Wapentekoste Ngara wahamia msituni; wangoja kunyakuliwa

Wapentekoste Ngara wahamia msituni; wangoja kunyakuliwa

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,095
Reaction score
43,307
Katika hali inayokumbushia kisa cha "Wasabato Masalia" kundi la kina mama Wapentekoste na watoto wao wameamia kwenye msitu huko ngara wakiziacha nyumba na familia zao katika kile wanachoamini kuwa wanatekeleza mapenzi ya Mungu ya kutotumia madawa yanayotengenezwa na binadamu huku wakikesha kuomba wakingojea "wanyakuliwe".

 
Last edited by a moderator:
RELIGION IS AN OPIUM OF MIND, By Carl Marx
 
Waache wakeshe.Mbona kuna wanao kesha kwa waganga ili wapate mali na uongozi??????
 
Zion Dauta yaani huoni tatizo watoto kuachishwa masomo, na kuchapwa mboko ili waimbe mapambio kutwa nzima?
 
Zion Dauta yaani huoni tatizo watoto kuachishwa masomo, na kuchapwa mboko ili waimbe mapambio kutwa nzima?
Tatizo hujatufafanulia vizuri hapo juu kuwa wanakataza watoto wasisome.Mie nilidhani wanaenda nao wakati wa likizo.Kama wanakatazwa kusoma,basi wachukuliwe hatua haraka.Mungu ni Mungu wa utaratibu na zaidi sana neno linasema Mshikilie sana Elimu wala usimwache aende zake.......
 
Zion Dauta yaani huoni tatizo watoto kuachishwa masomo, na kuchapwa mboko ili waimbe mapambio kutwa nzima?

MM hayo masomo yako wapi? wakienda shule wanaishia kucheza na kununua vitumbua vya walimu tu. Wamechanganyikiwa wanaona bora Yesu arudi, maisha yamekuwa magumu.
 
Ndio siku za mwisho zenyewe hizi, wanajiandaa kunyakuliwa!
 
Aiseeee. Huyo kiongozi wao inabidi apewe Phd kwa hisani ya watu wa Marekani maana kuwashawishi watu wahamie porini si kitu kidogo.
 
Vijiji vingi ndani ya Tz chini ya serikali ya ccm havina tofauti na maisha ya msiituni. Ni kijiji gani Tz kinaweza kuvuna mazao wakati wa msimu ikiwa Mungu hakuwanyeshea mvua? Hakuna jitihada zozote za serikali kuweka miundo mbinu ya kilimo cha umwagiliaji, na kama zipo basi zitakuwa ni takwimu kwenye makaratasi za miaka nenda rudi. Hivyo wanavijiji hawaoni tofauti ya kuishi kwenye kile kinachoitwa kijiji na msituni.
WAPENTEKOSTE ZIDISHENI MAOMBI YENU, YESU AWACHUE KUPUMZIKA ILA KWA JINSI NINAVYOZIJUA HURUMA ZAKE HATAWACHUKUA NINYI ILA ATAINYAKUA CCM KUWATOA MADARAKANI NA KUWAKABIZI KWA CHAMA KINGINE KITAKACHO SABABISHA UKOMBOZI WENU KIMAISHA.
 
  • Thanks
Reactions: J C
kama kuna mkono wa Mungu hapo, siwezi kupinga, ila kama hakuna mkono wa Mungu, basi hawatafika mbali. Mungu ndiye mhukumu wetu, na ndiye atakayeweka wazi kwa wakati wake kama ni mapenzi yake iwe hivyo au kama ni mawazo tu ya kibinadamu. Bwana Yesu asifiwe!
 
Katika Biblia hakuna mahali pamezuiliwa mtu kwenda Hospitali ila ikiwa mtu ana imani yake ya kupona bila kwenda Hospitali ni sawa kwani hakuna jambo lisilowezekana kwake aaminiye. Pia ikumbukwe kuwa kiwango cha imani hutofautiana kutoka mtu hadi mtu kwahiyo mwenye kuamini kutokwenda hospitali asimlazimishe mwenye imani ndogo kufanya hivyo kwani kama mtu ana mashaka moyoni mwake hata maombi yake ni bure. Kuhusu kuhamia porini na kusubiri kunyakuliwa hapa panaleta utata kidogo kwani Biblia inatuambia hakuna ajuaye siku wala saa atakayokuja BWANA YESU kwa mara ya pili kulichukua kanisa lake. Kwahiyo nashawishika kusema kuwa hii dini inaweza ikawa ni dizaini ya akina Kibwetere in the name of Pentekoste kwani Wapentekoste ni watu wenye ufahamu wa hali ya juu katika masuala ya MUNGU kutokana na uongozi wa ROHO Mtakatifu katika maisha yao
 
Zion Dauta yaani huoni tatizo watoto kuachishwa masomo, na kuchapwa mboko ili waimbe mapambio kutwa nzima?
Sioni tatizo maana nimepigwa mboko sana madrasa ili nikalili kuran badala ya kwenda shule ya msingi na hakuna aliyenitetea.
 
labda wameshauza kadi zao za kupigia kura tayari!!!!
 
Katika hali inayokumbushia kisa cha "Wasabato Masalia" kundi la kina mama Wapentekoste na watoto wao wameamia kwenye msitu huko ngara wakiziacha nyumba na familia zao katika kile wanachoamini kuwa wanatekeleza mapenzi ya Mungu ya kutotumia madawa yanayotengenezwa na binadamu huku wakikesha kuomba wakingojea "wanyakuliwe".



MWANAKIJIJI HII TAARIFA INATUAMBIA NINI KUHUSIANA NA SIAS, UCHUMI, ELIMU NA AFYA YA WATANZANIA ...MIMI NAONA ITS MORE THAN IMANI.....kwanini hawa watu wanaipingaa serikali na hawako tayari kusikiliza cha mtu!!!! kwanini wameamua kuachana na society yao na kuamua kuwa na kanchi kao wenyewe!!!! kwanini wanakijiji wengine hawawaelewi...nini chanzo cha wao kudharau hata elimu ya watoto wao! mmmmmh kuna zaidi ya imani hapa! ni msululu wa mambo mengi umezaa hii imani....kukata tamaaa mpaka na jiografia ya vijiji vyao vya asili
mix with yours
 
Last edited by a moderator:
Katika Biblia hakuna mahali pamezuiliwa mtu kwenda Hospitali ila ikiwa mtu ana imani yake ya kupona bila kwenda Hospitali ni sawa kwani hakuna jambo lisilowezekana kwake aaminiye. Pia ikumbukwe kuwa kiwango cha imani hutofautiana kutoka mtu hadi mtu kwahiyo mwenye kuamini kutokwenda hospitali asimlazimishe mwenye imani ndogo kufanya hivyo kwani kama mtu ana mashaka moyoni mwake hata maombi yake ni bure. Kuhusu kuhamia porini na kusubiri kunyakuliwa hapa panaleta utata kidogo kwani Biblia inatuambia hakuna ajuaye siku wala saa atakayokuja BWANA YESU kwa mara ya pili kulichukua kanisa lake. Kwahiyo nashawishika kusema kuwa hii dini inaweza ikawa ni dizaini ya akina Kibwetere in the name of Pentekoste kwani Wapentekoste ni watu wenye ufahamu wa hali ya juu katika masuala ya MUNGU kutokana na uongozi wa ROHO Mtakatifu katika maisha yao

umeongea vyema sana. nakuunga mkono kabisa. wapentecost ni watu wanaomjua Mungu kwa ukweli kabisa. mimi ninatoka makanisa ya pentecost...yaani makanisa ya kilokole yanayoamini ujazo wa Roho Mtakatifu kuwa ni wa lazima kwake yeye aaminiye. makanisa haya ni mengi sana, na yote yanajumuishwa kuwa ni ya wapentecost.

cha kufahamu ni kwamba, inawezekana, wakati mwingine, kukawa na mtu anayeleta imani fulani ambayo haina uongozi wowote wa Roho Mtakatifu, akaita mlokole na watu wakamdefine kuwa ni mpentecost...akachafua wapentecost wote. cha kuelewa ni kwamba, KITU CHOCHOTE AMBACHO HAKINA UONGOZI WA ROHO MTAKATIFU, HAKIKA YAKE NI UHARIBIFU TU. kwenu nyie mnaomjua Mungu, kama kitu haujaongozwa na Roho Mtakatifu,umeongozwa ether na chuki yako, elimu ya kidunia, ufahamu na hekima za kidunia, doctrine ambayo haikuanzia kwa Roho mtakatifu etc, hakika yake, mwisho wake ni aibu tu na huwa haufanikiwi..kwasababu kila jambo linalofanyika kimwili hilo ni la uharibifu. NDIO MAANA NI MUHIMU KUJAZWA NA KUISHI NA ROHO MT. ili akuongoze, na chochote atakachokuambia Roho, hakika yake hata kama unaona kama utapitia hatari fulani, mwisho wake ni mwema. ndio maana mimi nilisema, inawezekana kuwa, hao watu ni wa Mungu na inawezekana kuwa ni hekima ya kibinadamu tu au mchomeko wa shetani tu anayevaa sura ya malaika wa nuru....HIVYO, KAMA NI JAMBO LA KIMUNGU, LITASIMAMA, KAMA SI LA KIMUNGU, LITAISHIA KAMA WALE WASABATO MASALIA. pamoja na kwamba mimi hapo siungi mkono kabisa.

Shetani baada ya kuona watu wanaokoka na kuzijua nguvu za Mungu, anatumia mawakala wake wengi tu siku hizi ili waingie kama malaika wa nuru, kusudi walete picha chafu kwa watu wanaotaka kumpokea Mungu..ili shetani aendelee kuwa na kundi kubwa la watu wanaoelekea motoni....hivyo kila kitu lazima kipimwe kwa Neno la Mungu, na kwa Roho Mtakatifu.
 
Sioni tatizo maana nimepigwa mboko sana madrasa ili nikalili kuran badala ya kwenda shule ya msingi na hakuna aliyenitetea.

tanzania maendeleo yatachukua muda kupatikana kwa vitu kama hivi. kwa kuwa wamekakosolewa wapentikoste lazima waingizwe waislam nao kwenye mjadala.

sheria ni msumeno tu, kama anaevunja ni mwalmu wa madrasa au mwalimu wa sunday school
 
Sioni tatizo maana nimepigwa mboko sana madrasa ili nikalili kuran badala ya kwenda shule ya msingi na hakuna aliyenitetea.

Kichwa ngumu ndio maana unapigwa mboko uelewe huhitaji mtetezi...na huko kwenye Qur'an uzembe hauhitajiki..dogo..

Hawa walioenda porini walikosa nini mjini? madrasa zote ziko town!

Ama kweli ukristo unakua palipo na wajinga..lakini watu wa mjini (wenye akili) hawawezi kukubali huu ulimbukeni..
 
Back
Top Bottom