DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Ameir, ametoa wito kwa wahitimu wa elimu ya juu nchini kujikita katika kujiajiri kama njia ya kutimiza malengo yao ya kiuchumi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Ameir ametoa wito huo hii leo wakati wa mahafali ya 19 ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), ambapo amesisitiza kuwa serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuweka mazingira wezeshi kwa vijana wahitimu.
Amesema kuwa wahitimu wanapaswa kutumia kikamilifu maarifa, ujuzi na ubunifu walioupata wakati wa masomo yao ili kujenga fursa za ajira, badala ya kuendelea kusubiri kuajiriwa katika sekta ya umma.
Aidha amebainisha kuwa kupitia sera, mipango na programu mbalimbali, Serikali inalenga kuwawezesha wahitimu kutumia elimu yao katika kuanzisha miradi na biashara endelevu itakayosaidia kupunguza tatizo la ajira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi
nchini.
Ameir ametoa wito huo hii leo wakati wa mahafali ya 19 ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), ambapo amesisitiza kuwa serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuweka mazingira wezeshi kwa vijana wahitimu.
Amesema kuwa wahitimu wanapaswa kutumia kikamilifu maarifa, ujuzi na ubunifu walioupata wakati wa masomo yao ili kujenga fursa za ajira, badala ya kuendelea kusubiri kuajiriwa katika sekta ya umma.
Aidha amebainisha kuwa kupitia sera, mipango na programu mbalimbali, Serikali inalenga kuwawezesha wahitimu kutumia elimu yao katika kuanzisha miradi na biashara endelevu itakayosaidia kupunguza tatizo la ajira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi
nchini.