Sheillah Sheillah
JF-Expert Member
- Jun 17, 2020
- 583
- 1,478
Za weekend?
Hivi mwanaume timamu kabisa mke wako kagombana huko na wanawake wenzake halafu wewe unaenda kuingilia ugomvi na kuanza kusutana na wanawake?
Kwanza mwanaume unatoa wapi ujasiri wa kurushiana maneno na mtoto wa kike? Mpenzi wako akiudhiwa huko na marafiki zake wewe msaada unaoweza kumpatia ni kwenda na wewe kusutana?
Hapo ndio unaonesha Manhood yako? Ndio mkitoka hapo akuambie "safi sana mpenzi wangu umewasuta mpaka wamekoma"? Ndio sifa mnazoziona za maana siku hizi?
Leo nimepita mahali nikakuta kuna ugomvi wa watu wanatoleana maneno(kusutana). Mnaweza mkafikiri ni wanawake eh? HAPANA! ni mwanaume tena mume wa mtu kaenda kumsaidia mke wake kusutana na Bi dada mmoja ambaye anauza duka hapo.
Karibia kila mtu aliyekuwa anashuhudia lile alisikitika sana na kuona aibu kwa ile misuto mwanaume tena mume wa mtu aliyokuwa anaitoa.
Wanaume wenye hizi tabia badilikeni mnakera na kuaibisha sana. Tafuteni hela mpenzi wako akigombana huko mnaenda police na sio unaenda kumsaidia kusutana.
Acheni kujitoa uwanaume wenu kwa vitu vya ajabu. Wanawake kwa wanawake kugombana ni kawaida ila kisicho kawaida ni mwanaume kuingilia ugomvi na kusutana.
Mwanaume unayesutana na mwanamke au hata kutupia maneno wanaume wenzako unajishusha sana. Unadhalilisha nguvu ya manhood iliyowekwa ndani yako. Mwanaume pesa maneno maneno tuachieni sisi wanawake.
Hivi mwanaume timamu kabisa mke wako kagombana huko na wanawake wenzake halafu wewe unaenda kuingilia ugomvi na kuanza kusutana na wanawake?
Kwanza mwanaume unatoa wapi ujasiri wa kurushiana maneno na mtoto wa kike? Mpenzi wako akiudhiwa huko na marafiki zake wewe msaada unaoweza kumpatia ni kwenda na wewe kusutana?
Hapo ndio unaonesha Manhood yako? Ndio mkitoka hapo akuambie "safi sana mpenzi wangu umewasuta mpaka wamekoma"? Ndio sifa mnazoziona za maana siku hizi?
Leo nimepita mahali nikakuta kuna ugomvi wa watu wanatoleana maneno(kusutana). Mnaweza mkafikiri ni wanawake eh? HAPANA! ni mwanaume tena mume wa mtu kaenda kumsaidia mke wake kusutana na Bi dada mmoja ambaye anauza duka hapo.
Karibia kila mtu aliyekuwa anashuhudia lile alisikitika sana na kuona aibu kwa ile misuto mwanaume tena mume wa mtu aliyokuwa anaitoa.
Wanaume wenye hizi tabia badilikeni mnakera na kuaibisha sana. Tafuteni hela mpenzi wako akigombana huko mnaenda police na sio unaenda kumsaidia kusutana.
Acheni kujitoa uwanaume wenu kwa vitu vya ajabu. Wanawake kwa wanawake kugombana ni kawaida ila kisicho kawaida ni mwanaume kuingilia ugomvi na kusutana.
Mwanaume unayesutana na mwanamke au hata kutupia maneno wanaume wenzako unajishusha sana. Unadhalilisha nguvu ya manhood iliyowekwa ndani yako. Mwanaume pesa maneno maneno tuachieni sisi wanawake.