Wanawake: Ukimpenda mwanaume mtongoze

Wanawake: Ukimpenda mwanaume mtongoze

Hao wanawake unaowaongelea mkuu wa mwaka gani...au hawa hawa wa awamu hii ya tano....ha ha ha wanawake siku hizi tumevurugwa tukipenda tunafungukaa....hatuna shida labda useme wa miaka ya 80 huko lakini si sasa au hao unaowaongelea wa kutoka huko kyambamkumbe sio dar es salaam hii.
 
Mkubwa mi naona iyo ni kama natural imeshajitengeneza kuw mwanaume ndo wa kutongoza na mwanamke ni wa kutongozwa kwaiyo mi naona tuwavumilie tu kwa ilo
 
Hahahaa umetisha sana
Ukimpenda mwanaume mtongoze...hakiyanani mimi Mwanamke akinitongoze kila siku Asubuhi lazima nimpe angalau kilo na nitamuheshimu sana sana Aiseee coz nitamuona jasiri sana sana hata
 
Ukimpenda mwanaume mtongoze...hakiyanani mimi Mwanamke akinitongoze kila siku Asubuhi lazima nimpe angalau kilo na nitamuheshimu sana sana Aiseee coz nitamuona jasiri sana sana hata
Kilo? Unatafuta mafuriko pm eeh?
 
Hilo la pesa sio sana ila mara nyingi huwa ni neno la kujifariji kutokana na kushindwa kueleza hisia zetu.
Mkishindwa kabisa basi andikenj hata barua, au tumeni washenga hamuoni India wenzenu wanatoa hadi mahari kabisa
 
Kwa upandea wangu mwanamke akinifata na kunitongoza kabla hata sijamfata mm au kuonesha ishara ya kumuhitaji Automatically anakosa mvuto kwangu na ikatokea nikakubali hatuta dumu sana,

raha ya mpenzi umfate kiume umtongoze akusumbue sumbue kidogo akupe tumbo joto....siku akikubali huwezi mchukulia simple na utamjali sana, binafsi ndo nilivyo.

hata nilie nae kunisumbua kumpata ndo kumenifanya nizidi kumthamini kila siku.

"Real Men knows what/whom they want and how to get them"
Niuzamani huo
 
Mie mke wangu alikuwa na haibu sana kwangu....yaani ni mwanamke mzuri na alikuwa mcheshi sana kwa wengine ila kila aliponiona sehemu ghafla alikuwa anaishiwa nguvu na kubaki kunitizama tu hata kunisalimu alikuwa anashindwa. Siku ya siku tukakutana hana kwa hana, nikamshika mkono na kumsalimu akabaki anatetemeka na kuangalia chini. Nikamwambia najuwa unanipenda nami nakupenda, ghafla akageuka na kunikumbatia. Toka siku ile mpaka leo ni miaka 13, tuko na watoto 3 na tabasamu alituishi kila tukikumbuka.

dah.!!.
mkuu mpaka nimekuonea wivu yani...
 
Kwa kuongezea tu, niliwahi kumuuliza mke wangu kwa nini alikuwa hapendi kunisalimu wakati nilikuwa ninamuheshimu na kumsalimu kama wanawake wengine, akanishangaza kwa kusema eti alikuwa anaogopa nitamchunia na kama angenitongoza mimi ningemuona yeye kuwa malaya na alishazoea mchezo wa kutongoza wanaume. Akanishangaza zaidi kwa kuniambia kuwa aliwakataa wanaume wawili kwani alihisi iko siku nitamuoa au kutoka naye na alishamuomba Mungu niende kumtongoza, kwa kweli niliumia sana alivyoniambia hivi. Samahani ila ilinibidi nilie kidogo lakini si mbele yake, nililenda chooni. Nilimuhurumia sana mke wangu kwa kuwa jasiri wa kukaa na maumivu ya kunipenda wakati mwenzake sikuwa na hili wala lile juu yake, wanawake jamani msijiumize mioyo, jitokezeni kutongoza wanaume. Kuna wanaume wengine hawajuwi kutongoza kwani kutongoza si kila mtu anajuwa.

ebwana jamaa hyo 'Movie' yako na mkeo jinsi mlivyoakutana na kujuana mpaka mlipofikia nimeipenda mno.
mnastahili pongezi.
Mungu azid ijaalia familia yenu furaha na amani
 
Back
Top Bottom