Wanawake wa kisasa na tatizo la "Double standard"

Wanawake wa kisasa na tatizo la "Double standard"

Shida ya wanawake wengi ni kuwa akishapata Nguvu za kiuchumi tu tayari anadhani yeye na wewe mnalingana katika kuongoza familia, anasahau kuwa mwanaume ni mwanaume tu na ndiyo kichwa cha familia (kwa mujibu wa maandiko matakatifu) hivyo huyo mkeo alianza kuzuzuka baada ya kupata Kazi huko TRA na kuanza kulamba mpunga.Shame on her! NB: Mchango wangu huu nimeutoa nikiamini kuwa ulichoandika ni ukweli vinginevyo ningepaswa kwanza kumsikia na mkeo anasema nini kuhusu hiyo issue.

Ni namna ya kumuonyesha kuwa sijaridhishwa na mwenendo wake.......na ni njia ya kistaarabu ya kumuelekeza mwanamke .......ningemtoa yeye isingekuwa ustaarabu hata kama kanikosea......

Ulitumia hekima sana
 
Hapana si kweli.......ndumi la kuwili ni traitor...........mtu ambaye anashika jambo moja huku anataka kufanya jingine........kama unataka kuhakiki naomba ugoogle hilo neno utapata tafsiri yake mtandaoni.........double standard kama linavyojielezea lina maanisha kuzidisha kiwango......au kupitiliza.......mifano ipo mingi kuelezea double standards......
ni kweli ndumilakuwili ni traitor ila nawe una kaubishi bro! ukiwaambia watoto wako nyumbani ni marufuku kula sukari na atakayekula atachapwa viboko vitatu halafu mtoto wa kwanza akala ukamchapa, wa pili akala ukamkanya kwa maneno hapo utakuwa umekuwa na double standards. Yaani kanuni hiyo hiyo moja unai-judge tofauti. Sasa mbona kama unaonyesha kuwa mkeo tu ndo anahitaji kupelekwa "unyago" kufundishwa mambo ya ndoa? We nae unahitaji shule usijione umesimama.
 
Yes brother .......ndiye yule yule.......ndio nakomaa naye hapa .......ndoa ni ngumu ndugu yangu ..........bado ananiletea majaribu ingawa sasa hivi ni mizaha mizaha tu......tofauti na kipindi kile........yule jamaa alinijia na polisi.........kunishtaki kwa uharibifu wa mali......polisi m'moja aliyekuja naye ni mwanangu hivyo nikaitwa tu kituoni bila kukamatwa kwa shurti......tulipofika kituoni nikaambiwa niandike maelezo......nikasema sawa nitaandika kwa sharti moja......mke wa yule mzee aitwe awe shahidi katika hiyo kesi......mbona mzee aliingia mitini maana alijua hiki kisanga kikimfikia mkewe ni inshu so kesi ikapotea kisela hivi hivi.

now i see. you have a serious psychological problem. uko kwenye toxic relationship na addict ni wewe. Mwisho wa siku utakuja kuuwa au kujiuwa. Una low self esteem na unconsciously au consciously unajaribu kuifukia kwa kutumia njia za mabavu ili ku-maintain nafasi yako ambayo ndani unahisi imepwaya. Unavyoonekana mbishi natamani kukuuliza utoto wako ulikuwaje ila naogopa. Kama umeamua kwenda kwa dr. chris mauki jipeleke mwenyewe binafsi kwanza ndo uende na mwenzi wako.

ningekuwa kwenye nafasi ya chris ningekwambia utoke kwenye huo uhusiano sijui ndoa. mambo gani hayo mpaka ushapigana na mwanaume mwenzio kisa mwanamke? kwani huyo mwanamke ni mdoli hana utashi? bado uhangaike ku-hack mawasiliano yake, mara ulilie message za mchana akiwa kazini.......mpaka anakwambia humsisimui mpaka labda usafiri...we bado upo tu unahangaika kumrekebisha. Huko ni kuwa gerezani.

Fikiria kutafuta uhuru. unatakiwa ukiwa na mwenzi uwe na amani ya moyo. akichelewa uhisi kapatwa na dharura au kitu kibaya na si kuwa anazini. sasa wewe dah!
 
ur genius bro ume solve ipasavyo.....wanawake ni hamnazo tatizo wametuzaa tu .tungekua tunatoka kwenye MITI au MATRANSFOMER mbona wangeelewa KAZI

Mbona mnatutusi hivyo jamani? Eti hamnazo!!!!
Hivi hujasoma ukaelewa kwamba huyo dada aliomba msamaha usiku huohuo? Hujaona kwamba na asubuhi aliamka akaendelea kuomba msamaha! Hiyo yote ni kwa sababu anajitambua na alijutia kosa lake, angekuwa hamnazo angezidi kutilia kiburi ebo!!!

Alafu wanaume bhana, sometimes mnafurahisha na kukera juu!
Hiko kijikosa cha kuflirt ndo kimewafanya wengine mvimbe macho na kutuita hamnazo ilihali nyie michepuko mmeitandaza kila kona.
Mnashangaza!!!
 
Nimependa usimuliaji wako mkuu, we ni mwandishi mzuri aisee

Pia nimependa ulivyodili na hilo kadhia, that was mature enough

Mungu alivyosema tuishi na hawa viumbe kama tunavyoishi na mtoto mdogo hakukosea, alivyosema tuwe vichwa vyao I mean tuwaongoze hakukosea vile vile. Ni wepesi sana wa kujisahau na kutoka nje ya mstari, so ni jukumu letu kumrudisha kwenye mstari kama ulivyofanya, BIG UP!!!
 
2007 hadi leo bado analeta makuzi hayo?....mpige mimba fasta,hizo stori za mtoto acheze kwenye sebule yao tupa kule!...2-3 yrs to come kwa pigo hizo utakosa mwana na maji ya moto!...ila mwanaume hakimbii nyumba arif!..ukisusa wenzio wala!
Mengine ya Dr Chriss,mi nimekushauri ki-NIGGA!
 
Hapana bado hatujatafuta mtoto tunavuta muda kidogo tuwe na kwetu kabisa two to three years from now.........mtoto acheze kwenye sebule yao sio ya kwa watu.........ndio inakwenda mwaka wa tatu now.......but we r together tokea 2007........
nakushauri usiendelee kupoteza mda mpe mimba ndugu kabla haiajwa too late
 
Jeuri hii ni ya chekechekea best........huyu anajua kwa jinsi nilivyotoka naye mbali akileta za kuleta atajitia mikosi maana nimem'badilisha kwa mengi na kuvumilia utoto mwingi ..........sasa anajua yupo na mtu mzima......
Ngoja nikupe siri......unaona ni kwanini huwa tunawapenda mama zetu ni kwasababu ni wanawake ambao walijitoa kwetu.......sasa hata wewe utakapojitoa kwa mtu na kumvumilia kwa yote......siku unapokuwa mbali na yeye atahisi sehemu ya maisha yake inatoka..........ndicho nilichomuonyesha.......

Mkuu hongera sana big up
 
Mkuu pole sana, bora wewe umeoa...maana mimi imenitokea hali kama yako kidogo yangu tofauti maana mimi nilikuwa na gf ambae nilimvumilia mpaka kamaliza chuo baada ya kufanya kazi 7 month ikabidi niache kazi baada ya kupata scholarshp kupiga masters ya Engineering hapa hapa Bongo.

Ikabidi nimpush dogo akapige masters au akapractise law hahahahaha... akapata sehemu kupractise hizo mambo yao wakawa wanampa posho kama laki 3 si akaanza kuleta dharau

Nikajitahid kumuweka sawa nikashindwa ikabid nimwambie bora uende maana usije kunitoa kwenye reli nikashindwa kumaliza ata hii masters kwa stress ambazo hazina msingi...sometimes hawa dada zetu sijui wanakuwaje
 
Binafsi nimeisoma thread yako mkuu nimeumia sana coz mambo kama haya yanatutesa sana sisi vijana tunaoanza ndoa hasa tukiwa na umri wa kati, hii inatokana na uwezo mdogo wa kuchukua maamuzi sahihi na kwa wakti gani? pindi tatizo linapotokea.

Hili si ttzo dogo kama unavyofikilia sbb litaendelea kukusumbua mda mrefu tu usipokuwa makini anachokifanya huyu sasa usitegemee kama ataacha ghafla au kubadilika ndani ya mda mfupi, ule usemi wa kila mtu atabeba msalaba wake nadhani aanza kuufanyia kazi, inawezekana kabs amebadilika kutokana na mazingira baada ya kupata kazi au wewe mwenyewe umeteleza mahali fulani ktk kufanya maamuzi sahihi.

Nahisi tabia hii imeanza kuota mizizi na si kwamba imeanza leo kama usemavyo bali alikuwa nayo tangu awali ila hukuijua coz hakuwa huru sana kwako kabla ya kupata kazi, ngoja nikwambie kitu kaka inawezekana kosa lako kubwa umeruhusu kwa kiasi kikubwa ayajue mapungufu yako mengi kwa mda mfupi pili ndugu yangu umekosa msimamo haiwekani ghafra tu abadilike kuna mahli kuna weakness upande wako

Ninachokijua mwanamke ni kama mtoto anahitaji maelekezo sahihi ikitokea ukajisahau tu anakudharau sana , jambo lako lolote hasa unaloamini litajenga ndoa haijalishi atalipokea vp mweleze tu akuelewe mlie tyming akiwa amesettle mweleze kinaga ubaga ataelewa tu.

Kamwe usikubali akuyumbishe akutoe kwenye reli hata kama umempenda vp mheshimu mpende lkn uwe na limit,ukijisahau tena ukmheshimu kupita maelezo ukamnyenyekea sana na kulia lia na vsms kama unavyoendelea kufanya AISEE!atakusumbua sana zaidi ya sasa mimi nahisi ttzo siyo kazi aliyopata ukweli ni kwamba umekosa msimamo na maamuzi kama mwanaume, huko kwenye simu na sms zake unahangaika bure kaka, mwanamke hachungwi kama mbuzi au kondoo utapasuka kichwa.

Kama ningekuwa mm ndio ww (inagawa haiwezekani) ningefanya hivi, kwanza simu yake nisingekuwa na mda nayo kbs pili huyu ni mkeo siyo fiancee au girl friend ungejitahidi ucheze na sku zake umtandike kitambi bila yeye kutegemea tatu kama mlikuwa na msaidizi yaani housegirl mpumzishe kwa mda ili huyu aanze kujua wajibu wake kama mkeo, mambo mengine mfanyie maksudi tu ili akuheshimu(ingawa inaweza kuonekana kama utumwa lkn lengo ni kujenga) mfano anaweza tenga chakula harafu mwambie kimaksudi akunawishe mikono akupakulie akimaliza asali harafu ww kimya. ukimaliza kula hivyo hivyo atanyooka tu kama ulikuwa na mpango wa kuwa na watoto zaidi ya mmoja hakikisha hawapishani sana miaka other wise utarudi humu jamvini kuja kulalamika tena kuwa kaja na mpya nyingine!

Ni hayo tu mkuu!
 
ur genius bro ume solve ipasavyo.....wanawake ni hamnazo tatizo wametuzaa tu .tungekua tunatoka kwenye MITI au MATRANSFOMER mbona wangeelewa KAZI

Kula like mkuu... yaani hawa watu bana hawatabiriki ni wepesi kusahau hata ukisimamia kucha bado tu.. hizi ndoa zinaficha mambo sana.
 
Mkuu pole sana, bora wewe umeoa...maana mimi imenitokea hali kama yako kidogo yangu tofauti maana mimi nilikuwa na gf ambae nilimvumilia mpaka kamaliza chuo baada ya kufanya kazi 7 month ikabidi niache kazi baada ya kupata scholarshp kupiga masters ya Engineering hapa hapa Bongo.

Ikabidi nimpush dogo akapige masters au akapractise law hahahahaha... akapata sehemu kupractise hizo mambo yao wakawa wanampa posho kama laki 3 si akaanza kuleta dharau

Nikajitahid kumuweka sawa nikashindwa ikabid nimwambie bora uende maana usije kunitoa kwenye reli nikashindwa kumaliza ata hii masters kwa stress ambazo hazina msingi...sometimes hawa dada zetu sijui wanakuwaje

Daaaah.. yuko wapi huyo? Hemu nipatie hata phone no. Tafadhari maana wanawake kama hao kuna aina flani ya wanaume ambayo ndio kiboko yao
 
Back
Top Bottom