Wanaume tuheshimiane

Wanaume tuheshimiane

Status
Not open for further replies.
Dah pole but kama kuna liwezekanalo mchukue mwanao ban nae
"mama tu" ndo anauwezo wa kumpa mwanae "kila kitu na kwa uhakika zaidi"
Evelyn Salt sikumuacha tu ati mim nakula maisha hapana, nilimwachia kwa kua nipo masomoni, mwanzo nilitaka niwaachia wazazi wangu lakini anatabia ya ugomvi sana so nikamwachia yey hata hvyo yey anaishi kwa wazazi wake mara nyingi ila ndio hvo. Ila mwakani nitamchukua.
 
Last edited by a moderator:
Kisa cha kuja kunitukana hapa ni nini? sasa Dawa yako najiua tuone utafaidika nini.....Mtakao baki duniani siku ya uchaguzi chagueni Lowasa, mwambieni kura moja imepotea kizembe kabisa

Ngoja kwanza ucfanye maamuzi kabla hujanipm ili nikupe mkasa wangu ngd plzzzzzzzzz


Kampeni.nackiliza lkn kura yetu mimi na ww unaesoma hapa kwa El mwana UKAWA
 
Yes Lizzy

Hawa baba na mama wa huyo binti wote nadhani hawana muda wa malezi ya mtoto.

Heri wampeleke kwa bibi/ babu wa upande wowote ambao mtoto atakuwa salama. Kisha waendelee kuonyesheana ubabe.

Si rahisi kama unavyofikiria kwanza kwa wazaz kuachana, ukiona hyo ujue hali ilishindikana kabisa.

Hata hvyo mtoto yupo kwa wazazi wake, kwa kua hata yeye anakaa kwao muda mwingi, mim sina tatizo nae kikubwa mtoto ninapomuhtaj nimpate, ila sio mambo ya matusi wakati kila mtu anaendelea na maisha yake.
 
lazima nyie ni watoto wa uswazi.
Pia umri wenu ni mdogo

Kuhusu kuwa watoto wa uswaz inawezekana.

Ila kiumri sio watoto kama uwazavyo, hata wew ni mdogo sana kwangu achilia yeye aliyekuacha maaka zaidi ya 10, nimekwambia hayo kwakua nakufahamu vizuri sana.
 
BADILI TABIA unampa mtu ushauri ambao hauhitaji na japo huyo baba mtu pengine anastahili lawama kwa kiasi fulani lakini sio kwa asilimia zote kwasababu pengine hayo yanapotokea (mf. mtoto kusafishwa) yeye anakuwa hayupo. Na huyu mwenzie (MTOA MADA na MLALAMIKAJI MKUU) hafanyi lolote kusaidia hiyo situation. Anaishia kulalamika bila kufanya kile ambacho kwa maoni yake ni sahihi/bora zaidi.

#Amesema YEYE ndo aliyemuachia mwanaume mtoto. Sasa kama alijua hatopata malezi mazuri huko au ana wasiwasi kwanini alimuacha huko?
#Amesema alienda ustawi wa jamii kulalamika kuhusu kunyimwa kumuona mtoto, sio kumchukua ila kumuona.
Sasa anatakaje? Mtu utakaaje pembeni ukilalamika "ohh mtoto wa kike anasafishwa na kijana, mtoto wa kike analala na baba mdogo" huku ukiendelea kuishi maisha yako bila kujali kwamba malezi ya bintiye ni jukumu lake pia? Anaonekana ni mtu mlalamishi ambae ha-take responsibility kwa lolote lile. Ye anaona anaonewa tu.

Kaka usiongee kirahisi, sikumuacha mtoto kwakua nataka kujiachia, niliyajua yote hayo na nilipiga moyo konde kwamba sina namna, Nilimwacha kwake kwakua nipo masomoni sasa mlitaka mim nifanyeje??? Hata ningeweza kumpeleka kwetu ila najua huyu mwanaume angekwazana na wazazi wangu tu, hasa ukizingatia wazazi wangu wapo mbali sikutaka kuleta sintofahamu.
 
Last edited by a moderator:
Jamaa anakusumbua kwa kua anakumbuka sana kitumbua cha ngano a.k.a Mpunyenye a.k.a Mpododo
 
Mbona masharti magumu hivi????

Nitaghairi mie



Hahaha. Japo hili ni tusi, tutakufikiria mpendwa. Meanwhile, kati ya vigezo vya kuwa mwanachama ni pamoja na 1. Uwe na certificate of good conduct, kutoka Interpol. 2. Uwe na uwezo wa kutumia urinals 3. Uwe na uwezo wa kurubuniwa 4. Uwe na serikali mbili (vichwa viwili).

Masharti mengine tutayajadili baada ya kutimiza hayo.
 
Turudi kwenye maada sasa
kwa historia fupi uliyotoa hapa naweza sema Jamaa bado anakupenda Sana na bado anahisia na wewe lakini tatizo lake kubwa ni pombe zake ambazo humtoa akili na ufahamu na bado anakumbuka mema mengi yako na kila akumbukapo lazima nafsi yake ijute na aanze kukusumbua sana, wewe kuandika hapa ni vyema lakin umemuongezea hasira pia na njia Bora nakushauri ufuate utaratibu hasa kwa wazazi wa pande zote ili yaishe kwani mahusiano ya namna hii hua hayaishi visasi na zaidi hupelekea hadi vifo kwani mwisho akikukosa anaona bora mkose nyote.
 
Katika mahusiano pamoja na mifarakano inabidi tuisisitize amani baina yetu kwani unaweza kukuta jamaa toka umuwache hawezi kufikiria maisha mengine na hawezi kuwaza zaidi ya pale isipokua kunywa pombe tu ili ajiliwaze, japo nimekusoma katikati ya mistari wewe pia ni Mbabe na unapenda ligi sana na huyo jamaa
 
Mbona masharti magumu hivi????

Nitaghairi mie

Haha sio lazima group hilo tu. Nina ma-group mengi sana. Kuna group la "wapendwa" (imebaki nafasi moja tu, ya kwako). Kuna group la "warubuniwaji"(pia kuna nafasi yako). Kuna group la "wasio na group"(how ironic, right?). Kuna group la "admins" wote. Pia tunaweza kuanzisha la "kubadili tabia". Kazi kwako tu.
 
Kwa sasa fuatilia ustawi (ingawa ustawi wetu majanga matupu) mtoto atoke hapo. Mazingira ya sio mazuri kwa mtoto


Kaka usiongee kirahisi, sikumuacha mtoto kwakua nataka kujiachia, niliyajua yote hayo na nilipiga moyo konde kwamba sina namna, Nilimwacha kwake kwakua nipo masomoni sasa mlitaka mim nifanyeje??? Hata ningeweza kumpeleka kwetu ila najua huyu mwanaume angekwazana na wazazi wangu tu, hasa ukizingatia wazazi wangu wapo mbali sikutaka kuleta sintofahamu.
 
Kuhusu kuwa watoto wa uswaz inawezekana.

Ila kiumri sio watoto kama uwazavyo, hata wew ni mdogo sana kwangu achilia yeye aliyekuacha maaka zaidi ya 10, nimekwambia hayo kwakua nakufahamu vizuri sana.
Makubwaz.wengine mnajuana humu-wewe dada ni kosa kumwambia mtu unamfahamu humu,utasababisha member wakimbie JF-naomba uzingatie masharti
 
Kuna tatizo kwako pia wewe dada,kwa mtu anaejua kusoma lugha ya maandishi anaweza kukubaliana na mimi kwenye hili,wewe dada na wewe unaonekana ni mkorofi sana,unaonekana una lugha kali ya ubabe.
Anyway kwa kuwa umesema muhusika nae yupo hapa jamvini,ngoja tumsubiri nae aje atoe maelezo yake ili tuweze kutoa ushauri wa maana.ila na wewe ni chanzo cha huu mgogoro wenu wala usimsingzie huyo mshikaji.
 
Nimelisha anzisha jaribu kuwa nawatuma wadogo zangu kwenda kumuona mtoto na hata kumchukua, akawa analalamika kwa watu mimi siendi kumuona mtoto wala sipigi sim, pia walikua wanawatreat vibaya sana wadogo zangu wakienda pale, yaani kuna wakati nilibadili line hadi nikahisi kuchanganyikiwa.

Nawaza pia hilo, japo sioni njia rahisi kwa kweli




Unajua hua sipendi hata kumpigia hata hivyo hua simpigii hadi niwe namuhita mtoto, kwa hiyo inaweza kupita hata wiki 3 mimi sijui mwanangu anaendeleaje, Lakini pia inanilazimu kumfuatilia maana ni mtoto wa kike n kuna mambo nikiyafikiria huwa nakosa amani kabisa.

mfano, kunasiku nilimuuliza mtoto nani anakusafisha ukienda chooni?? mtoto akanijibu anasafishwa na kaka wa ng'ombe(mfanyakazi wa ng'ombe) nikampigia nikamwambia kwanini mtoto anasafishwa na kaka wa ng'ombe?? hakuonyesha kujali hata kidogo, aliona ni kawaida tu, lakini mimi nilishamfundisha mwanangu kujitegemea kwa kila kitu, sasa sijui ilikuwaje hadi kumruhusu kaka wa ng'ombe kumsafisha mtoto wa kike.

Zaidi wakati mwingine wanaruhusu mtoto wa kike eti alale na baba ake mdogo mwenye umri wa miaka kama 23 au 24 jamani hebu niambieni kweli hawa watu wanaakili kweli???????

Kwakweli moyo wangu una maumivu sana nikifikiria hayo na nipo kwenye mkakati wakuomba nimchukue na niondoke nae mbali kabisa.


Asieee dada wewe unamoyo sijui au huna akili?
Samahani kama nitakuwa nimekukwaza kwa kusema hivyo ila tangu lini ukaona jogoo na vifaranga? lini wapi na nsaa ngapi? Kwanini ukamwacha mwanao angali mdogo? kwani wewe huna pakulala huna chakula huna wazazi? Your first priority should have been your child tangu ulipoamua kubeba mimba jukumuu la malezi sio la mwanaume dada yangu jamanii.... Hivi huyu mtoto akibakwa,(kwanza utajuaje huyu anaemtawaza kama hamwingii vidole) je utamlaumu nani baba yake? Wewe ndio utakuwa wa kulaumiwa na jamii hata mtoto, mtetea na vifaranga dada ......

Utaachaje mtoto kwa baba alaf kabisa unatuma ndugu zako kabisaa unaona ni sawa kuongeanae kwenye simu tuu? JUA mdogo wako wewe, furaha na fajara atakayo pata mtot0 kukuona wewe na ukamkumbatia au kumpa busu kucheza nae ni tofauti na anayopata kwa ndugu zako. Najiulizamaswali kadhaa;
Huyu mtoto lini atajua mapenzi ya mama?
Lini atajua joto la mama yake na thamani ya neno " MAMA"?
Ni lini utamkuza huyu mtoto katika njia impasayo na nani atamwombea mtoto na kukesha nae?
Atasimilia nini watoto wake kuhusu mama yake?
Je! akikua nayeye si ataona fresh tuu kuzaa na kuacha watoto kwa manaume?
Kesho ukimkuta njiani akikutukana utaumia?
ATAJUA WAPI UPENDO WA MAMA?
Kamchukue mtoto tafadhali ni kosa kubwa kumwachia mtoto mwanaume tena asie jali kama huyu wako maana angalau hata angekuwa baba bora, yaani mtu mwenyewe bora baba alaf unampa mtoto? Mtu asiejua thamani asie na heshima kwa mwanamke alaf mbaya zaidi ndugu zake hawakupendi sasa unafikiri wana mda wakuangalia huyu mtoto wako?wampende kwa lipi hasa?
Mwanamke kamii mwanamke anae jua wajibu wake haachi watoto nyuma wala kuwagawa kama pipi.

FIGHT FOR YOUR CHILD USIKUBALI AKAE MBALI NAWEWE
 
Nimelisha anzisha jaribu kuwa nawatuma wadogo zangu kwenda kumuona mtoto na hata kumchukua, akawa analalamika kwa watu mimi siendi kumuona mtoto wala sipigi sim, pia walikua wanawatreat vibaya sana wadogo zangu wakienda pale, yaani kuna wakati nilibadili line hadi nikahisi kuchanganyikiwa.

Nawaza pia hilo, japo sioni njia rahisi kwa kweli




Unajua hua sipendi hata kumpigia hata hivyo hua simpigii hadi niwe namuhita mtoto, kwa hiyo inaweza kupita hata wiki 3 mimi sijui mwanangu anaendeleaje, Lakini pia inanilazimu kumfuatilia maana ni mtoto wa kike n kuna mambo nikiyafikiria huwa nakosa amani kabisa.

mfano, kunasiku nilimuuliza mtoto nani anakusafisha ukienda chooni?? mtoto akanijibu anasafishwa na kaka wa ng'ombe(mfanyakazi wa ng'ombe) nikampigia nikamwambia kwanini mtoto anasafishwa na kaka wa ng'ombe?? hakuonyesha kujali hata kidogo, aliona ni kawaida tu, lakini mimi nilishamfundisha mwanangu kujitegemea kwa kila kitu, sasa sijui ilikuwaje hadi kumruhusu kaka wa ng'ombe kumsafisha mtoto wa kike.

Zaidi wakati mwingine wanaruhusu mtoto wa kike eti alale na baba ake mdogo mwenye umri wa miaka kama 23 au 24 jamani hebu niambieni kweli hawa watu wanaakili kweli???????

Kwakweli moyo wangu una maumivu sana nikifikiria hayo na nipo kwenye mkakati wakuomba nimchukue na niondoke nae mbali kabisa.

Dada beba mwanao kama umeamua kuachana Na huyo mwanaume...unakaa kabisa unakula chakula kinashuka hujui mtoto wako amekula nini...anaumwa...amekumiss... Duuhh tunatofautiana roho!!
 
Mianaume mingine bwana, mxiuuuuuu!
 
Dada beba mwanao kama umeamua kuachana Na huyo mwanaume...unakaa kabisa unakula chakula kinashuka hujui mtoto wako amekula nini...anaumwa...amekumiss... Duuhh tunatofautiana roho!!

Mtoto ana umri gani?
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom