Wanawake acheni kuvaa mawigi

Wanawake acheni kuvaa mawigi

We ndo umepaniki, kuja kulalamikia mawigi ya mwanamke, kama ulikuwa hujui sio mara zote wanawake wanajiremba kwa ajili ya wanaume hiyo ni psychology ya wanawake... They are competitive among themselves.
Hata ningekuwa nimelivaa wewe halikuhusu, hata liwe la kijani teh teh
Ingekua ni kuvutia wanaume wote tungerudi kwenye kuwa natural..
Kuna vitu vingine vingi vinachangia,watuache tu na mawigi yetu...
 
Ushaathirika kisaikolojia kwa Uvaaji wa Hiyo midude kwahiyo hata uambiwaje huwezi kuelewa. Bila shaka una matuta ya Viazi kichwani
Kama mimi nlivoathirika na kukata.

Napenda niwe na nywele za kufunga ki pony tu.

Ingekuwa Tanzania Kuna biashara ya kuuza nywele baada ya kuzikata mbona nngekua tajiri.
 
Alafu utakuta wigi linatoa HARUFU kama kinyesi ptuuuuuuu
 
Hodi mjini, eti Wigi ni nini? Na inavaliwa na wanawake kwanini?
 
Kama mimi nlivoathirika na kukata.

Napenda niwe na nywele za kufunga ki pony tu.

Ingekuwa Tanzania Kuna biashara ya kuuza nywele baada ya kuzikata mbona nngekua tajiri.
hongera sana bibie hakika ww ndio mke wa kuoa
 
Asante.

Ni kujiamini tu. Kama ntaambiwa siendi na wakati pia Sawa.

Kuna na ule mtindo wa kunyoa nyusi th.en wakaweka na wanja. Sijui nani kawadanganya kama wanapendeza wanawake wenzangu. Mi hapana aisee
Nakuelewa sana bibie natamani wale mabingwa wa kunyoa nyusi na kikoleza na wanja wapite hapa wakusome. Unakuta wigi lina mwezi kichwani harufu ndio usiseme lakini unamkuta mwanadada Hajali hilo. ni kweli ulilosema kuwa Wengi hawajiamini na hawaamini urembo waliopewa na MUUMBA
 
Asante.

Ni kujiamini tu. Kama ntaambiwa siendi na wakati pia Sawa.

Kuna na ule mtindo wa kunyoa nyusi then wakaweka na wanja. Sijui nani kawadanganya kama wanapendeza wanawake wenzangu. Mi hapana aisee
Yaani mtu anaenyoa nyusi nachukia sana kitendo hicho. Mke wangu hajawahi kufanya hicho kitu na nilimwambia sitaki kuona wala kusikia kuwa amenyoa nyusi. Jitu kama hilo likitoka kuoga nadhani litakuwa linaonekana kama shetani hivi
 
Yaani mtu anaenyoa nyusi nachukia sana kitendo hicho. Mke wangu hajawahi kufanya hicho kitu na nilimwambia sitaki kuona wala kusikia kuwa amenyoa nyusi. Jitu kama hilo likitoka kuoga nadhani litakuwa linaonekana kama shetani hivi
Ha ha haaaaa.

Binaadam awe hana nyusi lazima atishe.

Ni kujiamini tu. Unajiweka kwenye status ya u natural mpk watu wanakuzoea.

Na wanawake wenzangu sijui hawaelewi kuwa wanaume wengi wanapenda wanawake wawe natural. Huu ndo ukweli
 
Nakuelewa sana bibie natamani wale mabingwa wa kunyoa nyusi na kikoleza na wanja wapite hapa wakusome. Unakuta wigi lina mwezi kichwani harufu ndio usiseme lakini unamkuta mwanadada Hajali hilo. ni kweli ulilosema kuwa Wengi hawajiamini na hawaamini urembo waliopewa na MUUMBA
Mi nimejifunza kwa mamaangu.

Na kikubwa nilichojifunza hata nikapendelea kuwa natural ni kutochakaa kwa uso.

Mapodozi yakizidi yanazeesha kwa kweli.
 
Wengine hayo mambo twayasikia mtaa wa saba. Mwezi mzima kichwa hakiingii maji, damn it..unalalaje na mtu wa hivyo kitanda kimoja? Manake lazima kuwe na odour isiyoridhisha, hata kuchezea nywele...daaah!!
Mengine inabidi tu ukae na kushukuru Mungu...!
 
Aiseehhh mimi huwa nakerwa zaidi nahisi, yani mimi na mama watoto wangu ndo ugomvi kila kukicha,namkataza lakin wapi,unakuta wigi la rangi sijuwi kijani, sijuwi pink yani hakuna relation na uhalisia wa nywele za binadamu, siyapendi mawigi na sipendi kumuona alady amevaa
Dah!! Kama mama watoto anaweka mpaka mawigi ya rangi namna hiyo kama mchezo shoo , huyo ametisha sana.. pole sana ndugu yangu ,
 
Mi nimejifunza kwa mamaangu.

Na kikubwa nilichojifunza hata noikapendelea kuwa natural ni kutochakaa kwa uso.

Mapodozi yakizidi yanazeesha kwa kweli.
H
Mi nimejifunza kwa mamaangu.

Na kikubwa nilichojifunza hata nikapendelea kuwa natural ni kutochakaa kwa uso.

Mapodozi yakizidi yanazeesha kwa kweli.
wengi hawalijui hilo wao wanachojua ni kuwa ukijipoa na mavipodozi huku wakisukumia na mawigi basi wanadhani wanaongezeka urembo kuliko malaika kumbe wanazidi kuwa vibibi bila kujijua. Mwanamke anayejikubali alivyo ndio mwanamke sahihi wa kuoa na ndio mwanamke sahihi mwenye hofu na Mungu. Kama umeumwa na chogo ni Upendo na Uumbaji wa Mungu lakini wenzenu wanadhani ndio wataonekana warembo
 
Umenena ya kweli nywele za asili ni nguzo ya pambo la kichwa kwa mwanamke yeyote..binafsi napendezwa sana nikikutana na mwanamke aliye na nywele zake za asili na zaidi sana akiwa amevaa kilemba kichwani yaaani ananivutia sana nakumuona kuwa ni mwanamke anaejua thamani ya mwili na umbo lake la asili alopewa na Muumba wake...ni kweli wanawake acheni kuvaa mawigi mnatukuza ufalme wa asili msiyoijua kuweni na akili na tena mjiongeze mwajifananisha na sura za kichina,kihindi, kimalasia,kifilipino,kibangladeshi watu masikini wa kwanza duniani niny mnakimbilia minywele yao nanyi akili zenu zitakuwa zakimasikin, mjifananisha na waingereza mara warasha taabu kweli kweli ulishamuona mzungu au mwanamke gani wakihindi anasuka nywele za kiafrika? jib ni hakuna msiuze utu wenu kwa kuiga tamaduni usizozijua...
 
Mwanamke anapendeza na kuvutia zaidi anapokuwa na nywele zake za asili wala sio mawigi. Hiyo ni FACT.

Mawigi yanaboa na yanatupunguzia hisia, mfano pale mwanaume unavyozishika au kujaribu kuzichezea halafu unajua kabisa hizi nywele sio.

Ni kama likofia fulani hivi linalovaliwa au kushonwa kichwani kwa mwanamke, ambayo pamoja na kwamba KIUHALISIA halimuongezei mwanamke mvuto (hata kama ni la Laki Moja), linatakiwa libadilishwe kila baada ya muda fulani.

Wanawake bakini na nywele zenu za asili, zipeni matunzo na usafi wala hamna haja ya kuhangaika na kubadilisha mawigi maana wanaume {99.99%} hatuzipendi. Zinaboa hata kuangalia.

Cha kushangaza, utamkuta mwanamke wa kibongo eti naye anahangaika kuweka liwigi lake vizuri kanakwamba linamzuia kuona vizuri wakati ni FAKE HAIR na yeye mwenyewe kaliweka hivyo kwa makusudi kuiga Wazungu.

Say NO to Fake Hair.
Mwanamke kupendeza kaa na ushamba wako
 
Back
Top Bottom