Wanawake fake!!....

yote hayo mnasababisha nyie nyie wanawake fake,ndio maana tunaenda kutafuta tulizo huko!!!

aka! mi si kisababishi, we kama una anayekusabisha kwenda msemee yeye, na umueleze unavyomkomoa kwa kwenda nje...useless!
 
Haya usemayo ni kweli,lakini faham kuwa comvincing power ya mwanamke ni kubwa sana kama atataka mabadiliko katika mahusiano/ndoa yake!

Convincing power!! Unakiri udhaifu kuwa sis tuna convincing power kubwa sana, ndo yale yale mtu anafanya upuuzi anasingizia shetani,mara sijui hata Eva alimdanganya Adamu...use your common sense, mwanamke ni binadamu tu, na ana uwezo wa kutumia akili yake vibaya au vizuri kama ulivyo wewe.....na kwenye hili wanawake tumetofautiana.
 
Michelle,achana na tofauti za akili,pia hapa sizungumzii excuse ya kufanya kosa na kumsukumia lawama shetani,nazungumzia nguvu ya kimaumbile aliyonayo mwanamke kwa mumewe anapotaka jambo fulani litokee,mf,Adamu na Samsoni!Nguvu hii Mungu alimwekea mwanamke kwa malengo chanya ya kumsaidia kumsaidia mwanaume kufanikiwa,kumfariji pamoja na kumpa pumziko,haya kwa wanawake wa leo hayapo!Ni vurugu kila kukicha na pilika za hovyo coz wamekua wa hovyo sana!
 
Michelle,achana na tofauti za akili,pia hapa sizungumzii excuse ya kufanya kosa na kumsukumia lawama shetani,nazungumzia nguvu ya kimaumbile aliyonayo mwanamke kwa mumewe anapotaka jambo fulani litokee,mf,Adamu na Samsoni!Nguvu hii Mungu alimwekea mwanamke kwa malengo chanya ya kumsaidia kumsaidia mwanaume kufanikiwa,kumfariji pamoja na kumpa pumziko,haya kwa wanawake wa leo hayapo!Ni vurugu kila kukicha na pilika za hovyo coz wamekua wa hovyo sana!

Wanaume wa leo wakoje? Hudhani kwamba yale mnayopokea ni kwakuwa mnastahili hayo?? Wapo wanawake wazuri walio tayari kushirikiana na mwanaume kufanikiwa, kuwa tu na subira na malengo sahihi na omba Mungu...!
 
Ni vurugu kila kukicha na pilika za hovyo coz wamekua wa hovyo sana!

Eiyer unataka kulelewa kama yai?? Unataka ukihitaji kujisaidia uletewe poti?? Unataka mke wa kukulindia nyumba, kukupikia, kukufulia nguo na kukusafishia chumba tu au?? Unataka mke utakaekuwa unamgea hela kwa kumrushia alafu anasema 'as you wish my lord'?
 
Kama mngekua na akili ya kutulia na wake/girlfriend zenu bila kutafuta wanawake wa nje basi mngepata muda wa kugundua huwa tunawajali na hio fakeness mnatengenezeana nyie wenyewe wakati wa uchumba mpaka ndoa infact huwezi ku generalize basing on sample ulizokutana nazo wewe au few examples ulizoona. Daaah!
 
ama kweli kila mwamba ngoma uvutia kwake, yan wanaume ndio chanzo cha matatizo yote kuanzia kwenye mahusiano had ndoa!
kwanza hamjuagi mnataka nn, macho yenu yako juu juu kama mnachambua mchele kazi kuendeshwa na matukio halafu lawama watupiwe wanawake duuh! very unfair, badilikeni muone basi.
 
Tatizo sio mtu kujua kama ana nguvu au la ni mtu kuwa na malengo au kutokua nayo. . . kua na fikra za kujiendeleza na kuendeleza familia au la. Hata asie na hayo bado anatumia unamke wake kuchezea vijisenti vya mume na kumnyamazisha asilalamike/kumfanya asiache kutoa hizo pesa na kadhalika. Kwahiyo wote wanatumia hiyo nguvu. . .kinachotofautiana ni matumizi.

Ndio maana bado ntasema kosa linaanzia kwa wanaume wanaingia ndoani na wanawake ambao hawana malengo wala fikra za kujijenga kwa faida ya baadae ilhali sio aina ya mwanamke wanaetaka kuishi nae milele milele. ACheni kudanganywa na hayo mawigi mnauolipia na muanze kuangalia mambo ya msingi. Ndio maana wengine tunachagua mpaka tunaonekana tumezidi. . yote hiyo ni ili kupata mtu wa aina ile tunayohitaji na sio anaevutia machoni tu. Hamtokula sura wala maumbo kwahiyo huo usiwe msingi wa yale mnayotumia kuchagua mke.
Hivi duniani humu kuna binadamu aliyekamilika,can you, for that matter any person,find a soul partner who will PERFECTLY fit the bill? Bishanga wonders!
 
Kama mngekua na akili ya kutulia na wake/girlfriend zenu bila kutafuta wanawake wa nje basi mngepata muda wa kugundua huwa tunawajali na hio fakeness mnatengenezeana nyie wenyewe wakati wa uchumba mpaka ndoa infact huwezi ku generalize basing on sample ulizokutana nazo wewe au few examples ulizoona. Daaah!

Lakini Amyner,siku hizi,has mijini mi naona mshiko umepewa kipaumbele sana na wanawake wanasema openly kuwa......'mwanamke haongi anahongwa bana'.....yaani hat a ndani ya ndoa nyingi haka ka element kapo ban a.
 
Eiyer,ckubalian na ww kwa namna ulivotugeneralaiz hapa,napingana nawe kwa nguvu zote co wanawake wote tuko ivo,bahati mbaya tu umekutana na wa ivo,kwan wapo wengi tu wamepata wake wa ukweli,mmojawapo atakaenioa japo cjakamilika km binadam ila sio wa hovyo!ukiwa fake utakutana na fake mwenzio,na km ulichagua koroma uctarajie kupata tui zito!kafanye na resechi ya wanaume uone namba ya walio hovyo ilivokubwa!
 
Inafahamika kuwa linapokuja suala la uimara na ubovu wa ndoa,kufu au kudumu kwa ndoa wanawake mara nyingi ndo wanakua na nguvu sana,sisi wanaume hapa hatuna ubavu
.

ALAA??Kwanini hamna ubavu wakati nyie ndio viongozi wa familia? Hujui kuwa kiongozi ni kama nahodha.Kama hajui kuendesha chombo si lazima kizame? Utamlaumu abiria aliyeketi kiti cha mbele na nahodha?

Hivyo basi mwanamke akiwa fake/mjinga nk, na ndoa au mahusiano huwa hivyohivyo.

Toka lini mkalijua hili? Ni ufahamu mpya?Kwanini uchague mwanamke mjinga mjinga wa hovyo kuwa mkeo?

Siku hizi wanawake wengi ni hovyo
Ehee...ulifanya utafiti wapi? Hao wengi ni aslimia ngapi ya idadi gani?

ndo maana na mahusiano/ndoa nazo ni za hovyo,siku hizi wanawake hawataki majukum ya kike,wanajua ndoa ni kuzaa na kuwatupia watoto ma HG.Hawajui namna ya kumhudumia mume,huduma wanayoijua wao ni ngono tu,hawawezi hata kumshauri mume namna ya kubajeti matumizi ili angalau wapate ka jumba hata ka vyumba viwili,wao wanajua kubana hela ili wakanunue mawigi,skin jeans,vimin nk,kama ni mfanyakazi mshahara unaishia hukohuko na machinga watajazana nyumbani kwako kukudai hela ya rangi za kucha,khanga na upuuzi mwingi tu!Hawa ndo wanawake watakaotusaidia kusonga mbele kimaendeleo kweli?

Pole sana aiseee..yalikufika ehh? Chagua vema, usikurupuke.
Ama kweli kwa mtindo huu ndoa nyingi zitakua za hovyo ka sababu ya uhovyo wa wanawake wa leo.WANAUME kazi tunayo!
Kazi mnayo si kidogo!
 
Lakini Amyner,siku hizi,has mijini mi naona mshiko umepewa kipaumbele sana na wanawake wanasema openly kuwa......'mwanamke haongi anahongwa bana'.....yaani hat a ndani ya ndoa nyingi haka ka element kapo ban a.

kama ulianza kumhonga kwenye uchumba kwanini usimhonge kwenye ndoa? Au ndio yale yale mwanamke akishaolewa basi mambo yanahamia kwa mahawara wa nje?
Mkijengeana utaratibu wa ku balance maisha interms of benefits and expenses tangu mwanzo automatically itawezekana kusaidiana katika mambo tofauti.
 
Tausi,niliposema hatuna ubavu ni kwamba,hata kwenye kampuni yoyote GM kuna maeneo hana ubavu nayo,inatakiwa apate maelekezo kutoka kwa wataalam wake japokua yeye ni GM,so Mungu alipogawa majukumu hakumpa mwanaume kila jambo ila yeye ni msimamizi wa jumla tu,lakini kama ilivyo kwa GM anavyohitaji sapot na ushauri kutoka kwa walio chini yake ili kupata maendeleo,vivyo hivyo kwa mume pia!Kuhusu risach uliyouliza siokila jambo linahitaji kufanya utafiti mambo yako wazi kabisa,fungua macho utaona.Pia sikuchagua wa hovyo ila nimewakilisha matatizo ya wanaume wenzangu,jitahidi kusoma ili uelewe vyema!
 
Back
Top Bottom