Kuna kaukweliMambo ya ndoa huwa yana mambo mengi sana lakini bahati mbaya yanapokuja kuharibika huwa tu nasikia Habari za upande mmoja tu huku kila mmoja akivutia upande wake......
Nimekumbuka Habari ya bwana mmoja aliyekuwa na mgogoro na mke wake kila kukicha.....huku yule bwana akimtuhumu mke wake kutoka nje ya ndoa yao na mwanaume mwingine......baadae kuja kugundua ni kuwa yule bwnaa alitumia nguvu ya wazazi tu kumuoa yule bibie na kipato chake lakini si kwa mapenzi ya yule bibie.....Sasa katika hali kama hiyo mwanamke ataachaje kutoka nje ya ndoa....
Jambo lingine ambalo wanaume tunalidharau kwenye ndoa ni sex na romantic words.....haya mambo wanawake huwa wanayapa uzito sana kwani huwa fanya wajione kuwa ni wenye thamani.....
Wanawake sex wanaipa nafasi kubwa sana kwenye mahusiano kinyume chake ni kuwa sisi wanaume mwanamke akishakuwa ndani hili jambo huwa tunalipuuzia sana na kama tunalifanya basi huwa ni chini ya kiwango kabisa......huu ni ukweli ambao wanaume hawawezi kuukiri hadharani lakini iko hivyo kwenye ndoa nyingi sana......
NB;
Migogoro ya ndoa huwa inaanzia mbali sana