Wanaume wengine bwana!!

Zero One Two

JF-Expert Member
Sep 16, 2007
9,347
3,023
Kuna dada mmoja.ni rafiki yangu tunafanya naye kazi na tumetoka naye sehemu moja. Huyo dada aliunga urafiki wa kimapenzi mwaka juzi na kaka mmoja anafanya kazi wizara ya ardhi uhusiano wao ulikuwa wa furaha coz mara nyingi huyo bi shost alikuwa akinihadithia alivyokuwa anainjoy na mpenzi wake huyo na kuna wakati nilikuwa nikitoka nao kwa kweli walipendezea na walionekana wakiwa na furaha.

Walikuwa wanaishi kila mtu kivyake ila mwaka jana mwanzoni waliamua kutafuta nyumba kubwa ili waishi wote na amani ilikuwepo pale pale.
Ktk jambo la kheri yule dada akapata ujauzito mwishoni mwa mwaka huu kwenye mwezi wa 11 yule kaka akafanya fasta kumtambulisha kwao na yule dada kadhalika. Sasa wakati dada analea tumbo visa vilianza cha kwanza akajitokeza mwanamke akasema amezaa na huyo kaka mtoto wa kiume na wanafanya nae kazi ofisi moja na dogo ana 5 years na ni mpenzi wake toka wanasoma chuo cha ardhi so ni mwanamke wake zaidi ya 15 years kuulizwa kidume akasema suala la mtoto ni kweli anaulizwa na demu wake kwanini hakumuweka wazi jamaa akajitetea aliogopa labda wangeachana kutokana na ukweli huo.

Huyu dada akasema sawa akaendelea kuishi na jamaa ila kutokana na ukweli huo kujulikana yule dada akawa anaishi kwa mashaka makubwa mno ikafikia wakati wa kujifungua sasa ameenda kwao kilimanjaro hapa ninavyokwambia anyday atajifungua.but kilichompata sasa wiki kama mbili zilizopita alikuwa anawasiliana na huyo mpenzi wake kama kawaida kwa sms na calls ilipofika mida ya saa 2 usiku simu ya huyo mpenzi wake ikazima yule dada akamtumia msg koz ni kitendo ambacho yule dada hakipendi hata kidogo.akamtumia msg mbona umezima cm na tulikubaliana hutafanya hivyo bby??.

Yule dada alikaa usiku kucha asubuhi saa moja ile msg ikaonyesha deliverely report then namba ya mpenzi wake ikabeep yule dada haraka akapiga cm kumuuliza mwenzie kulikoni alisikia sauti ya kike badala ya mpenzi wake ikimuuliza wewe kwa nini unatuma msg kwenye cm ya mme wangu naomba ukome tena sana iwe mwanzo na mwisho yule dada alikuwa jasiri akamwambia naomba basi niongee na huyo mumeo yule dada akakata simu ikawa imezimwa ikakaa kama lisaa ikapatikana tena yule dada kupiga akapokea mpenzi wake cha kwanza kuuliza akamuuliza yule kaka uko wapi jamaa akajibu home akamuuliza hujatoka kwenda ppt akajibu no toka niingie kulala jana cjatoka yule mwanamke ndo akamuuliza sasa imekuwaje kuna mwanamke nimeongea naye kwenye simu na amenitukana nisikuzoee na ametumia simu yako? Yule kaka alikosa jibu mpaka leo hii anachosema ni kwamba hakuwa na mwanamke that day.

Dada yule amechoka kimawazo na anataka kuachana na huyo kaka kwasababu ameona huyo kaka sio mwaminifu na amekosa imani nae na huyo kaka naye amepunguza mapenzi sio kama mwanzo walivyokuwa pamoja hana muda na mwenzie toka amlete kujifungua hajaja hata kumpa hi jamani tunamsaidiaje huyu binti wa watu?????
 
kuna dada mmoja.ni rafiki yangu tunafanya naye kazi na tumetoka naye sehemu moja.<br />
Huyo dada aliunga urafiki wa kimapenzi mwaka juzi na kaka mmoja anafanya kazi wizara ya ardhi
<br />
<br />Kwahiyo unataka tufanye nini?
 
Mhhh hapo Sasha ni balaa. Inaonekana jamaa sio mwaminifu. Kama kuna issue ya mtoto tena mkubwa kiasi hicho na hakuona haja ya kumwambia mwenzake na bado simu za wanawake mhhh achunguze sana kabla hajarudi kwa huyo jamaa
 
aggghhh..... Mijitu mingine ndio inalaana. Hela zake zote atakazokuwa akipata zitakuwa zinaishia kwa wanawake. Hatojenga, wala hatototunza hata wazazi wake kwa jinsi ambavyo wanawake tulivyomlaani.
 
Japo itamwia vigumu sana ni vema akajiweka pembeni kwani huenda kuna mengi atakua amemficha
 
Mmh! Hapo mwambie huyo dada kuwa aende kwa wale aliowatambulisha ili awaeleze hayo matatizo yake,nafikiri kuna mmoja hatamsaidi
 
nadhani jamaa nia yake ilikuwa ni starehe tu na si kuoa. aiona raha kumega tu na kupikiwa. kuweni makini sana wanawake, mara nyingi sana huwa nawaambi ukiona mwanamme aba ku entertain saaana sijui nitoko miiingi (hicho ndo kinacho waua) kila wikiendi kiwanja kipya huyo si muoaji. na nyie akina dada msiwe rahisi kuhamia kwa mwanaume haraka haraka na kukubali kubeba ujauzito kabla ya ndoa jamani. wengine km huyo ana mtoto tayari so uzazi kwake kazoea so no xcitement km ingekuwa ndo firstborn. mpe pole huyo dada!!
 
Kupitia kipindi kigumu hivo tena karibu anajifungua! Mungu amsaidie asije pata kifafa cha mimba,maana msongo wa mawazo unaweza mpelekea akapata matatizo wakati wa kujifungua, atulize akili ajifungue kwanza, kwa sasa amwache tu huyo kaka asimfatilie, akishamfata ndio waongee sasa inakuwaje?
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;Kwahiyo unataka tufanye nini?
<br />
<br />
If u'r not interested to the topic do not post any thing. Si kwamba wote hawana chakufanya with ths thrd. Kila mmoja inamgusa kwa namna yake. Kama we haikugus, u better skip to the topc that u think unaweza kufanya chochote. Hapa jf kuna watu wengi, dont generalize u'r views to all. Binafsi sipendi hii tabia.
 
Ndo maana kila siku tunawaambia dada zetu msikimbilie kubeba mimba za watu ambao hamuwahamu vzuri. Ona sasa huyo ni mtoto mwingine ambaye nina uhakika atakosa malezi ya baba
 
Back
Top Bottom