Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Kuchinja!? Kuchinja mnyama ndio kusababishe nasi tupigane na tuuane? Kweli ndugu zangu watanzania? Siamini kabisa.Kwani kuna tofauti gani ya ladha ya mnyama aliyechinjwa na Mkristu au Muislamu? Kwani nguruwe wanaoliwa na baadhi ya wakristu huchinjwa na nani? Na wanyamapori je?
Ndugu zangu watanzania,umefika wakati wa kusisitiza uhuru wa kuabudu na mipaka yake. Imani yako,pamoja na unavyotakiwa kuvifanya kwa mujibu wa imani yako,usilazimishe kila mtu aifuate. Hata wakati wa Mtume Mohammad(S.A.W.) na hata Yesu Kristu,wapo waliowapinga na kutofautiana nao. Wao hawakulazimisha.Waliendelea kuwajenga waliowaamini na kuwafuata.Basi.
Kilichotokea Buselesele( au Buseresere) Geita hakivutii.Hakipendezi. Yaani watanzania tunaopendana kwa dhati na kuheshimiana tunapigana na kuuana kwa sababu ya kuchinja? Thamani ya wanyama tunaogombania kuwachinja haifanani na thamani yetu kama binaadamu.Thamani yetu ni kubwa mno kwa wanyama.Kubwa sana!
Tuzipende dini/imani zetu na tupendane pia...
Ndugu zangu watanzania,umefika wakati wa kusisitiza uhuru wa kuabudu na mipaka yake. Imani yako,pamoja na unavyotakiwa kuvifanya kwa mujibu wa imani yako,usilazimishe kila mtu aifuate. Hata wakati wa Mtume Mohammad(S.A.W.) na hata Yesu Kristu,wapo waliowapinga na kutofautiana nao. Wao hawakulazimisha.Waliendelea kuwajenga waliowaamini na kuwafuata.Basi.
Kilichotokea Buselesele( au Buseresere) Geita hakivutii.Hakipendezi. Yaani watanzania tunaopendana kwa dhati na kuheshimiana tunapigana na kuuana kwa sababu ya kuchinja? Thamani ya wanyama tunaogombania kuwachinja haifanani na thamani yetu kama binaadamu.Thamani yetu ni kubwa mno kwa wanyama.Kubwa sana!
Tuzipende dini/imani zetu na tupendane pia...