakiwa above 18.
----
Rejea hizi thread
Ok
 
Tabia na mwenendo wa binti husika, haijalishi ni wa kijijini au wa mjini.

Kinachojenga Tabia ya binti ni Malezi toka kwa Wazazi wake, na Jamii inayomzunguka katika makuzi yake

Njia bora ya kupata binti mwenye maadili ni kuangalia
  • Familia yake kwa ujumla ni jinsi gani wanalea watoto.
  • Kwa kijijini Wakina Bibi na Babu huwa wanatusaidia sana kujuafamilia husika, na hupewa angalizo kabisa mapema, kama kuoa basi familia ile inafaa zaidi na sio ile ne ile familia.
  • Maisha na mazingira ya mjini ni changamoto kwa makuzi na kumlea Binti, Hasa Familia (Baba na Mama) wasipokuwa makini.
  • Hivyo ndugu Dismas Mmasi jambo litakalokusaidia kupata binti bora ni; Hakikisha unafanya kila liwezekanolo kuijua vyema na kiundani familia anayotoka binti husika, kabla ya kufanya maamuzi.
  • Tafiti zinaonyesha kuwa maisha na malezi wanayoyapitia watoto wakiwa chini ya miaka 18 (hapa Familia na Jamii inayomzunguka inahusika), ndio huathiri mwenendo na tabia zao pindi wakiwa above 18.
----
Rejea hizi thread
Nimepitia thread zote mbili baada yakumalizi kupitia andiko lako nilichoelewa unachomaanisha katika kuamua jambo la kuowa kunahitaji umakini na kuchunguza kabla ya kuamua
 
Elimu,kazi yake,kabila lake,rangi yake,umbo lake,anapotoka si vitu vya msingi.
Oa au olewa na mtu unayempenda kwa dhati.
Hiyo ndiyo kanuni ya msingi na kuu.
Kumpenda mtu tuu haitoshi kukuhakikishia usalama wako
Kumpenda mtu hakudhibiti tamaa au hisia zake kuona na kutamani pengine
Sifa ulizojaribu kuziweka apo zinazingatiwa sana kabla mtu hajaamua kuanzisha tuu mahusiano yakimapenzi na mtu kunanguvu zakihisia zinajijenga kati yenu unafika maali unajuta kwanini ulianzisha mahusiaono nae mnaachana ila inafika maali zile nguvu za kihisia zinakushinda unakuta unarudiana nae
Kuowa unatoka mafichoni unadhirisha na mnafungwa kiimani kwamba ninyi nikitu kimoja alafu ndugu yangu uniambie nipende kwa dhati bila kuangalia mengine??
 
Nimekumbuka tu..

"Kumbuka nilikukuta kijijini sitimbi
Umebeba mahindi na furushi la maimbi
Nguvu ziliniishia mithili ya kufa maji
Nafsi nayo ikakidi kwamba mimi nakuhitaji
Kigoli mwenye umbo kama la mdori
Wala sikutaraji ungepiga nami stori
Nilifurahi kuweza kukufahamu
Na nikakuahidi subiri zangu salamu
Kwa kuwa nilikwenda tu kumtembelea bibi
Yote yaliyojiri tu kumweleza ilibidi
Wote walishangaa kusikia namtaka mchumba
Kwani vijana wengi wa mjini tuna kasumba
Wakaweka kikao ndiposa niweze kutoa posa
Niliapa kujiua iwapo ningekukosa
Walinikabidhi nirudi nawe mjini
Na nikakusisitiza mjini kuwa makini"



Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
Kuna ya P mawenge yeye hakuowa alikuwa ni dada wakazi na mkeka ulichanika binti alivyopewa simu
 
Tatizo sio sehemu unapoenda kuoa tatizo unaishi wapi kama dar au mikoa iliyochangamka atabadilika tu akikutana na mashost wakware.
Ndiyo marafiki wanabadilisha sana watu na tena mwanamke ni rahisi kushawishika kwaiyo kama utakuwa kwenye eneo unalozungukwa na watu wengi ni wewe tuu kuweka mipaka na kuelimishana uko ndani
 
Tatizo siyo kuoa kijijini wala mjini bali ni nani unamuoa,utamaduni wake, imani yake, mahitaji yake, vipaumbele vyake, mtazamo wake katika mchezo kula na kulana na mwisho kabisa je,anakupenda na yuko tayari kuwa nawe katika mazingira yeyote ya kiuchumi in relation to your neighbours
Popote unaweza vuna siyo inategemea mazao yalitunzwaje kutoa chakula bora
 
Nimekumbuka tu..

"Kumbuka nilikukuta kijijini sitimbi
Umebeba mahindi na furushi la maimbi
Nguvu ziliniishia mithili ya kufa maji
Nafsi nayo ikakidi kwamba mimi nakuhitaji
Kigoli mwenye umbo kama la mdori
Wala sikutaraji ungepiga nami stori
Nilifurahi kuweza kukufahamu
Na nikakuahidi subiri zangu salamu
Kwa kuwa nilikwenda tu kumtembelea bibi
Yote yaliyojiri tu kumweleza ilibidi
Wote walishangaa kusikia namtaka mchumba
Kwani vijana wengi wa mjini tuna kasumba
Wakaweka kikao ndiposa niweze kutoa posa
Niliapa kujiua iwapo ningekukosa
Walinikabidhi nirudi nawe mjini
Na nikakusisitiza mjini kuwa makini"



Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
Aisee huyu jamaa apone kwa kweli

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
katika kuamua jambo la kuowa kunahitaji umakini na kuchunguza kabla ya kuamua
Sahihi, Ni muhimu sana.

Maisha ya amani na furaha, ya baadae katika familia yako yatategemea MAAMUZI utakayofanya wakati wa kuchagua mke.
 
Habari zenu wanajamvi

Tushirikishane mada hii nawakaribisha kuchangia kile unachoona ni sawa

Jee wewe kama kijana unatakiwa kuchagua moja kati ya mawili unapotafuta binti wa kumuoa, jee utachagua lipi na kwanini?

1. Kumuoa binti anayetoka kijijini (hajayajua mengi na hana mambo mengi )

2. Kumuoa binti mliyekutana mjini (ameshayajua mengi na hakuna asichokijua)

Karibuni
Oa mwanamke anayekupenda na anayejielewa na kujitambua mwenye hofu ya mungu ana aliye anayeheshimu maagano

Haijalishi katoka mjini au kijijini


La sivyo utaolea wenzio(bila kujali alipotoka)
 
Back
Top Bottom