Wanawake wakibeba mimba wanatukomoa

Wanawake wakibeba mimba wanatukomoa

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,932
Reaction score
11,849
Sijui wanawake wote wakibeba mimba wanakuwa hivi au ni huyu wa kwangu tangia abebe mimba ndani hakukaliki mara nina hamu na kitu fulani ukileta hali, amehama chumbani eti kinatoa halafu mbaya analala kwa housegirl.

Nimejitahidi kufanya usafi lakini wapi hataki hata kuingia humo nimebaki nalala mwenyewe kwa kweli kuna maudhi mengi mpaka nachoka hivi ni kweli hizo mimba zinawafanya hivyo.

Nimejaribu kuongea na marafiki ambao wenzi wao walibeba mimba walichonieleza anayoyafanya huyu wangu ni cha mtoto hivi kweli kwamba mimba huwafanya hivyo au mnatufanyia makusudi.
 
Si nafuu wewe mkuu,sitasahau mke wa dingi mdogo alikuwa na mimba yake ya kwanza mwaka 2000,basi mpaka dingi mdg kuna kipindi haendi job na alikuwa anamdekeza haswa...siku moja usiku wa saa 7 akatuamsha tena kwa hasira mimi na binamu yangu eti tukamtungulie mkewe mapera mabichi (japo mti haukuwa mbali) halafu tuje na matembele pia. Na kulikuwa na manyunyu usiku huo huyu binamu yangu alianguka kwny utelezi na kuumia hadi leo ana kovu,asubuhi yake alienda kwao (kwa Aunt yangu).
 
hizo ni mbwembwe tu mimi wangu anamimba na nimemwambia staki drama hapa tunalea taraatibu na katuliA



Omba mungu isimzingue la sivyo warning yako itakuwa yako yeye haimuhusu as long as unaenda kumnunulia miwa saa 8 usiku, au chips saa 10 alfajiri na sio za kupika home nooo, za mitaani. Mabadiliko ya hormones si mchezo.
 
Mkuu naona unachokipitia kidogo! Hapa naandika nipo sofani nimeshahama chumbani miezi mitatu iliyopita! Yaani mimba imebadilisha kila kitu! She love me real so much Lkn kichefuchefu hatari! Baadhi ya vyakula haviliwi humu kwangu! Hatari sana! Hapa nasubilia tu huyo mtoto kuzaliwa maana kila kitu kimebadilika!
 
Si nafuu wewe mkuu,sitasahau mke wa dingi mdogo alikuwa na mimba yake ya kwanza mwaka 2000,basi mpaka dingi mdg kuna kipindi haendi job na alikuwa anamdekeza haswa...siku moja usiku wa saa 7 akatuamsha tena kwa hasira mimi na binamu yangu eti tukamtungulie mkewe mapera mabichi (japo mti haukuwa mbali) halafu tuje na matembele pia. Na kulikuwa na manyunyu usiku huo huyu binamu yangu alianguka kwny utelezi na kuumia hadi leo ana kovu,asubuhi yake alienda kwao (kwa Aunt yangu).

hahaha dah....
 
I can feel what they're going through. Wangu hakuwa na mapozi sana lakini mtoto alipofia huko ndani, then yeye akapata massive complications, acha kabisa...hawa watu tuwaheshimu tu, huwa wanapitia kipindi kigumu wakati wa ujauzito.
 
Wakuu. Mke wangu katika hali hii kazidisha kunipenda sana,nikitoka tu nyumbani natafutwa. Ila yeye hapendi nyama,wali...anapenda sana ndizi rost,chips. Ila vituko vya ghafla haviishi kwake,mf anaweza kumzingua mtu kwa hasira...ila wakati wa ujauzito kwa ndoa hizi ni kumwomba Mungu tu sijui afupishe kipindi ata kiwe miezi mitatu...maaana.
 
Molembe

Pole yetu mkuu! Am going through the same situation hawa viumbe mwisho...! Sina hamu tena na hiyo mimba aisei...!
 
Last edited by a moderator:
Molembe,this is just a biggining, mengi zaidi yanakuja, lakin don't worry, baada ya Mitzi 3 ya mwanzo yataisha.
Molembe
 
Last edited by a moderator:
Molembe

Hongera muraa,baada ya miezi mitatu itaisha.
 
Last edited by a moderator:
Si nafuu wewe mkuu,sitasahau mke wa dingi mdogo alikuwa na mimba yake ya kwanza mwaka 2000,basi mpaka dingi mdg kuna kipindi haendi job na alikuwa anamdekeza haswa...siku moja usiku wa saa 7 akatuamsha tena kwa hasira mimi na binamu yangu eti tukamtungulie mkewe mapera mabichi (japo mti haukuwa mbali) halafu tuje na matembele pia. Na kulikuwa na manyunyu usiku huo huyu binamu yangu alianguka kwny utelezi na kuumia hadi leo ana kovu,asubuhi yake alienda kwao (kwa Aunt yangu).

Hahahahaa...poleni mie nakumbuka ujauzito wa wife alikuwa anapenda pespi baridi ile chupa yake inamdomo mwembamba....siku moja ziliisha kwa friji imefika saa tisa usiku akaniamsha mzee tulizunguka baa zote dar nikaja ipatia kona bar sinza toka mbezi kimara....tumerudi om tayari kumekucha...
 
Hahahahaa...poleni mie nakumbuka ujauzito wa wife alikuwa anapenda pespi baridi ile chupa yake inamdomo mwembamba....siku moja ziliisha kwa friji imefika saa tisa usiku akaniamsha mzee tulizunguka baa zote dar nikaja ipatia kona bar sinza toka mbezi kimara....tumerudi om tayari kumekucha...

Miye nishazungushwa mji mzima wa Makambako usiku wa Manane kutafuta kitimoto. Ni balaa ndani kulikuwa hakukaliki. Halafu kituko chake unakuwa mpole kama kondoo. But now its about 6yrs tunapendana na mtoto wetu pia.
 
ndio gharama za ubaba hizo vumilia..... utakapokuwaunacheza na mwanao utayasahau yote hayo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom