Mwambie huyo jamaa aanze mazoezi ya kulala
bila nguo,na baada ya siku kadhaa
atajikuta ameishaondoa woga
wa kumtokea mke wake bila nguo.
Faida ya kuoga pamoja ni kila mmoja
anamfahamu mwenzake vilivyo
hata ukipata ajali mwili ukapoteza sura
mtu wa kuitambua maiti yako kwa alama
za ndani ni mke/mme.sasa kama mtu anaogopa
kuoga na mwenziwe uwezekano wa kuzikwa
na city unakuwa mkubwa japo hatuyaombei hayo
Faida ya pili ni mwenzio kukusaidia
kusafisha vizuri sehemu ya mwili
usiyoifikia sawasawa.
kama sababu hizi hazitamtosha
mwulize kwanini alioa
akikupa sababu,mwambie basi msikilize mkeo
maana hukulazimishwa kuoa,na usipomsikiliza huyu ujue
na utakayemleta baadaye naye mtaachana
maana sababu ya kufarakana na huyu si ya msingi.