Hbr za jioni Wapendwa wana JF wenzangu??,Nimekuwa nikisikia mara kadhaa kuwa Wilaya ya Rombo,mkoa wa Kilimanjaro kuna shida sana ya ulevi,hivyo kupelekea akina Baba kutowajibika vema ktk majukumu ya familia km Baba.
Leo katika kufuatilia kipindi cha RIPOTI MAALUMU kinacholetwa na ITV,nimeona jinsi ulevi ulivyokithiri huko Rombo ambapo akina mama wanalalamika kuwa Waume zao hawatimizi majukumu yao ktk familia,wamekuwa legelege,kazi za Kutumia nguvu hawawezi kuzifanya,Mama mmoja amesikika akisema kuwa hata mambo ya chumbani hawawezi tena (poor performance).
Mwanaume mmoja alipoulizwa kuhusu hali hiyo hususani kushindwa kuwahudumia wake zao Mambo ya ndoa,alijibu kuwa yeye hana muda wala interest na Mambo ya ndoa.
Bibi mmoja alipoulizwa kuhusu hali hiyo amesema anasikitika kwasababu kizazi hicho kinaelekea mwisho kwasababu Wanaume wanazidi kuisha huko Rombo hivyo itakuwa vigumu kupata watoto kutokana na ulevi uliopindukia.
Aidha Ktk mahojiano ya mwandishi na vijana wengi,imeonekana kuwa vijana wengi wa kiume wameachana na wake zao kutokana na ulevi hivyo Wanaume hao wanalelewa na mama zao, huku watoto wao wakiishi na wake zao.
My take: Vijana wa Kiume kutoka Mikoa mingine twendeni Rombo tukawasaidie Wanaume wenzetu walevi kuwahudumia wake zao ili kizazi cha Rombo kiwe endelevu.
Chanzo: RIPOTI MAALUMU-ITV