Wanawake na magari

Kasie

Platinum Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
22,801
Reaction score
43,177
Habari zenu wapendwa.
Nikiwa njiani leo kuelekea kazini kuna mama mmoja tyroad hand ikaachia tairi ya mbele kulia ikakaa migulu baja.

Nikiwa kwenye foleni mama akawasha hazard na kuchukua kilongalonga probably alikuwa anampigia husband au fundi.

Mbele kidogo nikiwa kwenye hizi barabara za vumbi maana tunapita huko kukwepa foleni njia kuu. Ikapita gari mama mwingine tairi ya mbele kushotoina pancha mama hana habari anakanyaga wese tuu.

Nikajikuta nawaza wanawake wanapenda magari na kuendesha kwa mbwembwe.

Issue inakuja gari ikiharibika inakabidhiwa mwanaume. Ni kudeka au ndo kawaida maana mie gari pancha nabadili mwenyewe, na vitu vidogovidogo.

Au kwakuwa mie sina husband nimejiseti tatizo likitokea ni langu.
 
Ni kudeka au ndo kawaida maana mie gari pancha nabadili mwenyewe, na vitu vidogovidogo. Au kwakuwa mie sina husbandi nimejiseti tatizo likitokea ni langu.

1. Kwanza, hongera kwa kuwa tumejua unamiliki gari...

2. Pili, si kila jambo ulijualo wewe wengine wanafahamu na ndio maana hata vidole vya kiganjani havifanani...

3. Tatu, hivi siku hizi hufanyi tena mazoezi ya kukimbia hadi morocco?
 
Umenikumbusha sister angu mmoja alisha wahi kunokisha engine ya gari hata haina week... kisa kajifanya siku hiyo kufungua boneti kaweka maji kasahau kufungu mfuniko... kakanyaga mafuta na safar zake mpaka gari likazimika
 
wengi wanajua kudrive tu tena hizo zenye automatic gear system akikanyaga mafuta hadi anafika. Hawana ujanja ikizngua wanajua wanaume watahusika hapo
 
Mkuu Kasinde
Hata wazazi nyumbani wanawagawanya watoto kwa vizawadi kutokana na jinsia. Mimi nina pacha wangu yeye ni KE, tulivyokua wadogo baba akileta zawadi basi mimi naletewa toy ya kigari na yeye analetewa kimdoli.

Hii inaonyesha dhahiri wadada na magari hasa kutengeneza sio mambo yao, wachache wanafanya.
 
Last edited by a moderator:
1. tie rod end/ball joint etc ikikatika sio mwanamke tu hata mwanaume huna ujanja,utapaki pembeni utaita wenye kazi yao....fundi labda wewe mwenyewe uwe fundi magari.

2.pancha inahitaji uzoefu,kuna wanaume wanapata pancha nao hawajui mpaka unamshtua kwahio unahitaji kauzoefu fulani kuhisi mabadiliko kwenye gari yako na si kila mtu ana uwezo huo.

kuna wanaume wengi tu hawawezi kubadili tairi,wakipata pancha utawaonea huruma wanavyohangaika wakikosa mtu wa kuwatolea....
 
Sister duu ana miliki ndinga ehehehe!
Hawezi kubali kuja kwangu huyu kapanda bajaji mwee
 
Kama wataka lote lote inabidi usubiri kidogo nikuwekee oda toka japan...hapo vipi?

Yani hapa nilipo hadi nimeanza kutetemeka kwa furaha.Kwa hiyo unaniagizia gari gani?......lol
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…