Hivi kwanini mwanamke akimpenda mwanaume anapata shida sana ataanzaje kumwambia, mwanamke kikawaida akimpenda mwanaume anamuonesha 'signals' ishara ila ukiiona mwanaume haelekei kuja kukutongoza mfuate, anza kutongoza!
Na nyie wanawake pia mmeumba na hisia tena kali kuliko za mwanaume, ukimpenda mwanaume na kumuonesha ishara na kuona haelekei mfuate mtongoze!
Mimi hadi kuandika hii post kwa hili group ni mtoto wa kiume ambaye tangu utotoni hadi sasa hivi kote niliko pita nimekutana na wanawake wengi waliotokea kunipenda, baadhi walijitoa muhanga kuja kunitongoza kama 20% ila 80% walio baki waliishia kunionesha signal na kushindwa kunifuata.
Alafu wanawake mnanichekeshaga sana mkitokea kumpenda mwanaume na kushindwa kumwambia moja kwa moja utasikia, Bariki una macho mazuri, sijui una kifua, utasikia umependeza hata kama umevaa magunia, utasikia una akili hata kama ulipata division 0, yani atakupa sifa za kila aina na nyingine unakuwa hata hauna ila anakusifia tu ili apate attention yako kwake na ni sub conscious mind, anaweza fanya hivyo bila kugundua kama anafanya.
Wanawake mnanichekeshaga sana aisee Dah! Kwa ushauri wangu kwenu wanawake, ukimpenda mwanaume go straight mtongoze mwambie nakupenda, usianze kuzunguka zunguka na nyie pia mliumbwa na emotion tena kali kushinda hata zetu wanaume.