Lol i'm talking out of personal experience nilishadate na mwanaume hana pesa kwa miaka miwili pesa alizowahi kunipa kiujumla hazizidi hata elfu kumi yaani hata akinikopesha elfu mbili atanidai lakini kilichofanya nimuache wala siyo huo ubahili wake bali ni ubabe wake
Alitaka kila anachoamua yeye nifanye hakutaka kunisikiliza hata mawazo yangu halafu mbaya zaidi kwake kuna vitu vilikuwa na umuhimu zaidi kuliko mimi alikuwa anapenda sana mpira hata kama tulipanga kuonana kama kuna mechi yuko radhi ahairishe kuonana na mimi akaangalie mpira na siyo mara moja
Anyway mimi sikumkataza kufanya starehe zake ilikuwa too much hadi watu wengine wakawa wanamshangaa nilidhani angebadilika lakini alikuja kunihakikishia mwenyewe kuwa hawezi kubadilika hivyo ndivyo alivyo hata tukioana bado atakuwa hivyo hivyo tena hapo nimeongea machache tu ila ningeongea yote nisingeyamaliza hapa
Hapo ndipo nilipoamua nijiengue tu mapema well hadi leo ninavyoongea na wewe hapa ananiomba turudiane lakini mwenzie nilishafunga huo ukurasa anasema eti akiachana na mimi itabidi ajiandae tu kisaikolojia kupata mwanamke anayependa pesa hapo ndo nikakumbuka ule msemo hauwezi kujua thamani ya kitu hadi kipotee