bahati mbaya
JF-Expert Member
- Oct 23, 2012
- 578
- 193
Wanaichukulia kuwa biashara matangazo!
Nipo Nyerere road hapa katikati ya Jiji la Mwanza.Hapa nilipo kuna wadada wawili wote wameolewa na wamevaa sketi fupi sana.Kitendo hiki kinanifanya nijiulize maswali yafuatayo.Kwanza nikiri kuwa huu ni muendelezo wa wanawake kuvaa nguo za ajabu ajabu bila kujali wameolewa ama la.
'
Hivi mwanamke ambae ameolewa kwanini anavaa nguo za kuonesha maungo yake?
'
Sihalalishi mwanamke alieolewa kuvaa hivyo kwa kuwa sina mamlaka hayo,lakini pia huenda ambao hawajaolewa wakawa wanaonesha matangazo ya "biashara"!
'
Lakini inakuaje pale unapoifanyia maonesho biashara au bidhaa ambayo tayari imeshanunuliwa?
'
Au kuna sababu ya wake za watu kuonesha maungo yao?
asante kwa kutupenda na sisi tunakupenda pia!
kama nguo alieivaa yuko okay nayo na anajisikia vizuri mtu mwingine anakereka nini?!....standards hizo za mavazi haya yanafaa haya hayafai kaweka nani?!
Kiazi mwingine huyu,,we unafuata maadili au dini yako inasema hivyo?usiwe unafikiri kwa MASABURIKama mumewe hajamkataza acha avae, pengine wote wanapenda.
Binafsi sidhani kama kuna umuhimu wa mtu kukereka na mavazi ya mtu mwingine ambae hamhusu hata kidogo (sio mke, ndugu wala rafiki yako) maana kila mtu na mambo yake. Wewe unayoyaita maadili pengine mwenzio hayajui wala hayamhusu, kimaadili kwao wanafunga kaniki fupi tu chini na maziwa wanaacha wazi. Leo hii anakuja mjini, anajitahidi kujifunika kwa kiasi chake we unamsema kuwa anaenda KINYUME na maadili bila kufikiria kwamba maadili yako sio lazima yawe yake yeye.
Nipo Nyerere road hapa katikati ya Jiji la Mwanza.Hapa nilipo kuna wadada wawili wote wameolewa na wamevaa sketi fupi sana.Kitendo hiki kinanifanya nijiulize maswali yafuatayo.Kwanza nikiri kuwa huu ni muendelezo wa wanawake kuvaa nguo za ajabu ajabu bila kujali wameolewa ama la.
'
Hivi mwanamke ambae ameolewa kwanini anavaa nguo za kuonesha maungo yake?
'
Sihalalishi mwanamke alieolewa kuvaa hivyo kwa kuwa sina mamlaka hayo,lakini pia huenda ambao hawajaolewa wakawa wanaonesha matangazo ya "biashara"!
'
Lakini inakuaje pale unapoifanyia maonesho biashara au bidhaa ambayo tayari imeshanunuliwa?
'
Au kuna sababu ya wake za watu kuonesha maungo yao?
Awe mfano wa kuigwa na nani?...kuna mahali popote kuna nukuu hii au umejisemea tu??
uige maisha/tabia za mtu zinakuhusu nini??
Eiyer, watu wamenena. Elewa kwamba kila mtu ana standard zake za mavazi. Huenda unachovaa wewe wengine kamwe hawatathubutu kuvaa, haimaanishi kuwa kuna tatizo na nguo zako. La hasha. Mavazi ni relative.
Kwani nguo fupi ikoje? Wengine ikivuka kisigino tayari umeonesha too much. Na maungo yao hasa ni nini? Mapaja? Wangekuwa wamevaa kaptula ya mazoezi ungekuja kuanzisha thread hapa? Aisee unanikumbusha mwaka 94 mama yangu alikuwa amevaa suruali watu wanamshangaa mtaani Dar es Salaam. Ilikuwa suruali ya "heshima", yaani haijabana maungo ya kitambaa cha cotton, sio jeans. Siku hizi suruali ni kitu cha kawaida. Subiri utazoea hizo sketi in no time.
Otherwise, mind your business. Mkataze mkeo au binti zako lakini si watu usiowafahamu.
Mbona huvai kimini ukiwa na wazaz wakog?ni ushamba wa kugeza kila kitu..na usijidanganye km ndo unatutega wanaume mi ntakutamani nikutumie km kondom then cwez oa m/mke mwenye hzo mambo nivalimie mimi mme wako unamuonyesha mat.a.k.o nani au mapaja?
Pole sana.ila tambua kila mtu anamtazamo wake juu ya mavazi na mtazamo wangu mimi ni huo.kuna nguo za kuogelea,za job na hapa inategemea na Aina ya kazi unayofanya,za mazoezi,za mtoko,za kuingilia kwenye nyumba za ibada n.kkwa Hiyo mtu anatakiwa achague nguo kutokana na eneo husika.na uelewe kuwa unachokipenda wewe sicho akipendacho mwenzio wengine mavazi hayo wananunuliwa na waume zao na ndo wanapenda wavae hivyo.
sawa furahisha nafsi ila usishangaze jamii inayokuzunguka pia Suprise!unaweza tazamwa kama umependeza pia waweza tazamwa ukiwa kituko mbele za watu,mi kuna umri ukifika sina budi kustopisha vimini vya kutisha kwa sasa twende kazi!
Mhhh! wabongo bana!
Mbona jamaa wa kimasai wengi hawavai Nguo za ndani wala suruali na muda mwingine Madude yao yananinginia,
mama zao na dada zao wanavaa zile bangili za miguuni hatushangai, na tunawasifu kweli jinsi wanavyobeba uAfrika wao!
wengine tunawapigia kelele kweli na kuwadhalilisha!
Hizi Double standards zatoka wapi??
Kwanini ustopishe ukifika huo umri!