Wanawake wana roho mbaya sana

1. Hebu akangalia mwanamke alivyokutunza miezi tisa tumboni huku akiteseka na masickness kibao.
2. Akapata uchungu mkali wakati anakuzaa.
3. Hakulala usingizi akikubembeleza na kukunyonyesha na kuharibu ujana wake kwa ajili yako!
4. Akifua matapishi na mimavi yako kipindi unajinyea
5. Akakusomesha hadi umekuwa na pesa kidogo, hadi umesahau kila kitu na kuanza kumsemea mbaya MAMA yako ambaye ni Mwanamke!

Dada kinachoshangaza kinatokana na magumu anayopitia mwanamke/haya uliyoorodhesha. Lakini inashangaza kuona kuna baadhi ya wanawake japo wanapitia haya yote lakini bado roho zao zina kutu sana.

ninaamini kwa upande wa mawifi ni suala la wivu tu hasa ikiwa kaka anamtunza mkewe kuliko dada zake wanayvotunzwa na waume zao.
 
Hii concept ndio inaharibu hata uwape malezi mazuri watoto wa kulea au hg wao either wanakufight back au kujiiweka wanyonge tayari hata malezi yanakuwa magumu! Mwanamke atakuwa victim tu ndo mwenye kuangalia nyumba nyie wanaume mnakaa nyumbani? Hata wotevmkifanya kazi mwanamke ndo wa kuangalia hapa pakoje nyumbani mle nini! Issue si kutoa pesa tu! Jamani kuweni na heshima kwa mwanamke! It takes a lot kwenye hizo nyumba mpaka muone ziko live watu wanishi ndani! Wakati huo kama una watu ndani ya nyumba kuhakikisha wote wanaparticipate na bado wengine wakishiriki wanaonekana wanaonewa!

Kwa nini kuna hili jina la mama wa kambo kama halijatokana na nyie wanaume wengi kuza either kabla ya ndoa au nje a ndoa? Sasa kuweni na heshima kwa wanawake wanaoyabeba haya! Sasa hivi imekuwa ni majeraha yasiyotibika ukizingatia ndoa nyingi saivi zina watoto wa hivi, hata ulee vizuri vipi kuna watu nje kwa tayari una jina la mama wa kambo wanafuatilia bila malipo mnaishije despite kwamba mumeo pengine anakupa heshima ya kumlelea watoto na watoto pia hauna shida nao but watu kama nyie mko so negative mnawapa hali gani hawa wanawake! Imekuwa kama adhabu kwenye society! Najua wapo wanawake wenye roho mbaya lakini haisaidii kusema hivi mana pia wapo wanaume wa ajabu katika jamii! I hate this name MAMA WA KAMBO sasaivi i think its high time labda lisitumike katika jamii!
 
Kwa ulinganisho huu wanaume ndo wana roho mbaya zaidi ya wanawake!
1 ni rahisi kusema hgeli anaonewa kwa sababu anagombezwa kwa kutofanya wajibu aliopangiwa. Hata wewe kazini kwako unagombezwa kwa email ama kwa simu (wanajeshi wanarushwa vichura na boss wao, sio?). Siku utaachiwa jukumu la kusimamia hgeli na watoto utapata wazimu. Ningekuwa mkeo ningesaka sababu ya kuondoka home 3 months only nikusikie!
2 hivi kuna mwanaume anaishi na mtoto wa kambo? Ni wachache sana na huwa wanakuwa na mambo yao mengi tu! Sema wanawake tunajua ku-appreciate na kusema walau kaniruhusu mwanangu ajibanze hapa niishi nikimuona. I bet wanawake wenye watoto wao huwa wanakuwa na kafungu ka ziada kuweza kuleta ulinganifu.
3 wanaume wangapi wanaishi na wakwe zao? Hivi baba wa mkeo akihamia kuishi na wewe hapo ndani, na ajitie faza house utabaki unachekelea? Ukisema una hamu na ugali anamuambia mwanae hakuna kupika ugali usiku, anaanza kukupangia na muda wa kurudi nyumbani kwako na kukataza kuvaa jeans anataka uvae sarawili za kijani kuenzi ccm?
Ili ujitambue una roho mbaya kiasi gani, mara ya mwisho lini umetoa hela ukamtumia baba mkwe wako? Amesomesha mwanae hukuwepo, mwanae ana kazi ya kuchangia kukutunza na wanao na kujenga nyumba yenye jina lako, na unatamba staki ngebe nyumbani kwangu, utasema mkeo ni mgeni! Unamtumiaga mkweo hela bila kuombwa?
4 Ungekuwa na vishemeji vinakaa kwako na vinataka kukusaidia kuendesha mji wako ungekuwa na roho nzuri sana na kuwaachia jahazi?
Dawa ya kukaa vizuri na watu ni kuweka pua yako inapostahili. Sikatai wapo wagomvi na wachokozi. Mie nimekua na kaka wa kambo lakini sikuwahi kujua ana mama yake hadi nikiwa std 5, na ni kwa sababu mama yake alikuja kumtembelea. Yeye mwenyewe alijua ana mama yake wakati. Kamaliza form 4! Wanawake hawana roho mbaya, wana VISASI vibaya.
Wanawake wana roho mbaya sana na sijui ni kwanini. Ukitaka ku prove fuatilia haya hapa.

1. Wanavyoishi na ma house girl
2. Wanavyoishi na watoto wa kambo
3. Wanavyoishi na wakwe zao
4. Wanavyoishi na mawifi.

Na pia angalia mwanamke akawa Blandina Nyoni fulani hivi usipime huo moto wake kwa wanawake wenzake.
 
Tena kama nyie mlioenda enda shule ndo mna roho mbaya sana. Mnajifanya hamu entertain mambo ya extended family. Hivi unafikiri ulivyonikuta mimi nina kagari na kaofisi unadhani nilidondoka toka mbinguni? leo hutaki kaka zangu wala nani

Mkuu hapo umenena, wanawake hawa wasomi hawaelewi kabisa.
 
Pale ambapo sielewi sawasawa ni mwanamke kumchukia mama mkwe wake au wifi yake. Hawa wote ni wanawake, inakuaje hapo?
 
Ukimzaa mwanao ndo umchukie na kumfanyizia mtoto wa kambo? Usitake kuleta hapa guilty concious eti mama alikuzaa. Ukweli bado unabaki. Roho mmmbayyyyya!
kamwe tena narudia kukuonya kamwe usimlinganishe MWANAMKE NA MWANAUME
 
Mwanamke asiye katili ni yule mwenye undugu wa damu na wewe tu. Mliemuoa, mchumba au unaemgonga sio ndugu kaka! hapo lala jicho moja wazi kila siku....wengi wao vichaa tuu!
 
Ukimzaa mwanao ndo umchukie na kumfanyizia mtoto wa kambo?
Usitake kuleta hapa guilty concious eti mama alikuzaa.
Ukweli bado unabaki.
Roho mmmbayyyyya!

Oaneni wenyewe kwa wenyewe basi!
 
Wakati libac lako limempa mama yako mimba likamkana mama yako akafukuzwa nyumbani akawa anatangatanga mtaani kutafuta chakula wakati wewe ukiwa tumboni, siku ikafika akakuzaa kwa uchungu, akawa anakubeba mgongoni na karai la ndizi kichwani, anazunguka mtaa hadi mtaa kuuza ndizi ili apate hela ya kukununulia chakula, wakati huo baba yako anakula raha na vimwana, leo unaongea ongea tu.
 
Mie nadhani ndaku una matatizo ya akili....kati ya hao wanawake wenye roho mbaya basi na mama yako nae yupo....pole sana ndugu..
 
Hujamalizia sentensi yako. Wanawake hawana roho mbaya bali Wanawake wana roho mbaya sana kwa wanawake wenzao.
 
Hana hoja, atashindanaje?
Wanawake wanakuwa subjected to impossible situations hatafu wanalazimishiwa kukubaliana nazo! Hivi kuna mwanaume mkewe anaweza akazaa na houseboy halafu mumewe akamsamehe na wakaendelea kulea huyo mtoto? Na huyo baba akitoka kazini anamletea mtoto wa hboy toys na kucheza nae? Sikubaliani na kutesa mtoto lakini pia sikubaliani na kumlazimisha mtu kufanya mambo asiyoyataka.
Acha gadhabu mkuu! Uzi huu umeleta mwenyewe, wale wanaokwenda kinyume
na wewe mawazo yao yafanyie kazi. Shindana kwa hoja.
 
Yah, its true...wanawake wote ni wakatili wa kutisha, hakuna mwanamke mwenye huruma wote huwa wana-pretend tu, hasira zao wanazimaliza kwa tukio baya sana...
 
Back
Top Bottom