Wanaume tuheshimiane

Wanaume tuheshimiane

Status
Not open for further replies.
Kuwa mshenga sio kazi ndogo. Kikinuka unaambiwa unaanzia kwa wasimamizi wa ndoa...kisha mshenga....then ndio wazazi.

Sasa mshenga inabidi anunue smartphone ili atumiwe screenashot za matusi ili akusanye ushahidi

Hahahhah...lol
 
Asieee dada wewe unamoyo sijui au huna akili?
Samahani kama nitakuwa nimekukwaza kwa kusema hivyo ila tangu lini ukaona jogoo na vifaranga? lini wapi na nsaa ngapi? Kwanini ukamwacha mwanao angali mdogo? kwani wewe huna pakulala huna chakula huna wazazi? Your first priority should have been your child tangu ulipoamua kubeba mimba jukumuu la malezi sio la mwanaume dada yangu jamanii.... Hivi huyu mtoto akibakwa,(kwanza utajuaje huyu anaemtawaza kama hamwingii vidole) je utamlaumu nani baba yake? Wewe ndio utakuwa wa kulaumiwa na jamii hata mtoto, mtetea na vifaranga dada ......

Utaachaje mtoto kwa baba alaf kabisa unatuma ndugu zako kabisaa unaona ni sawa kuongeanae kwenye simu tuu? JUA mdogo wako wewe, furaha na fajara atakayo pata mtot0 kukuona wewe na ukamkumbatia au kumpa busu kucheza nae ni tofauti na anayopata kwa ndugu zako. Najiulizamaswali kadhaa;
Huyu mtoto lini atajua mapenzi ya mama?
Lini atajua joto la mama yake na thamani ya neno " MAMA"?
Ni lini utamkuza huyu mtoto katika njia impasayo na nani atamwombea mtoto na kukesha nae?
Atasimilia nini watoto wake kuhusu mama yake?
Je! akikua nayeye si ataona fresh tuu kuzaa na kuacha watoto kwa manaume?
Kesho ukimkuta njiani akikutukana utaumia?
ATAJUA WAPI UPENDO WA MAMA?
Kamchukue mtoto tafadhali ni kosa kubwa kumwachia mtoto mwanaume tena asie jali kama huyu wako maana angalau hata angekuwa baba bora, yaani mtu mwenyewe bora baba alaf unampa mtoto? Mtu asiejua thamani asie na heshima kwa mwanamke alaf mbaya zaidi ndugu zake hawakupendi sasa unafikiri wana mda wakuangalia huyu mtoto wako?wampende kwa lipi hasa?
Mwanamke kamii mwanamke anae jua wajibu wake haachi watoto nyuma wala kuwagawa kama pipi.

FIGHT FOR YOUR CHILD USIKUBALI AKAE MBALI NAWEWE

Dada beba mwanao kama umeamua kuachana Na huyo mwanaume...unakaa kabisa unakula chakula kinashuka hujui mtoto wako amekula nini...anaumwa...amekumiss... Duuhh tunatofautiana roho!!

Kwa sasa siwezi kukaa nae, nipo masomoni ndio sababu kubwa ya kumwachia, anafahamu na hata ustawi wa jamii walimwambia mwakani mtoto lazima nimchukue, ivo kwa sasa sina tatizo na yeye kukaa nae, tatizo ni yeye kutumia matusi na jazba bila sababu.
 
Nadhani ni hasira tu lakini still you love the person, nakupa another year uje kutupa mrejesho hapa kama hajakuongezea mtoto wa pili huko huko ulipo. Mi watu walio vuana kyupi huwa sishauri ....tena for seven years mnavurumishana.... mmmh haya sie tupo yetu macho.
 
Hahahahahaj
Hayo magroup yote siyataki kasoro hilo la ma-admins.....mnipe u-invisible wa huko



Haha sio lazima group hilo tu. Nina ma-group mengi sana. Kuna group la "wapendwa" (imebaki nafasi moja tu, ya kwako). Kuna group la "warubuniwaji"(pia kuna nafasi yako). Kuna group la "wasio na group"(how ironic, right?). Kuna group la "admins" wote. Pia tunaweza kuanzisha la "kubadili tabia". Kazi kwako tu.
 
Kwa sasa siwezi kukaa nae, nipo masomoni ndio sababu kubwa ya kumwachia, anafahamu na hata ustawi wa jamii walimwambia mwakani mtoto lazima nimchukue, ivo kwa sasa sina tatizo na yeye kukaa nae, tatizo ni yeye kutumia matusi na jazba bila sababu.

Mmhhh ngumu sana kumeza!!
 
Kwa sasa siwezi kukaa nae, nipo masomoni ndio sababu kubwa ya kumwachia, anafahamu na hata ustawi wa jamii walimwambia mwakani mtoto lazima nimchukue, ivo kwa sasa sina tatizo na yeye kukaa nae, tatizo ni yeye kutumia matusi na jazba bila sababu.


KWA HIYO SIO TATIZO KWA MTOTO WAKO WA KIKEE KUOSHWA SEHEMU ZAKE ZA SIRI NA MWANAUME? TENA MTU BAKI?

OOOOKAAAAAAY!! Basi atazidi tu kukutukana saana tuu.

Kama baba yako aliweza kumzuiaaikuoe basi asingeshindwa kumzuia kufanya fujo kama mtoto angekaa kwenu
SIO TATIZO KWA MTOTO WAKO KULALA NA KIJANA WA MIAKA 24?
 
Hayo matusi na jazba vipeleke polisi.
Sms si unazo???????
Mbona ni ushahidi wa kutosha?????



Kwa sasa siwezi kukaa nae, nipo masomoni ndio sababu kubwa ya kumwachia, anafahamu na hata ustawi wa jamii walimwambia mwakani mtoto lazima nimchukue, ivo kwa sasa sina tatizo na yeye kukaa nae, tatizo ni yeye kutumia matusi na jazba bila sababu.
 
Hahahahahaj
Hayo magroup yote siyataki kasoro hilo la ma-admins.....mnipe u-invisible wa huko

Hilo tu? Inabidi tukuchunguze kwanza kama wewe ni liability, au asset. Meanwhile, itisha mkutano na waandishi wa habari na ujibu tuhuma zote walizonazo juu yako na za utendaji wako kwa ujumla.
 
Nimependa huu msemo: "Act like you trust people, but don't"
 
KWA HIYO SIO TATIZO KWA MTOTO WAKO WA KIKEE KUOSHWA SEHEMU ZAKE ZA SIRI NA MWANAUME? TENA MTU BAKI?

OOOOKAAAAAAY!! Basi atazidi tu kukutukana saana tuu.

Kama baba yako aliweza kumzuiaaikuoe basi asingeshindwa kumzuia kufanya fujo kama mtoto angekaa kwenu
SIO TATIZO KWA MTOTO WAKO KULALA NA KIJANA WA MIAKA 24?


Maneno mazito aya, yameniuma mpaka kumoyo, dah Chitikita, think twice if not tripled
 
Kwani wakati mnaanza mlianzia jf?Umetuchosha na habari yako.Hapo ww nenda kwa mwenzako bado anakupenda.
 
na wewe kweli mvumilivu,,,, miaka 7 mnafanyaga matusi tuuu....pole mama....angalau aliweza kulenga ka1, la sivyo wala usingeahangaika kuja hapa....pole mweeee
 
Dada beba mwanao kama umeamua kuachana Na huyo mwanaume...unakaa kabisa unakula chakula kinashuka hujui mtoto wako amekula nini...anaumwa...amekumiss... Duuhh tunatofautiana roho!!

huyu mwanadada Mimi nimemuelewa..

Hana pesa ya malezi ya mtoto na yupo shule kwa sasa...

Ni kweli hafurahishwi na jinsi mtoto wao anavyolelewa lakini atafanyaje sasa...?

Kulea mtoto vilevile kunahitaji commitment na mambo mengi Tu ya zaida...mzazi mwenzie yupo vizuri kiuchumi ndo maana hata alikubali kumuachia mtoto Mara ya kwanza amlee..

kwangu Mimi huyu mwanamke Ni mpumbavu.

alipomuacha mtoto wake kwa huyu jamaa mlevi alitegemea nini? Haya yanayotokea Ni lazima yalikuwa yatokee na aliyajua kabisa....ila anajitoa ufahamu hapa kwa kutafuta sympathy ya wana jukwaa hapa,..


Pengine huko anakosoma kashampata mtu mwingine na kamdanganya Hana mtoto....

wewe mtu Una akili timamu mwanamke umejifungua mtoto Wako kwa uchungu unamuacha mtoto wa kike wa miaka mitano aishi kwa Baba mlevi...??

kweli?


Nyie wanawake mlipewa uwezo finyu Sana wa kufikiria.


Stupid
 
Naomba kusema, wanaume tuheshimiane tena tuheshimiane, tabia ya kuachana na mwanamke lakini huishi kumfuata fuata kwa maneno jiheshimu tena jiheshimu.

Nimechoka na nimekuchoka ndio maana nimekuja kukuambia hapa, kwa kuwa ni member hapa najua utasoma na unajua mimi ni nani.

Nimechoka kukunyamazia, mwanaume gani unakosa busara hata chembe tu? jiheshimu narudia tena jiheshimu.

Huyu mtu mimi nilikuwa kwenye mahusiano nae yapata miaka 7 na tuna mtoto mmoja alikua amefanya taratibu zote za kufunga ndoa isipokuwa tulikuwa bado kufunga ndoa tu.

Tukaja tukashindwana kila mtu akaendelea na maisha yake, wakati wakuvunja mahusiano mimi kama mtu ambaye nilihisi kuchoka.

Niliifahamisha familia yangu na nilitoa sababu zangu ambazo kwa upande wa familia waliamua kumwambia mshenga.

Basi mshenga akapewa taarifa na kwakua mshenga alikuwa anajua habari za huyu mtu wangu vizuri alieleza mengi pia kwa familia yangu hasa ambayo hata mimi sikutaka familia wayajue.

Kutokana na taarifa hizo baba yangu akikasirishwa sana na kuniomba kikao cha pande mbili.

Tulikutana kwenye kikao wazazi wake wakaongea na yeye akaongea, na mimi nikaongea na mshenga akaongea khaa!

Jambo la ajabu yeye akasema "jamani naomba mimi na mwenzangu tutaenda kuyaongea" khaa!

Baba yangu akahamaki na kumwambia kuanzia leo nauvunja huo uhusiano, wewe kajirekebishe na huyu akasome.

Baada ya hapo kama utakuwa umejirekebisha mlango upo wazi nitakukaribisha, kuanzia leo mwanangu yupo chini yangu. tukafunga kikao.

Baada ya hapo yeye alinibembeleza sana nisiachane nae kwakua tuna mtoto na aliahidi angejirekebisha, na mimi roho ilikuwa inaniuma kuhusu mtoto.

Nikawa najitahidi kuwa karibu nae kwakua mtoto nilimwachia yeye mimi nilienda kukaa sehemu nyingine ambayo sikutaka kabisa yeye aijue maana namjua vizuri lakini sikuacha kila wkend kwenda kumuona.

Sasa shida sikuwahi kuona mabadiliko kwa zaidi ya miezi 8, kwanza kila siku ilikuwa afadhali ya jana, mwanaume mgomvi, anamatuasi yaani akilewa ananivua nguo kwa maneno mchana kweupe.

Nikaamua kukaa kimya kwa muda ila mtoto nilikuwa nawatuma wadogo zangu wanaenda kumuona na kumpelekea vitu vya mtoto.

Baada ya muda nikawa nikipiga simu kutaka kuongea na mtoto, hapokei, yaani zaidi ya mwezi simu haipokelewi wala msg hajibu.

Nikaamua kumpeleka ustawi kudai haki yakumuona na kuongea na mtoto, kumbe bwana huyu akavuta jiko wakawa wanaishi wanapika na kupakua.

Kilichofuata ni ndugu zake kunishambulia mimi nakusahau mema yote niliyokuwa nawatendea, kwakua tulichokanaa hiyo siku yeye kaja na timu toka kwao, mimi peke yangu, tukatukanana mbele ya polisi hadi basi, baada ya siku mbili akanipigia simu mimi 'eti niende nikawaombe msamaha ndugu zake kwa kua yeye hataki kuachana na mimi" nikamuuliza kwa lipi?

Eti umewatukana wazazi wake hawana kazi za kufanya, nikamwambia usinitafute maneno, na hilo haliwezekani kamwe, akawa ananitukana sana kwa msg kuna wakati hadi najikuta namjibu.

Nikaa kama mwezi, akaanza tena kunipigia "Ooohh! naomba turudiane," nikamwambia wewe si umeoa?

Akasema mimi naishi tu na huyu mwanamke lakini sina mapenzi wala malengo nae" nikamwambia endelea kuchezea watoto wa watu, huo ni uchafuzi, kuhusu mimi sahau sahau.

Baada ya hapo akaa kimya cha muda lakini jambo la ajabu kaanza tena kunitukana sana kwa msg, kiasi kwamba sielewi ana tatizo gani?

Mimi naishi naendelea na maisha yangu kwa amani lakini yeye kila siku anaishi anawaza kukabiliana na mimi, mimi nimekuchoka na hizi tabia.

Wewe kaa ishi kwa amani yako, niache na mimi niwe na amani yangu, Nilikupa nafasi miaka 7 tena kwa uaminifu mkubwa, uliyoyafanya unayajua vizuri sasa tulia, "usiweweseke kujua kuhusu mimi" na lazima ujue naishi maisha mapya SITAKI STRESS TENAAAA,

Nimekuchoka najua utapita hapa, soma ukimaliza nenda kawasimulie waliokudanganya ukakosa mwana na maji ya moto.

ndoa zote zilizofanikiwa na kudumu katika dunia hii ni zile ambazo kila mwenza alijifunza kustahimili mapungufu ya mwenzake na si vinginevyo.si mapenzi wala mahaba yanayodumisha ndoa,ni uvumilivu wa mapungufu au udhaifu wa mwenza hii ni kutokana kuwa kila mwanadamu ana mapungufu.hata wewe ulipo hapo una yako.tatizo kubwa katika mahusiano ya siku hizi ni pale ambapo mtu anataka fikra zake ziwe reality katika mahusiano.yaani anawaza kupendwa,kudekezwa,kuabudiwa etc etc wakati in reality ni vitu ambavyo mwenza hawezi kuvikamilisha kwa 100% kwani na yeye ni binadamu ana hisia zake na mapungufu yake.Mungu hawezi kukuletea almasi katika sahani ya dhahabu.atakupa wa kufanana nae ndipo sasa muanze ku adjust katika maisha yenu.

kumbuka kuwa mabadiliko hayana muda,mtu anaweza kubadilika akiwa 40 au 45 na ukaenjoy ndoa sana kuliko ilivyo sasa kwani bado wabichi na mihemuko ni mingi.katika mahusiano lazima mjipe nafasi ya kukua na kuwa watu wazima.

kwa maoni yangu ni kwamba huyo ndiyo alikuwa chaguo lako sahihi,ni basi tu wote kwa pamoja mmeshindwa kuwa wavumilivu wa kutosha ili muweze kufikia kule mlikokwenda.
 
huyu mwanadada Mimi nimemuelewa..

Hana pesa ya malezi ya mtoto na yupo shule kwa sasa...

Ni kweli hafurahishwi na jinsi mtoto wao anavyolelewa lakini atafanyaje sasa...?

Kulea mtoto vilevile kunahitaji commitment na mambo mengi Tu ya zaida...mzazi mwenzie yupo vizuri kiuchumi ndo maana hata alikubali kumuachia mtoto Mara ya kwanza amlee..

kwangu Mimi huyu mwanamke Ni mpumbavu.

alipomuacha mtoto wake kwa huyu jamaa mlevi alitegemea nini? Haya yanayotokea Ni lazima yalikuwa yatokee na aliyajua kabisa....ila anajitoa ufahamu hapa kwa kutafuta sympathy ya wana jukwaa hapa,..


Pengine huko anakosoma kashampata mtu mwingine na kamdanganya Hana mtoto....

wewe mtu Una akili timamu mwanamke umejifungua mtoto Wako kwa uchungu unamuacha mtoto wa kike wa miaka mitano aishi kwa Baba mlevi...??

kweli?


Nyie wanawake mlipewa uwezo finyu Sana wa kufikiria.


Stupid

Chukua like magnificent...!!
 
Evelyn Salt sikumuacha tu ati mim nakula maisha hapana, nilimwachia kwa kua nipo masomoni, mwanzo nilitaka niwaachia wazazi wangu lakini anatabia ya ugomvi sana so nikamwachia yey hata hvyo yey anaishi kwa wazazi wake mara nyingi ila ndio hvo. Ila mwakani nitamchukua.

Poa mwaya, pole......
 
aaaahhhh kwahiyo umeona ukileta huku ndio itakusaidi?
sasa kwa taarifa yako mtoto nampeleka kijijini akasome huko huko na ukitaka kujua hali yale uwe unakuja kuuliza jamii forum
 
Asieee dada wewe unamoyo sijui au huna akili?
Samahani kama nitakuwa nimekukwaza kwa kusema hivyo ila tangu lini ukaona jogoo na vifaranga? lini wapi na nsaa ngapi? Kwanini ukamwacha mwanao angali mdogo? kwani wewe huna pakulala huna chakula huna wazazi? Your first priority should have been your child tangu ulipoamua kubeba mimba jukumuu la malezi sio la mwanaume dada yangu jamanii.... Hivi huyu mtoto akibakwa,(kwanza utajuaje huyu anaemtawaza kama hamwingii vidole) je utamlaumu nani baba yake? Wewe ndio utakuwa wa kulaumiwa na jamii hata mtoto, mtetea na vifaranga dada ......

Utaachaje mtoto kwa baba alaf kabisa unatuma ndugu zako kabisaa unaona ni sawa kuongeanae kwenye simu tuu? JUA mdogo wako wewe, furaha na fajara atakayo pata mtot0 kukuona wewe na ukamkumbatia au kumpa busu kucheza nae ni tofauti na anayopata kwa ndugu zako. Najiulizamaswali kadhaa;
Huyu mtoto lini atajua mapenzi ya mama?
Lini atajua joto la mama yake na thamani ya neno " MAMA"?
Ni lini utamkuza huyu mtoto katika njia impasayo na nani atamwombea mtoto na kukesha nae?
Atasimilia nini watoto wake kuhusu mama yake?
Je! akikua nayeye si ataona fresh tuu kuzaa na kuacha watoto kwa manaume?
Kesho ukimkuta njiani akikutukana utaumia?
ATAJUA WAPI UPENDO WA MAMA?
Kamchukue mtoto tafadhali ni kosa kubwa kumwachia mtoto mwanaume tena asie jali kama huyu wako maana angalau hata angekuwa baba bora, yaani mtu mwenyewe bora baba alaf unampa mtoto? Mtu asiejua thamani asie na heshima kwa mwanamke alaf mbaya zaidi ndugu zake hawakupendi sasa unafikiri wana mda wakuangalia huyu mtoto wako?wampende kwa lipi hasa?
Mwanamke kamii mwanamke anae jua wajibu wake haachi watoto nyuma wala kuwagawa kama pipi.

FIGHT FOR YOUR CHILD USIKUBALI AKAE MBALI NAWEWE

huyu mwanadada Mimi nimemuelewa..

Hana pesa ya malezi ya mtoto na yupo shule kwa sasa...

Ni kweli hafurahishwi na jinsi mtoto wao anavyolelewa lakini atafanyaje sasa...?

Kulea mtoto vilevile kunahitaji commitment na mambo mengi Tu ya zaida...mzazi mwenzie yupo vizuri kiuchumi ndo maana hata alikubali kumuachia mtoto Mara ya kwanza amlee..

kwangu Mimi huyu mwanamke Ni mpumbavu.

alipomuacha mtoto wake kwa huyu jamaa mlevi alitegemea nini? Haya yanayotokea Ni lazima yalikuwa yatokee na aliyajua kabisa....ila anajitoa ufahamu hapa kwa kutafuta sympathy ya wana jukwaa hapa,..


Pengine huko anakosoma kashampata mtu mwingine na kamdanganya Hana mtoto....

wewe mtu Una akili timamu mwanamke umejifungua mtoto Wako kwa uchungu unamuacha mtoto wa kike wa miaka mitano aishi kwa Baba mlevi...??

kweli?


Nyie wanawake mlipewa uwezo finyu Sana wa kufikiria.


Stupid


Aisee!!!!!!!!!

Sikiliza nikwambie, isiishi kwakuongozwa na hisia,

Sitaki kutenda dhambi, baba yake mtoto anampenda mtoto wake kuliko unavyofikiria, kwa hilo sina shaka, tatizo mtoto analelewa kwao na yeye yupo hapo kwao sababu anawaangalia pia wazazi wake, tatizo ni waangalizi wa mtoto pale yeye anakuwa kazini na pia nadhani hata familia inatokea kuaminiana ndio maana mtoto anaweza kuachiwa mtoto wa kiume wao wakaona sawa, na ukisema unaonekana unawangilia, zaidi hana shida kabisa na mtoto na muda mwingi huwa na mwanae.

Mimi silalamiki yeye kuwa mtoto, kwakua ni jambo ambalo sina shaka nalo na soon litakuwa ndani ya uwezo wangu. ila ninalalamikia msg za matusi tu. nadhani umeelewa sasa.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom