Mademoiselle
JF-Expert Member
- Jul 11, 2022
- 722
- 2,914
Napenda sana criticism lakin mkuu, do you think hizi critics ni constructive? Zinajenga? Hata mzazi anafaa kumuadhibu mtoto kitofauti na sio kila siku fimbo.Wanaume wanaupendo wa kweli kwa wanawake na wanajipa jukumu la kuwalinda hata kama hawataishi nao.
Kwani nikuulize mwanamke akiolewa mimi kama mwanaume ninayepigia chapuo aolewe napata faida au hasara gani?
Ila nikuulize wewe ambaye unasapoti mwanamke mwenzako kukaa solemba akiishi tu kama ng'ombe asiye na mchungaji huku umri ukimuenda then akaishia kuzaa bila mume na kutaabika na malezi mwenyewe, kulea watoto wasio na baba, kutangatanga akijitafuta pesa ya malezi bila msaada, wewe hiyo hali inakufaidisha nini?
Kama haikufaidishi nikuulize swali, kuwa wewe furaha yako ni kuona wanawake wenzako wakiteseka hapa ulimwenguni au tukueleweje? [emoji848]
Sasa kila siku wanaoandika humu ukisoma between the lines ni deep resentment na sio kujengana huku. Hata kama baba zetu, kaka zetu mna mapenzi mema na sisi lakin sio dhihaka zinazoporomoshwa humu kila siku. Na by the way kuna mabadiliko?
Behind keyboards kuna mashauri mengi sana ambayo sioni kama yanakuwa presented rather yanakuwa thrown at us. Na zaidi we unaona mabadiliko huko mtaani? Halafu mnaandika sana humu lakin kitaa mambo ni tofauti sana. Tangu mwanzo Mungu alitaka mwanaume awe kiongozi kwa mwanamke so hata huu uharibifu kuna mahali mlilega..ukweli usemwe.
Utakuta mtu hapa anaponda mwanamke, lakin ukifika kwenye uzi wa kimasihara ana visa 10 na wanawake kadha wa kadha. Mtu huyu huyu kwenye PM katongoza wanawake 10. Ukienda kwenye whatsapp yake anatongoza wanawake 10 na hapo ana ndoa. Tena na watoto wa kike juu. Halafu akija humu anawaasa wanawake (as you term it upendo).
Sasa what is this...if we were genuine then ingeanza na huku mitaani tuone mabadiliko. Wanaume mkiwa sawa wanawake watajishebedua na nani..tutatuliza makomwe ovi....it begins with YOU!!!