Wapi bora zaidi kuoa, mjini au kijijini?

Wapi bora zaidi kuoa, mjini au kijijini?

DMmasi

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2020
Posts
609
Reaction score
965
Habari zenu wanajamvi

Tushirikishane mada hii nawakaribisha kuchangia kile unachoona ni sawa

Jee wewe kama kijana unatakiwa kuchagua moja kati ya mawili unapotafuta binti wa kumuoa, jee utachagua lipi na kwanini?

1. Kumuoa binti anayetoka kijijini (hajayajua mengi na hana mambo mengi )

2. Kumuoa binti mliyekutana mjini (ameshayajua mengi na hakuna asichokijua)

Karibuni
 
Habari zenu wanajamvi
Tushirikishane mada hii nawakaribisha kuchangia kile unachoona ni sawa

Jee wewe kama kijana unatakiwa kuchagua moja kati ya mawili unapotafuta binti wa kumuoa, jee utachagua lipi na kwanini?

1. Kumuoa binti anayetoka kijijini (hajayajua mengi na hana mambo mengi )

2. Kumuoa binti mliyekutana mjini (ameshayajua mengi na hakuna asichokijua)

Karibuni
Inategemea na mazingira na mtu mwenyewe
 
!
20220301_180716.jpg
 
Ukio kijijini unawaletea wajanja wa mjini kitoweo cha bure.
 
Aliyeona mengi ana uzoefu, hawezi kurubuniwa, huyo wa kijijini atakusumbua akisha yaona hayo mengi. Wanawake wengi wa mikoani wakija mjini wanakua malimbukeni, wanataka ku prove kitu au ku compensate ushamba wao kwa kufanya vitu ili waonekane wa mjini, wanakua wajuaji. Ushamba ni mzigo, unaweza ukamtoa mtu shamba lakini usitoe ushamba kichwani mwake.
 
1. Kumuoa binti anayetoka kijijini (hajayajua mengi na hana mambo mengi )

2. Kumuoa binti mliyekutana mjini (ameshayajua mengi na hakuna asichokijua)
Tabia na mwenendo wa binti husika, haijalishi ni wa kijijini au wa mjini.

Kinachojenga Tabia ya binti ni Malezi toka kwa Wazazi wake, na Jamii inayomzunguka katika makuzi yake

Njia bora ya kupata binti mwenye maadili ni kuangalia
  • Familia yake kwa ujumla ni jinsi gani wanalea watoto.
  • Kwa kijijini Wakina Bibi na Babu huwa wanatusaidia sana kujuafamilia husika, na hupewa angalizo kabisa mapema, kama kuoa basi familia ile inafaa zaidi na sio ile ne ile familia.
  • Maisha na mazingira ya mjini ni changamoto kwa makuzi na kumlea Binti, Hasa Familia (Baba na Mama) wasipokuwa makini.
  • Hivyo ndugu Dismas Mmasi jambo litakalokusaidia kupata binti bora ni; Hakikisha unafanya kila liwezekanolo kuijua vyema na kiundani familia anayotoka binti husika, kabla ya kufanya maamuzi.
  • Tafiti zinaonyesha kuwa maisha na malezi wanayoyapitia watoto wakiwa chini ya miaka 18 (hapa Familia na Jamii inayomzunguka inahusika), ndio huathiri mwenendo na tabia zao pindi wakiwa above 18.
----
Rejea hizi thread
 
Elimu,kazi yake,kabila lake,rangi yake,umbo lake,anapotoka si vitu vya msingi.
Oa au olewa na mtu unayempenda kwa dhati.
Hiyo ndiyo kanuni ya msingi na kuu.
 
Nimekumbuka tu..

"Kumbuka nilikukuta kijijini sitimbi
Umebeba mahindi na furushi la maimbi
Nguvu ziliniishia mithili ya kufa maji
Nafsi nayo ikakidi kwamba mimi nakuhitaji
Kigoli mwenye umbo kama la mdori
Wala sikutaraji ungepiga nami stori
Nilifurahi kuweza kukufahamu
Na nikakuahidi subiri zangu salamu
Kwa kuwa nilikwenda tu kumtembelea bibi
Yote yaliyojiri tu kumweleza ilibidi
Wote walishangaa kusikia namtaka mchumba
Kwani vijana wengi wa mjini tuna kasumba
Wakaweka kikao ndiposa niweze kutoa posa
Niliapa kujiua iwapo ningekukosa
Walinikabidhi nirudi nawe mjini
Na nikakusisitiza mjini kuwa makini"



Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Tatizo sio sehemu unapoenda kuoa tatizo unaishi wapi kama dar au mikoa iliyochangamka atabadilika tu akikutana na mashost wakware.
 
Aliyeona mengi ana uzoefu, hawezi kurubuniwa, huyo wa kijijini atakusumbua akisha yaona hayo mengi. Wanawake wengi wa mikoani wakija mjini wanakua malimbukeni, wanataka ku prove kitu au ku compensate ushamba wao kwa kufanya vitu ili waonekane wa mjini, wanakua wajuaji. Ushamba ni mzigo, unaweza ukamtoa mtu shamba lakini usitoe ushamba kichwani mwake.
Ila inategemea pia nakundi la marafiki atakao kutana nao mjini, rahisi sana mwanamke kubadilishwa na kundi la marafiki ila kama utamtunza inavyostaili nakumwonyesha anatakiwa kutembea vipi kwenye barabara mpya aliyokanyaga hatokuchafulia meza
 
Back
Top Bottom