Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,799
- 59,264
Dah. . . kumbe waMassai nao wanajua kuFLIRT ehhhh?Hehehe. . nilidhani hayo ni mambo ya watu wa mujini tu.
Nwy siku zote tunasikia na kuambizana kwamba mwanaume ni yule anaeweza kujali,lisha na kulinda familia yake (provide for them). Miongoni mwa watu wanaoonekana wanaume kwenye jamii yetu ni waMassai kwa uhodari wa kuwinda na hata kuua simba kwa mikono, tena wakiwa na mikuki/sime zao ndo kabisa wanaonekana wa ukweliii.
Pamoja na kwamba nimewahi kuishi nao miaka ya nyuma, sikuwahi kujua baadhi ya mila zao juu ya maisha ya kila siku na namna yanavyoendeshwa ila sasa nimejua na ndio nikapata maswali kadhaa juu ya wanaume hao.
Kwanza kabisa hawajengi. Anaejenga ni mwanamke (mke/wake zake), na ole wao mvua inyeshe alafu bwana anyeshewe. . . lazima mama aambulie kibano na aeleze kwanini 'bwana inyeshewe'( in a Massai accent).
Pili chakula anatafuta mama.
Kutwa nikiangalia naona wanawake ndio wanaopita na punda + madumu kwenda kutafuta maji na kuni wanakokujua wao.
Wanaume utawaona wanapita fimbo zao + mbuzi na ng'ombe kupeleka machungani tu BASI. Wakija dukani wanaume wengi ni wanaulizia kiroba na beer. . . wachache sana watataka chumvi, sukari, mafuta, mchele au hata pipi za watoto kuashiria anakumbuka na kujali familia.
Mashine (kusaga na kukoboa) wanaokuja ni wanawake. . .
Kukamua wao. . .
Kupika wao. . .
Malezi wao. . .
Yani wanaume wao ni machungani kwenda kupiga soga huko wakati wamama wanapanda na kushuka na barabara. Kwa ufupi. . .wanalelewa na kutunzwa na wake zao.
Je nao ni wanaume? Au ndo sawa na wale wanaoitwa 'MARIO' mjini? Au yeye sio muAfrika hivyo ule utamaduni wa 'mwanaume wa kiAfrika ni provider' hauwahusu?
Nwy siku zote tunasikia na kuambizana kwamba mwanaume ni yule anaeweza kujali,lisha na kulinda familia yake (provide for them). Miongoni mwa watu wanaoonekana wanaume kwenye jamii yetu ni waMassai kwa uhodari wa kuwinda na hata kuua simba kwa mikono, tena wakiwa na mikuki/sime zao ndo kabisa wanaonekana wa ukweliii.
Pamoja na kwamba nimewahi kuishi nao miaka ya nyuma, sikuwahi kujua baadhi ya mila zao juu ya maisha ya kila siku na namna yanavyoendeshwa ila sasa nimejua na ndio nikapata maswali kadhaa juu ya wanaume hao.
Kwanza kabisa hawajengi. Anaejenga ni mwanamke (mke/wake zake), na ole wao mvua inyeshe alafu bwana anyeshewe. . . lazima mama aambulie kibano na aeleze kwanini 'bwana inyeshewe'( in a Massai accent).
Pili chakula anatafuta mama.
Kutwa nikiangalia naona wanawake ndio wanaopita na punda + madumu kwenda kutafuta maji na kuni wanakokujua wao.
Wanaume utawaona wanapita fimbo zao + mbuzi na ng'ombe kupeleka machungani tu BASI. Wakija dukani wanaume wengi ni wanaulizia kiroba na beer. . . wachache sana watataka chumvi, sukari, mafuta, mchele au hata pipi za watoto kuashiria anakumbuka na kujali familia.
Mashine (kusaga na kukoboa) wanaokuja ni wanawake. . .
Kukamua wao. . .
Kupika wao. . .
Malezi wao. . .
Yani wanaume wao ni machungani kwenda kupiga soga huko wakati wamama wanapanda na kushuka na barabara. Kwa ufupi. . .wanalelewa na kutunzwa na wake zao.
Je nao ni wanaume? Au ndo sawa na wale wanaoitwa 'MARIO' mjini? Au yeye sio muAfrika hivyo ule utamaduni wa 'mwanaume wa kiAfrika ni provider' hauwahusu?