Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

Ziroseventytwo

Platinum Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
9,158
Reaction score
17,056
Miaka ya 1980 na 1990 kwenda 2000 kulikuwa na watu wanadaiwa kuwa ni wanyonya damu. Magari ya msalaba mwekundu tulikuwa kukikutana nayo lazima tutoke mbio kwa hofu ya kunyonywa damu.

Binafsi mimi kuna watu pale kijijijni kwetu mkoani kilimanjaro walikuwa wakihusishwa na unyonyaji damu. Mmoja nadiriki kumtaja alikuwa akiitwa Michael Ibrahim wa kijiji cha Longuo. Huyu bwana alikuwa akiogopwa na kila mtu.

Watoto wadogo wakimwona walikuwa lazima wakimbie. Pia baadhi ya wakina mama nao pia walikuwa wakimwogopa. Kuna taarifa za wakati huo kukutwa kwa miili ya watu wakiwa wamekufa na huku miili yao ikiwa imegongwa mihuri kuonyesha kuwa yule marehemu kanyonywa damu. Na wengi wa watu ambao walikuwa akisemwa kuwa ni wanyonya damu walikuwa ni watu wenye kipato. Hivyo kipato chao kuhusishwa na unyonyaji wa damu.

Kilichonifanya nilete huu uzi hapa ni kutaka kujua hii kadhia ni kweli ilikuwepo? Na kama ni kweli hiyo damu walikuwa wanapeleka wapi?

Sababu mimi nachojua ni kwamba damu ni kwa ajili ya tiba yaani kwa ajili ya kumwongezea mtu aliyepungukiwa na damu.

Sasa inakuwaje utoe uhai wa mtu kwa ajili ya kuokoa uhai wa mtu?
 
Hakuna ukweli wowote ni uzushi tu,pia ikazushwa eti kuna wachuna ngozi!

Ikaja ukiwa na kipara unakatwa kichwa! Mara ukiwa na mwanya unakatwa kichwa!

Ikaja ukiwa na alama ya M kiganjani unakatwa mkono!

Hizi ni hadithi za kufikirika tu za utotoni.
 
ni utoto tu uoga na kutopata elimu ya kutosha kwa kile kilichokuwa kinafanyika.pia kufanya kitu bila idhini ya mtu kama kumvuta damu its so frightening.!
ukweli ni kwamba miaka ile kulitokea upungufu wa damu hasabank za damu mahosptalini.so wakaona njia ni kukusanya damu kutoka kwa watu mbalimbali lakini hawakutoa elimu ya kutosha kwa jamii .halafu imagine ghafla unaingia shule unamshika kwa nguvu mtoto wa mtu unamdunga sindano kinguvu unavuta damu ili ukaipime thn uanze kumtoa damu bila idhini yake .si kitu chema.mfanye mtu mzima sio mtoto.
enzi nipo st kayumba walimfos mtoto wa watu wakamvuta damu kumaliza kalegea hajitambui kumbe ana upungufu wa damu.kuanzia siku hiyo tukiwaona nduki!
kuna siku tulikua vipindi shule nzima kusikia king'ora shule nzima tulitimua..nakumbuka nliishia chumbani bila hata hodi kesho nkagoma kwenda shule.
 
ni utoto tu uoga na kutopata elimu ya kutosha kwa kile kilichokuwa kinafanyika.pia kufanya kitu bila idhini ya mtu kama kumvuta damu its so frightening.!
ukweli ni kwamba miaka ile kulitokea upungufu wa damu hasabank za damu mahosptalini.so wakaona njia ni kukusanya damu kutoka kwa watu mbalimbali lakini hawakutoa elimu ya kutosha kwa jamii .halafu imagine ghafla unaingia shule unamshika kwa nguvu mtoto wa mtu unamdunga sindano kinguvu unavuta damu ili ukaipime thn uanze kumtoa damu bila idhini yake .si kitu chema.mfanye mtu mzima sio mtoto.
enzi nipo st kayumba walimfos mtoto wa watu wakamvuta damu kumaliza kalegea hajitambui kumbe ana upungufu wa damu.kuanzia siku hiyo tukiwaona nduki!
kuna siku tulikua vipindi shule nzima kusikia king'ora shule nzima tulitimua..nakumbuka nliishia chumbani bila hata hodi kesho nkagoma kwenda shule.
Nakusalimu aggy
 
Hakuna ukweli wowote ni uzushi tu,pia ikazushwa eti kuna wachuna ngozi!

Ikaja ukiwa na kipara unakatwa kichwa! Mara ukiwa na mwanya unakatwa kichwa!

Ikaja ukiwa na alama ya M kiganjani unakatwa mkono!

Hizi ni hadithi za kufikirika tu za utotoni.
uchunaji ngozi ulikuwepo mkoa wa mbeya.niliwahi ona documentary yake live
 
Miaka ya 1980 na 1990 kwenda 2000 kulikuwa na watu wanadaiwa kuwa ni wanyonya damu. Magari ya msalaba mwekundu tulikuwa kukikutana nayo lazima tutoke mbio kwa hofu ya kunyonywa damu.

Binafsi mimi kuna watu pale kijijijni kwetu mkoani kilimanjaro walikuwa wakihusishwa na unyonyaji damu. Mmoja nadiriki kumtaja alikuwa akiitwa Michael Ibrahim wa kijiji cha Longuo. Huyu bwana alikuwa akiogopwa na kila mtu.

Watoto wadogo wakimwona walikuwa lazima wakimbie. Pia baadhi ya wakina mama nao pia walikuwa wakimwogopa. Kuna taarifa za wakati huo kukutwa kwa miili ya watu wakiwa wamekufa na huku miili yao ikiwa imegongwa mihuri kuonyesha kuwa yule marehemu kanyonywa damu. Na wengi wa watu ambao walikuwa akisemwa kuwa ni wanyonya damu walikuwa ni watu wenye kipato. Hivyo kipato chao kuhusishwa na unyonyaji wa damu.

Kilichonifanya nilete huu uzi hapa ni kutaka kujua hii kadhia ni kweli ilikuwepo? Na kama ni kweli hiyo damu walikuwa wanapeleka wapi?

Sababu mimi nachojua ni kwamba damu ni kwa ajili ya tiba yaani kwa ajili ya kumwongezea mtu aliyepungukiwa na damu.

Sasa inakuwaje utoe uhai wa mtu kwa ajili ya kuokoa uhai wa mtu?
Hii naisi ilikua Kilimanjaro na mm nakumbuka jina la Tarimo yaan nlikua nkisikia ilo jina nataman Ardhi ipasuke!!! Afu nlikua mdogo hata chupa ya soda ya damu sidhani kama ingejaaa .sasa hata sijui nlikua nakimbia nn wakat hao wanyonyaji wasipoteza muda wao kuangaika na nusu chupa ya soda ya damu
 
Miaka ya 1980 na 1990 kwenda 2000 kulikuwa na watu wanadaiwa kuwa ni wanyonya damu. Magari ya msalaba mwekundu tulikuwa kukikutana nayo lazima tutoke mbio kwa hofu ya kunyonywa damu.

Binafsi mimi kuna watu pale kijijijni kwetu mkoani kilimanjaro walikuwa wakihusishwa na unyonyaji damu. Mmoja nadiriki kumtaja alikuwa akiitwa Michael Ibrahim wa kijiji cha Longuo. Huyu bwana alikuwa akiogopwa na kila mtu.

Watoto wadogo wakimwona walikuwa lazima wakimbie. Pia baadhi ya wakina mama nao pia walikuwa wakimwogopa. Kuna taarifa za wakati huo kukutwa kwa miili ya watu wakiwa wamekufa na huku miili yao ikiwa imegongwa mihuri kuonyesha kuwa yule marehemu kanyonywa damu. Na wengi wa watu ambao walikuwa akisemwa kuwa ni wanyonya damu walikuwa ni watu wenye kipato. Hivyo kipato chao kuhusishwa na unyonyaji wa damu.

Kilichonifanya nilete huu uzi hapa ni kutaka kujua hii kadhia ni kweli ilikuwepo? Na kama ni kweli hiyo damu walikuwa wanapeleka wapi?

Sababu mimi nachojua ni kwamba damu ni kwa ajili ya tiba yaani kwa ajili ya kumwongezea mtu aliyepungukiwa na damu.

Sasa inakuwaje utoe uhai wa mtu kwa ajili ya kuokoa uhai wa mtu?
Avatar yako yaukweli
 
Unanikumbusha kilichowakuta wale watafiti waliouawa Dododma kwa kuhisiwa wanyonya damu. Ni upuuzi usio na ushahidi wowote. Nakumbuka nilikuwa mkoa fulani tukawapa lift kina mama watatu, tukawauliza hamkuogopa kunyonywa damu maana kila mgeni anayepita maeneo hayo huhisiwa hivyo. Wakasema sikukadhaa zilizopita walipanda gari la jamaa mmoja anayeaminika kufanya hiyo biashara (bila kumjua kuwa ni yeye). Wakamsema vibaya sana njia nzima. Mwisho wa safari akawauliza mnamfahamu huyo mtu mliyekuwa mnamsema kuwa ananyonya damu? wakasema hawamjui, akawaambia mie ndiye huyo mtu. Wakaaibika sana. Hayo ni mawazo ya watu wajinga yasiyo na kichwa wala miguu.
 
Back
Top Bottom