Wanawake wengine hawajui kusamehe

Siwezi mlaumu huyu dada,mume hilo kosa halikuwa la kwanza...pengine mume alikuwa su mwaminifu kwa masuala ya unyumba sasa mke akaona kurudiana naye anaweza kuambukizwa maradhi bure japo moyoni kamsamehe.ajali ni ajali tu hata angemsamehe na kurudiana nae pengine angepata ajali na kufa vile vile
 
 
 

una hakika atalia? Mjomba angu alikuwa msumbufu sana kwenye ndoa. Mara kalala nje, mara kazaa na mtoto mdogo wa jirani, mara kaenda mkoani eti kutafuta maisha na hela yenyewe hata asitume nyumbani. Yaani ni ugomvi na uasherati. Mama wa watu kalia kachoka. Mjombangu alivyokaa mkoani karibu mwaka mkewe nae akajibanza kwa mbaba mwingine huko kijijini wakapeana na mimba. Mjomba sijui machale yalimcheza akarudi wakapeana unyumba, mara mke katumbo kakaanza kujitokeza. Hakushtukia chochote mpaka pale mke alipojifungua mtoto mkamilifu kabla ya miezi 9. Mjombangu eti akaanza ku-mind. Mamanagu mkubwa akamwambia tena unyamaze kimya umhudumie mwenzio. Mjombangu mkuki kwa nguruwe kwake ukawa mchungu. Siku ya siku kichanga kikiwa na miezi miwili mjombangu akapata mshtuko wa moyo akafa. Kwenye msiba mama zangu yaani dada wa marehemu na ndugu wengine walilia mpaka kuzimia. Chozi la mke halikudondoka ng'o. Siku 4 baada ya msiba kukaja kundi la watu 4 - wanaume wawili watu wazima, na wanawake wawili mmoja mtu mzima na mwingine msichana. Wazee wakajitambulisha wamekuja kutoa pole eti yule mjombangu alikuwa mchumba wa mtoto wao walikuwa wakiishi wote kule mkoani alikokuwa mjombangu. Wazee na binti wa watu hawakujua kama mjombangu ni mwanandoa wa miaka 12! Hapo wenyeji wanaangaliana na kufinyana. Mara akanyanyuka mke wa marehemu na kumrukia binti wa watu na kuanza kumchapa makofi eti yeye ndo alikuwa akimsababishia mateso yeye na wanae. Wageni wakatimka, yule mke akaenda kaburini akasema "yaani we mshenzi huko uliko natamani niongeze kuni uchomwe mpaka ushike adabu yako!". Hiki ni kisa cha kweli.
 
Tatizo letu wengi ni kutopenda kuwajibika. Actions have consequences, na kama ukikosea expect the worst consequences and hope for the best. Kushindwa kumsaheme mtu sio kosa, unless huyo mtu hajakosea. Na kila mtu ana misimamo yake kuhusu makosa na lipi la kusamehe na lipi si la kusamehe.

Me sijui alikosea nini, lakini siwezi kumlaumu mtu kwa kushindwa kusamehe unless I know the details
 
Masikini inatia huruma jamani nimejikuta nimeumia kuhusu watoto yaani sioni atawaambia nini wakikua juu ya kifo cha baba yao, halafu watu namna hii husumbua hata watoto baadae. Huyo mwanamke alijikweza sana yaani mtu anajishusha kuomba msamaha lkn bado u mgumu, ila kuna watu wahivyo wakiamua lao basi hawabadili msimamo. Kweli yapo mambo yanaumiza lkn ikiwa mtu amejishusha ni vema kusamehe. Sijui huyo dada ataishije na hili jambo duh
 
 

Kama wewe ni "Ke" hakika mumeo kapata mke...heri wewe umetambua hilo na Mungu akuzidishe msamaha huepusha mengi sana..katika maisha yetu. Watu wengi ni waumini wazuri lakini hawayaishi yale wanayofundishwa....hongera sana usichoke kusamehe!
Mke wa Rob angekuwa naufahamu japo kiduchu tu kama huo wako leo hii tusinge kuwa na hii post...anyway inatukumbusha kitu hapa wote hapa bado hatuja chelewa.
 

mimi na wewe hatujui kwa nini jamaa alikuwa namplease aruji nyumba huenda si kushare nae sex kama unavyo fikiri huenda ilikuwa ni kwaajili ya watoto wao tu. Ndoa lelemama usione kuta za nyumba zile zinaficha mengi sana...kwani hujui pana ndoa zipo kwa manufaa ya kule tu watoto wa wazazi kitaaambo hawashiriki. isipokuwa tu kuwalea watoto wao ili kesho na kesho kutwa wasije kuwa mtaani au laumu wazazi wao....hata uteteavyo viipi hapa sijui kama huyo mama atabaki salama..kuanzia personal confli ct na kwa watoto wake. Si rahisi kama tufikirivyo...
siku zoote anaeweza kukupa hali halisi ya magereza si askari magereza bali ni mfungwa.
asante
 

Hahahaha hapa mwisho pameniacha hoii
Mara nyingi wanaume ndo chanzo cha matatizo kwenye familia nyingi sana
 
Toa Mfano wa jambo lisilosameheka......maana hakuna kosa lisilosameheka isipokuwa kumkufuru Roho wa Mungu.

well said niongezew kiduchu tu na kumkufuru si kumtukana ila nikumkataa yeye "Roho wa Mungu" hapo ndipo hakuna msamaha...oops na shetani pia hana msamaa kwani kesha hukumiwa tayari.
 
mume:naomba nsamehe mkewangu!! mke:kwa ulichonifanyia kamwe sitokusamehe..! na hapo ndo kamaansha hapo.. POLE YETU WANAMUME
 
RIP...but hako kamgogoro kuna uwezekano wa kutujuza. Maana labda marehemu hayo makosa ni marejeo ya awali, roho inachoka sio wote wanasamehe kirahisi ikiwa roho ishafunga.
 

Mwanzo 4:7 Kama ukitenda vyema hutapata kibali?!... endelea kusoma. umesema vyema huwatunakosea sehemu flani nakujikutankuingia matatani tujifunze kutenda vyema na kuwa mbali na makosa/madhara yatokanayo na kutotenda vyema.
 
Marehemu alimkosea nini mkewe? Nijuavyo wanawake tunasamehe sana...

Hata ivo
Hakuna aijuaye/aliyeiona kesho
R .I.P Rob..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…