Wanaume wengine washamba tu kuazima azima vitu

Wanaume wengine washamba tu kuazima azima vitu

Tatizo lenu masista duu na wadada wengi wanampenda MTU kwa muonekano wake kitu ambacho sio sahihi.
Kaa na MTU umsome kwa muda utamfahamu tuu na home kwa MTU panajulikana. Mnawafose vijana wawadanganye.
Huwa naishi kawaida sana kimuonekana kiasi watu washawahi niuliza mara kadhaa kuwa kaka upo simple kiasi tunashindwa kukusoma.
Wadada kibao washawahi kuja kwangu na walishangaa sanaaa ila mmoja alijikuta ananiambia kuwa mbona nje upo simple kumbe unakaa pazuri hivi aiseee daaah sikuamini.
Nikamwambia kuwa that's who I'm
Selling manifesto,anotha gear I've learnt .
 
Tatizo unaweza kuta mtu amekupenda lakini wewe umejiweka level fulani ya juu kwahiyo ili akupate lazima atapretend kuwa na yeye ni wa level hiyo uliyoko au hata amekuzidi hata kama itamlazimu kwenda kuazima nguo,perfumes,gari,ghetto and all accessories ambazo lazima akupate.So you girls/women stop pretend being classic and we men/boys will have your path with us 😀😀😀😀😀
......."will have your path with us" umejitahid but it should be you not us.
 
Alaa unakuta mwanaume ameupala anang'aa mtaani, safari zake mliman city na mbezi Mbezi,

Kumbe nguo zenyewe kaazima,
Kama ni gari nalo kaazima ni mambo ya aibu mno,

Hasa kuna wale wahongo kama nini sijui, ooo Mimi Nina iki Mara kile, ooo Mara baba yangu sijui ni nani,

Ooo namiliki maduka ya hardware kumbe mnawekwa mjini na masugar mamy, mnasimamia tu ,

Funguo ya kitasa unapokaa inakutu vitasa vyenyewe mpaka unyanyue mlango makubwwa,

Ooooo baby nakupenda sijui nitakununulia kiwanja, we Mwenyewe huna godoro mxhiuuuu!!!!

Mbaya zaidi na chumba hujapanga wewe unawadanganya wasichana kwamba ni kwako kumbe huna hata kwako, unaazima kupigia dyudyu tu,

Wasichana amkeni ukiona mwanaume wako anakupeleka sehem anasema kwake anaishia sebuleni we ingia chumbani kwa nguvu , toa mashuka na nguo jifanye utayafua, au jifanye unasalimia majirani ,kijasho lazima kimtoke,

Eti Nina hela wakati hata simu anaazima,

Analeta ATM card kuonesha kumbe zime expire mwaka juzi, na anasema ni ya NMB wakati ni ya KCB

OOO BABY NINATAKA MWAKANI NIKUOE YAAN HAMNA SONI

TAFTENI HELA ACHA HABARI ZA KIJINGA,
Ninyi mnapenda wanaume wa namna hiyo nikikwambia ukweli kwamba mimi nalima mahindi huko kijijini Muharamba unaniona mshamba
 
Hahahaaa wanapenda Pesa mno,
Nakwambia kama nyani na ngedere wangekuwa na pesa bila shaka kuna wasichana wangekuwepo msituni mida hii wakifanya yao
Hahahah we mjamaa umewaza mbali dah
 
Wanaume! Wangap wamekudanganya na wewe unakubali tu kumbe wanakudanganya?
Halafu walishaisoma akil yako
 
Wakongomani waliwatafuna sana dada zetu mwishoni mwa miaka ya 90 na mwanzoni mwa 2000, jamaa walikua wanatembea na mabulungutu ya dollar fake. Sasa wakati wa ku clear bill Mkongomani anatoa wallet au bunda la dollar, demu anaambiwa hakuna change Cherie tutapitapo ku bureau de change wee lipa, kwa hiyo mwanamke analipa na kumhudumia jamaa kwa matumizi mengine hata wiki mbili, sasa mgeni akisharudizake Mbunji Mayi au Lubumbashi ndio Cherie anazinduka na kilio cha kuachiwa makaratasi na kesi juu!
Aisee hii ni hatari mno na kiukweli wanawake wenye uwezo wa enzi zile waliumizwa sana. Nina anko wangu ndio ilikuwa michezo yake kuwadanganya mademu wazuri wenye pesa. Alikuwa handsome and biggie kama kina fatjoe plus anajua mapigo enzi za ma fubu, coogi and dada! Masuti makali, inshort kuvaa viwalo vya laki 8 mpaka M haikuwa ishu na shopping anafanyia posta sio ushenzini utamtaka yani. Hapo ndipo watoto wakike walikuwa wanakolea na confidence alionayo ni ya kutotia shaka kwa lolote.

Dah alisumbua sana mjini hapa na harakati zake ilikuwa kujipa title ya u CEO ama mfanyabiashara wa kimataifa huku akiwapanga wadada kuwa kuna bishara kubwa anafanya kimataifa so ni mtu wa kusafiri sana na alikuwa na confidence ya ajabu.

Mwanzo huwa anatumia pesa yake kuhudumia na kukoleza penzi mwanamke anaona amepata mtu maana jamaa yupo njema mno very presentable lugha inapanda mno shughuli inaishia ambapo anazuga na kontena limekwama hebu niazime mil.5 mpenzi nimepungukiwa kidogo then nikishatoa mzigo ntakupa 10mil kabisa lazizi.

Demu akiingia kingi tu imekula kwake na wengi walikuwa hawachomoi maana anawapanga baada ya kuwakaza sawasawa ndani ya hoteli kali enzi za sheraton hotel.
 
Mbona nyie Nywele feki, sura feki, kope feki, chuchu feki, tako feki, kucha feki, kuongea feki,kutembea kifeki,kusimama kifeki, etc na unapata bahati ya kutongozwa?!
 
Hahahahahaha naona kuna mtaalamu kakuingiza mjini .
Pole sana ndo tatzo la kupenda hela.
 
Hao sio wanaume ni wavulana, acha kuhangaika na wavulana.
 
Pole sana Dada kwa kudanganywa, ila na nyie wadada inabidi mjitafakari upya. Unakutana na kamanzi kanawaza kupata bwana mwenye mafanikio yake wakati huyo manzi yeye unajua kupaka lipstick tu. Jiongezeeni thamani zaidi ya hizo lipsticks pia mjifunze law of attraction.
 
Bila kusahau na ninyi pia ni fake,
kucha feki
kope kama kofia ya peter manyika ................feki
kalio............................................................feki
Nywele.........................................................feki
Bikra............................................................feki
love ............................................................feki

Acha tuazime tu, maana it's not worth kutumia jasho halali kwenye fake zones.😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀
Mkuu sio hivyo tu unakuta wanajazana mlimani city kama vile wanafanya shopping kumbe maigizo tu, ukimtoa out anataka ale piza wakati kwao kaacha viazi na mihogo. Swaga nyingi kumbe vimeo tu.
 
"....Wasichana amkeni ukiona mwanaume wako anakupeleka sehem anasema kwake anaishia sebuleni we ingia chumbani kwa nguvu , toa mashuka na nguo jifanye utayafua, au jifanye unasalimia majirani ,kijasho lazima kimtoke..."

Aisee, unataka kuharibu mipango ya watu.

Kote huko mbali, tafuta jiko lilipo na kula chakula utakachokikuta huko,fungua friji kazi kunywa maziwa. Nenda kabatini angalia chochote kinacholika kula kama ni crips, chocolate.
Uone jamaa atakavyobadilika ghafla
 
Back
Top Bottom