Muwe mnatuwekea na bia.
Sasa kama unapika chuzi kama bahari ,ubwabwa utadhani mtu unatafuna karanga nani atakula au nyama ngumu mpaka kuimeza inabidi utafute kwa kuegemea au ugali mgumu mpaka kuumega mpaka misuli ya mikono inakusimama kama unanyanyua kitu kizito.....inatakiwa ujiulize kwanini hali sio unalalamika..kwani huyo ni mumeo.
cc mhusika
Hongera kwa habari nzuri.Kwa kweli wanaume wanakera utakuta mwanamke kapika tena vizuri alafu mwanaume akija hali mnakera wanau me muache hii tabia
Kuna jamaa mkewe
hampikii,mke anapita gengeni kununua vihepe
mume akirudi anatengeneza chai na ubwabwa mkavu.
Wananifurahisha sana.
wapo kiroho safi.
na sabuni ya kuoga
kila mtu nana ya kwake.
hata ndoo za maji.
Wanawake wazuri sana mtandaoni ila majumbani mnafanya vituko vitupu wengine hata kuweka maji ya kuoga ya mume au kauli nzuri ya kumfanya mume ajisikie kula hamna,mume akijua muda wa kurudi nyumban umefika anatamani aendelee kubaki kazini unadhani hapo hamu kula itakuwepo!?jichunguze na mchunguze mumeo kuna mmoja anamatatizo pia simu zipo kabla hujaandaa weka utaratibu wa kuwasiliana kama siku anachelewa kula akupe taharifa usipike na kama siku anawahi kula anakupa taharifa pia.Mimi mke wangu aandai chakula mpaka tuwasiliane maana pia inategemea siku hiyo nina hamu ya kula nini sio mchana nimekula ugali then jion tena uniwekee ugali maharage sili bora nikanywe soda nilale.
hata mi huwa namind sana hii tabia, najikoki pika weee karangiza af mtu anakula vijiko viwili ananiboa
cc: mhusika
Umezidi upana nawe.....lol!!!!
asubuhi usimpikie chai, kaanga moto cha usiku umpe
Hahahaha ale kiporo asubuh asubuh lol
Heshima kwako.
Dada kama ni kila siku, inaweza kuwa kuna kitu kinaendelea. Lakini kama ni baadhi ya siku hiyo, haina shida. Kiafya usiku mtu hutakiwi kushiba sana, maana hakuna kazi kubwa unayofanya. Usidanganywe na maoni ya watu wasiokuwa na ndoa kama yanavyoonekana hapo juu, mume ni wako, wewe ndo unamfahamu zaidi kuliko mtu mwingine. Unapaswa kuchunguza kwanza kabla ya kuchukua hatua ya kuamka na kula chakula chote hadi kuvimbiwa kama alivyokushauri Nivea.