labda mila za mtoa mada ndo haziruhusu. Mila za kwetu unaweza kuishi hata mwaka mzima kama muda wako unaruhusu. Wale ni wazazi wako kama walivyo wazazi waliokuzaa. Tena mara nyingi wakwe wanawapenda sana wakwe zao kuliko hata binti yao wakati mwingine. Mimi nikienda likizo huwa tunaanzia kwa wakwe, tunachinjiwa kuku siku ya kwanza kupasha. siku ya pili wanachinja Mbuzi, tukimaliza kumla kama siku mbili tatu hivi tunachinjiwa tena kuku. hapo ni siku si chini ya siku saba tunakuwepo kwao. Then tunahama mji kwenda kwetu kwa idadi ya siku kama tulivyoka kwa wakwe. Mtindo ni huo huo wa kula kuku na mbuzi hadi watoto wanaanza kugoma kurudi mjini. Inabidi wadanganywe kuwa wanatusindikiza sisi then wao watarudi kwa bibi na babu. ni full raha. kama hupendi kukaa kwa wakwe zako basi una matatizo binafsi. wale ni wazazi wenu wewe na mke wako.