Nimelisha anzisha jaribu kuwa nawatuma wadogo zangu kwenda kumuona mtoto na hata kumchukua, akawa analalamika kwa watu mimi siendi kumuona mtoto wala sipigi sim, pia walikua wanawatreat vibaya sana wadogo zangu wakienda pale, yaani kuna wakati nilibadili line hadi nikahisi kuchanganyikiwa.
Nawaza pia hilo, japo sioni njia rahisi kwa kweli
Unajua hua sipendi hata kumpigia hata hivyo hua simpigii hadi niwe namuhita mtoto, kwa hiyo inaweza kupita hata wiki 3 mimi sijui mwanangu anaendeleaje, Lakini pia inanilazimu kumfuatilia maana ni mtoto wa kike n kuna mambo nikiyafikiria huwa nakosa amani kabisa.
mfano, kunasiku nilimuuliza mtoto nani anakusafisha ukienda chooni?? mtoto akanijibu anasafishwa na kaka wa ng'ombe(mfanyakazi wa ng'ombe) nikampigia nikamwambia kwanini mtoto anasafishwa na kaka wa ng'ombe?? hakuonyesha kujali hata kidogo, aliona ni kawaida tu, lakini mimi nilishamfundisha mwanangu kujitegemea kwa kila kitu, sasa sijui ilikuwaje hadi kumruhusu kaka wa ng'ombe kumsafisha mtoto wa kike.
Zaidi wakati mwingine wanaruhusu mtoto wa kike eti alale na baba ake mdogo mwenye umri wa miaka kama 23 au 24 jamani hebu niambieni kweli hawa watu wanaakili kweli???????
Kwakweli moyo wangu una maumivu sana nikifikiria hayo na nipo kwenye mkakati wakuomba nimchukue na niondoke nae mbali kabisa.
Asieee dada wewe unamoyo sijui au huna akili?
Samahani kama nitakuwa nimekukwaza kwa kusema hivyo ila tangu lini ukaona jogoo na vifaranga? lini wapi na nsaa ngapi? Kwanini ukamwacha mwanao angali mdogo? kwani wewe huna pakulala huna chakula huna wazazi? Your first priority should have been your child tangu ulipoamua kubeba mimba jukumuu la malezi sio la mwanaume dada yangu jamanii.... Hivi huyu mtoto akibakwa,(kwanza utajuaje huyu anaemtawaza kama hamwingii vidole) je utamlaumu nani baba yake? Wewe ndio utakuwa wa kulaumiwa na jamii hata mtoto, mtetea na vifaranga dada ......
Utaachaje mtoto kwa baba alaf kabisa unatuma ndugu zako kabisaa unaona ni sawa kuongeanae kwenye simu tuu? JUA mdogo wako wewe, furaha na fajara atakayo pata mtot0 kukuona wewe na ukamkumbatia au kumpa busu kucheza nae ni tofauti na anayopata kwa ndugu zako. Najiulizamaswali kadhaa;
Huyu mtoto lini atajua mapenzi ya mama?
Lini atajua joto la mama yake na thamani ya neno " MAMA"?
Ni lini utamkuza huyu mtoto katika njia impasayo na nani atamwombea mtoto na kukesha nae?
Atasimilia nini watoto wake kuhusu mama yake?
Je! akikua nayeye si ataona fresh tuu kuzaa na kuacha watoto kwa manaume?
Kesho ukimkuta njiani akikutukana utaumia?
ATAJUA WAPI UPENDO WA MAMA?
Kamchukue mtoto tafadhali ni kosa kubwa kumwachia mtoto mwanaume tena asie jali kama huyu wako maana angalau hata angekuwa baba bora, yaani mtu mwenyewe bora baba alaf unampa mtoto? Mtu asiejua thamani asie na heshima kwa mwanamke alaf mbaya zaidi ndugu zake hawakupendi sasa unafikiri wana mda wakuangalia huyu mtoto wako?wampende kwa lipi hasa?
Mwanamke kamii mwanamke anae jua wajibu wake haachi watoto nyuma wala kuwagawa kama pipi.
FIGHT FOR YOUR CHILD USIKUBALI AKAE MBALI NAWEWE