Narudia tena Mungu atakupa anaefanana na wewe.
May be mimi chaguzi zangu nina hisia kali
Humu kuna mkaka he is super nikisema super namaanisha, na si hawa wanaishi sinza na meru, ni wale wanaokula maisha, kama ni ulaya kaishi ulaya kweri kweriiiii hana maisha ya kuigiza narudia tena he is super. He his just a friend.northing else.
Sasa wewe dia tueleze hapa chaguzi zako ziko vipi?
Una vigezo gani vya kuprove kuwa unaekwenda kumpa no ni mwanaume unaemtaka?
Sio kila utitili unakuja pm unaukubali utitili mwengine ni wa kukuambukiza umasikini.
Ati mwanaume anajichibua? Huyo sio shoga kweli?
Natamani niwafundishe jinsi ya kujua mwanaume halisi humu jf ila nitapoteza tu muda wangu. Maana humu kuna watu lengo lenu ni kupata mwanaume hamna vigezo vingine.
....................................
1:Simply mtu akikufata pm jiulize alijiunga humu lini?
2: Je unahisi ana umri gani?
So nyuzi zake +posts zake kuanzia 2008 to date, kama huwezi zisoma basi bebana na huo utitili wa kuomba vocha.
4: tenga week nzima.kabla hujamjibu soma comments zake hutokosa jibu, kuna sehemu utagundua alishaelezea maisha yake hata kwa ufupi.
5: soma kwa makini nyuzi zake alizozianzisha, mwanaume wa maana hanaga nyuzi za kujua harmonise kaachana na kajala, wema na kile kitoto huwezi kukuta kaanzisha uwo uzi.
6: HAWEZI KUWA ANACOMMENT HOVYO HOVYO.
7. Kwa mara chache sana anacoment nyuzi za matukio eg ndege precision kuanguka bukoba atachangia kwa ufupi
8.kwenye siasa hawezi kuchangia sijui vijana wa ccm na chadema wanafanya upuuzi upi. Mara chache atachangia vitu muhimu vya kitaifa kwa ufupi sana
9: anapendelea jukwaa gani? Huwezi mkuta anachangia eti uzi wa kimasihara na ikitokea alichangia basi ni sentensi moja tu.
10. Kama anaishi ulaya muulize nchi gani? Akikwambia angalia time diference ya hiyo nchi na huku tz, then ulinganishe anachangiaga humu muda gani.?
11.kama kweli anaishi ulaya nyuzi alizoanzisha yeye kama alijiunga 2010 haziwezi zidi 10 na comments kama 387 kwa miaka 12 tho hapa inategemea anaweza asiwe na uzi alouanzisha ila coments zake ni chache. Tho hapa kuna option anapendelea kuchangia nini kama anapenda mpira lazima comments zake ziwe nyingi.
Etc etc etc etc
..................
Usione uvivu kumchunguza mtu anaetaka kuingia kwenye maisha yako.
Nimalize kwa kusema hivi humu jf ndo kuna wanaume wa maana kwa nyie ambao mnatafu, kuna wanaume wana pesa chafu, wasafi wana ndiga za maana wana maisha halisi lakini dada hawawezi ingia kwenye maisha yako kwa sababu wewe huna standards.
Huna standards kwa maana ipi?
Hauko real
Kuna wakati unachangia ujinga ukijuwa hufatiliwi.
Dada ukifatwa pm unaruhusu mazoea na usio wajua je umesahau humu watu wana id hata tatu? Leo kaja na hii kesho kaja na ile?
Kama unahisi huyo mwanaume sio mwambia sikuhitaji usikubali kumpa no yako wakati bado una wasiwasi.
Nb nilichokiandika hakimulengi muanzisha mada ni kwa yeyote atakaeona akisoma kitamsaidia.